Diaspora tunadharaulika sana awamu hii

Diaspora tunadharaulika sana awamu hii

Awamu hii ya 5 imekuja kauli mbiu ya HAPA KAZI TU hata sijui waliitoa wapi hii kitu, haya sasa wameingia madarakani vurugu mechi kila mtu na wake FUKUZA FUKUZA kila kona, ukiangalia watueuliwa wote hakuna Diaspora hata mmoja. Jamani hii nchi ni ya kwetu wote mbona awamu ya 4 walitushirikisha kikamilifu? Hata ukienda Ubalozini (Washington DC) haupati ushirikaiano wa enzi zile za Awamu ya 4 maana kila mtu anatetemeka tu sijui ndo kuogopa fukuza fukuza! Tuajirini sisi Diaspora muone damu mpya na mawazo mapya katika utendaji wa serikalini nchi itanyooka.
Mkuu wewe peleka maoni yako pale panapohusika, mradi ni mtanzania naamini utasikilizwa tu.
 
huyo jamaa ameona kitu cha muhimu ni wao kupewa nafasi za uteuzi
waje hapa tusote halafu mchango wao ukionekana lazima watateuliwa tumeshaona wakina bilal walivyoifanya nchi hii
 
Rudini makwenu nyie awamu hii haina mchelea
 
Simlikua mkimzodoa JK leo kawa mtamu ee, subirini msahaulike kabisa
 
Serikali ya Magufuli ni vishindo na makeke,hatujui kinachoendelea,siku 100 nyingine labda ndio tutapata picha. Watu wamekuwa callous. Taifa linaweza kuadhibiwa. Mtu anaiba ndala anachomwa moto,wakati Mahakama zinajua jinsi ya kumuadhibu vizuri.
 
Awamu hii ya 5 imekuja kauli mbiu ya HAPA KAZI TU hata sijui waliitoa wapi hii kitu, haya sasa wameingia madarakani vurugu mechi kila mtu na wake FUKUZA FUKUZA kila kona, ukiangalia watueuliwa wote hakuna Diaspora hata mmoja. Jamani hii nchi ni ya kwetu wote mbona awamu ya 4 walitushirikisha kikamilifu? Hata ukienda Ubalozini (Washington DC) haupati ushirikaiano wa enzi zile za Awamu ya 4 maana kila mtu anatetemeka tu sijui ndo kuogopa fukuza fukuza! Tuajirini sisi Diaspora muone damu mpya na mawazo mapya katika utendaji wa serikalini nchi itanyooka.
Magufuli si yule mliyezoea mnabembea naye kisha mnamwandalia sherehe feki za kutunukiwa vyeti vya mtawala bora.
 
Tatizo wengi haja update mindset. Mliondika enzi za majuu, unyamwezini, majuu etc. Ni ngumuumia kujitambua na kujipima km mmeenda mbele, nimerudi nyuma au mmeganda. Awamu ya wasanii mlijiona kisanii kuliko halisia. Kazeni buti
 
Diaspora bado unataka kuajiriwa na serikali ?baada y kuwekeza nchi...kweli diaspora wengi hamjitambui...endeleeni tu kupiga picha za istagram
 
Kwanza wana dharau, kujisikia na kutaka kuabudiwa kama miungu watu pili hawana uchungu hata punje na nchi yao,tatu wanajiona wao ni bora zaidi kuliko mtanzania yyte kisa yupo ughaibuni usishangae akamdharau hata rais wako
 
Kwanza wana dharau, kujisikia na kutaka kuabudiwa kama miungu watu pili hawana uchungu hata punje na nchi yao,tatu wanajiona wao ni bora zaidi kuliko mtanzania yyte kisa yupo ughaibuni usishangae akamdharau hata rais wako
Utawajumlishaje watu maelfu kwa maelfu ambaobhata wao wenyewe kwa webyewe hawapatani uwaweke katika kundi moja hivyo?
 
Diaspora bado unataka kuajiriwa na serikali ?baada y kuwekeza nchi...kweli diaspora wengi hamjitambui...endeleeni tu kupiga picha za istagram

Diaspora kuna watu wa kila aina, maelfu kwa maelfu kama si mamilioni kabisa.

Kuwa specific unaongelea limbukeni fulani walio diaspora. Sio diaspora.

Hawa ndugu zetu wengine, if the account has any credibility at all, wanachafua jina la diaspora. Sawa, umeenda nje hela unaweza kukosa, basi hata elimu au exposure tu ya kujua kwamba kulilia kazi za serikali ya Tanzania usawa huu ni balaa tu umekosa?

Hivi hawa wazee wanavyoendeshwa resi bila hata common decorum wala dignity kuna mtu mwenye akili yake sawa analilia kazi ya serikali ya Tanzania tu?

How desperate and stupid does one need to be to do that?

Kuna watu hata ukitaka kutupa urais wa Tanzania burebure tunaweza kukukatalia jinsi tusivyo na hamu na kazi za serikali ya Tanzania.

Watu wanasajili ma patents, wanawekeza kuanzia stocks mpaka real estate, wako katika top 5 percent of earners US, bila wizi wala rushwa, walilie kazi za serikali ya Tanzania kwa msingi gani?

Hao limbukeni ambao wamejikuta wako nje ya Tanzania, probably wakihemea midomo, hawa represent Final Four ya Villanova.

You rookies, it's the final not the playoffs.
 
je nikirudi kuna qengeh yeyote atanilipa elf 47 kwa saa
Ninyi ni watu mnaodhani kwamba ni wa daraja fulani la juu pasipo kutizama mnamchango gani kwa taifa,mpo huko kutafuta maisha bt mmelisaidia vp taifa kwa juhudi zenu binafsi nje ya serikali,yupo mtu huku nyumbani anakipato cha kawaida lakini analipa kodi,huu ndio uzalendo,ninyi kaeni huko acheni kelele tuachieni tanzania
 
sasa nyinyi wala vumbi mnaojidai mna elimu iliyokamilika hata toothpick tu holaaaaaa. Nchi inajengwa kwa misaada. Badala mkimbilie kuwajengea wananch makazi mengi na bora pamoja na mfumo mzuri wa upatikanaji maji safi na salama manakimbilia miflaiova migorofa na midaraja kama ya kigambon.

Sasa iyo elimu yenu inawasaidia nini? Somen muelimike bana
Ndio mtz huyo,dharau kisa yupo ughaibuni,the most mnakaa huko inafika kipindi mlichofanya huko hakuna zaidi yakutoboa masikio na nyumbani napo hakuna mlichofanya wakati umri nao ushasonga,ninyi ni watu msio na faida kwa taifa hili,hamlipi kodi,hamuwekezi chochote huku nyumbani zaidi ya tambo zakiswahili,kiukweli baadhi yenu ni hovyo kabisa
 
Ndio mtz huyo,dharau kisa yupo ughaibuni,the most mnakaa huko inafika kipindi mlichofanya huko hakuna zaidi yakutoboa masikio na nyumbani napo hakuna mlichofanya wakati umri nao ushasonga,ninyi ni watu msio na faida kwa taifa hili,hamlipi kodi,hamuwekezi chochote huku nyumbani zaidi ya tambo zakiswahili,kiukweli baadhi yenu ni hovyo kabisa
Acha wivu.... Aliyeenda mbele huwezi lingana naye we mshindia limao
 
Uteuzi pia lazima uzingatie mchango wa muhusika katika nchi anakotoka.Uwe wa kodi nk
Ukiangalia ma diaspora wengi wangependa waje kuongoza mashirika mfano yanayolipa vizuri yaliyoanzishwa na watu wa ndani kwa kodi zao.Diaspora wanataka kuvuna wasipopanda.Utakuta wengine walikimbia nchi wakasema ina hali ngumu.Kuna watu wakabaki wakapigana wakiwa ndani hali ikawa nzuri sasa inapofikia uteuzi hivi Raisi aache kumpa mpiganaji aliyebaki ndani mwenye uzalendo na nchi yake jua liwake mvua inyeshe aende akatafute mkimbizi wa kiuchumi anayeitwa diaspora ampe?

Anyway ili Diaspora wa Tanzania muonekane wa maana igeni wenzenu ma dispora Wahindi,wachina na wazungu na waarabu

Diaspora wa kizungu,kihindi,kiarabu na kichina kazi yao huwa ni

1.Kueneza utamaduni wao kwenye nchi husika.Mfano mzungu ataleta mambo ya kizungu,hoteli za kizungu.Tabia za kizungu,mila za kizungu,Mavazi ya kizungu nk

Mhindi vivyo hivyo na mwarabu vivyo hivyo na mchina vivyo hivyo Kama mzungu.Mchina ataleta hadi CHINESE restaurant

Taabu inakuja kwa Diaspora la kitanzania likienda kwa watu ni taabu litaanza kila kitu kuiga cha kule lilikoenda.Unakuta hata uvaaji jitu nzima zee lakini limetinga kikaptula na kikofia cha machizi.Kula utakuta linajisifia kula MCdonalds nk Kuliko kula KANDE ZA KITANZANIA.

Hata kunyoa tu litanyoa kaa bweeege fulani hivi la marekani au ulaya hata huwezi lijua kama ni litanzania.

2.Madiaspora wa nchi za kizungu ,kichina,kiarabu na kihindi wao huwa kazi yao kuleta na kuuza bidhaa za kutoka kule kwenye nchi zao.Ukiwaona wazungu unajua atauza vitu vya kizungu,ukiona muhindi unajua yeye ni muuzaji wa bidhaa za india,Ukimwona mwarabu unajua kabisa biashara ya mafuta na gesi toka uarabuni yeye ndio mwenyewe ,Ukiona mchina unajua yeye ndio agenti mkuu wa biashara za china huko aliko.
Kwa kuwa mawakala wa biashara na bidhaa za nchi wanakotoka wanaziingizia nchi zao mapato kibao.

Ukija madiaspora wa kitanzania ukiuliza nani agent wa biashara za Tanzania kule unakuta hakuna! Wako tu kule kama vibarua wa wazungu halafu kesho utasikia mtukumbuke kututeua.

Sipingi Raisi kuteua lakini wameisaidia nini Tanzania sio familia zao.Mfano akiwepo Diaspora analeta watalii labda elfu moja kwa mwaka mimi nitakuwa wa kwanza kuomba huyo diaspora ateuliwe kuwa balozi mdogo kwenye ubalozi wa Tanzania kwenye hiyo nchi alipo.Lakini hivi hivi tu hakuna.MKONO MTUPU HAULAMBWI .kILA DISPORA ajiulize kwa nini anafikiri ateuliwe ametoa mchango gani kwa nchi?

Madiaspora wa Tanzania jifunzeni kwao muwe na faida kubwa kwa nchi yenu Tanzania kama wenzenu

Umeelezea vema kabisa mkuu,
Mwenye kuelewa na aelewe.
 
unamaumivu makali ya ndani eeh. Denmark haijavamiwa kwa taarifa yako ninamchango mkubwa sn kwenye hii nchi. My credit and crime record is good nalipa 36% tax am eligible to take a mortgage na mkopo hata wa 700k DKK. I might be an academic dwarf my Brother but this small nation appreciate my efforts and contributions. Nyinyi endeleen kujenga mibomba ya gesi mibasi iendayo kasi huku wananch maji ya shida wanashindia viwavi
Titi la mama ni tamu hata likiwa la mbwa,Tanzania ni titi la mama
 
Awamu hii ya 5 imekuja kauli mbiu ya HAPA KAZI TU hata sijui waliitoa wapi hii kitu, haya sasa wameingia madarakani vurugu mechi kila mtu na wake FUKUZA FUKUZA kila kona, ukiangalia watueuliwa wote hakuna Diaspora hata mmoja. Jamani hii nchi ni ya kwetu wote mbona awamu ya 4 walitushirikisha kikamilifu? Hata ukienda Ubalozini (Washington DC) haupati ushirikaiano wa enzi zile za Awamu ya 4 maana kila mtu anatetemeka tu sijui ndo kuogopa fukuza fukuza! Tuajirini sisi Diaspora muone damu mpya na mawazo mapya katika utendaji wa serikalini nchi itanyooka.
kila zama na nabii wake,huyu nabii mwingine kabisaa mjipange tu harembi wala nini
 
Back
Top Bottom