Diaspora Wetu Wanafanya Nini cha Kuonekanika Huko Ughaibuni?. Diaspora Mliofanikiwa, Onekanikeni Kupitia TAK na Rudisheni Tanzania Japo Kidogo!

Diaspora Wetu Wanafanya Nini cha Kuonekanika Huko Ughaibuni?. Diaspora Mliofanikiwa, Onekanikeni Kupitia TAK na Rudisheni Tanzania Japo Kidogo!

Mimi niliishia level ya kubeba box, sikufanikiwa kutusua, hivyo nikajirudia zangu Bongo. Hapa nawazungumzia diaspora wa Tanzania walotusua Marekani, wana vuta ma G -Wagon na ma Tesla, huku vijijini kwao walikotoka, kina mama wanajifungulia chini wanafunzi wanakaa chini kwa kukosa deski!.
Is this fair?.
P
Kwani serikali imeshindwa kuwawekea vitanda na hayo madeski ? Msaada sio deni, si mama amesambaza madeski nchi nzima na kujenga shule na vituo vya afya vya kisasa nchi nzima au yameliwa na mchwa ?
 
Mimi niliishia level ya kubeba box, sikufanikiwa kutusua, hivyo nikajirudia zangu Bongo. Hapa nawazungumzia diaspora wa Tanzania walotusua Marekani, wana vuta ma G -Wagon na ma Tesla, huku vijijini kwao walikotoka, kina mama wanajifungulia chini wanafunzi wanakaa chini kwa kukosa deski!.
Is this fair?.
P
Kila mwaka wa fedha serikali ya chama Chako Cha CCM,kinatumia 500+b kununua magari ya kifahari na wakati huo huo watu wanajifungulia chini na wanafunzi Wana kaa chini,mbona hautoi ushauri kwa serikali kuacha matumizi ya anasa na pesa kupelekwa kwenye sekta zinazo wagusa wananchi moja kwa moja ?

Alafu wakati huo huo unataka watu walio jipambania wenyewe bila msaada wa serikali ya CCM,kufanya Kazi ya serikali ya kudumisha miundombinu ya hospitalini na shuleni?
 
Watu wengi hawana interest kujulikana Bongo. Nchi imewakataa sasa washoboke nayo kwa nini?

Watu wanajulikana na familia zao na kwenye jamii zao huko.

Leo nilikiwa naongea na mtu kajenga zahanati na kituo cha polisi kwao huko kijijini.

Hicho ndicho muhimu kwake.

Kwenye kuwekeza nchi haina sheria rafiki watu hata kusaidia wanaombwa rushwa.

Yani unasaidia halafu unaombwa rushwa ili usaidie.

Nani anataka ujinga huo?
huyo mama aliyejenga kituo cha polisi na zahanati namfahamu sana. ni wa nyumban kabisa. alikuwa anafanya kazi hosp. na sasa amestaafu ila ukweli ni kwamba amesaidia sana wengi pale kijijini. hyo zahanat ilikuwa haina choo ndo kusaidia kujenga choo cha kisasa pamoja na maji
 
Mtu Mtanzania ana magari matano ya kifahari, nchini Marekani, anaendesha kwa kubadilisha tuu magari, halafu ile hospitali ya Kibon’goto pale Sanya, kuna wamama wajawazito, wanajifungulia chini kwa kukosa, kitanda, ile G-Wagon moja tuu, ingejaza vitanda hospitali nzima, au ma deski shule nzima!.

Na viongozi wa Tanzania wanashindana kutumia fedha za walipa kodi kununuliwa magari ya kifahari ya VX, safari zisizoisha Dodoma, Dar es Salaam, marupurupu fedha hizo zinazidi anazopata diaspora aliyejituma kwa kufanya kazi kwa bidii huku viongozi wa Tanzania wakitumbua mfumo wa hazina ya taifa kwa matumizi ya kufahari.

Kutumia mabilioni ya shilingi za kitanzania kufanikisha uchafuzi wa mchakato wa uchaguzi wa serikali za mitaa na Kuhitimisha uchaguzi feki wa 27 November 2024...

Hii ni mifano michache ambayo serikali ingeweza kutumia fedha hizo bila kutapaya ovyo hata huruma kutoa huduma ya afya buree kwa raia imeshindikana wakati nchi kama Cuba wameweza kuzuia maradhi na pia kutoa huduma bure kwa raia kwa kiwango cha huduma zinazilingana na zile za huduma afya katika nchi za dunia ya kwanza
 
Wanabodi,

Bado niko hapa nchini Marekani kwa ziara binafsi, nimejitahidi kujichanganya na baadhi ya wana diaspora wa Tanzania walioko nchini Marekani, na kujiuliza jee wana Dispora wetu, wanafanya nini cha kueleweka na cha kuonekanika?.

Nimejitahidi kuwasiliana na kile chama cha DICOTA, sikubahatika kupata ushirikiano mzuri, ila nitaendelea kuwatafuta Diaspora wetu waliofanikiwa Marekani, wanafanya nini, na hayo mafanikio yao, yanaifaidia vipi nchi yao ya Tanzania?.

Kwa kupitia juhudi binafsi, nimefanikiwa kumuona dada mmoja wa Kitanzania, aliyehamia Marekani, mwaka 1999, na yuko kule mpaka leo. Huyu dada, naomba nisimtaje jina kwasababu sikumwambia kuwa nitaandika. Nime note Diaspora wa Tanzania waliofanikiwa hapa nchini Marekani, hawapendi kutajwa au kuandikwa wanafanya nini Marekani.

Huyu Dada ni mmiliki wa kampuni inayo fanya biashara ya huduma, services industry, ameajiri watu zaidi ya 50, kila mwezi anawalipa mishahara ya zaidi ya milioni 500.

Dada kanikaribisha kwake, ana kaa mtaa wa kitajiri, anamiliki nyumba, kubwa ya ghorofa tatu na ana magari 5 ya kifahari, ikiwemo Benzi ya G Wagon na gari ya Kimarekani ya Tesla inayotumia umeme. Hesabu ya haraka haraka ya thamani ya magari ni zaidi ya Shilingi Bilioni 1 ya Kitanzania.

Huu ni mfano mmoja tuu wa Mtanzania aliyefanikiwa Marekani, ametoa ajira kwa watu, na kutengeneza faida kubwa. Nilipomuuliza kwanini asiwekeze Tanzania, alinijibu anasubiria uraia pacha, ndipo aje kuwekeza Tanzania.

Imetokea tuu mimi ninamfahamu huyu Dada, mpaka kule kijijini kwao, Sanya Juu Moshi, ambako mimi nimefika, na kabla sijakwenda Marekani, nilipita hapo kwao Sanya, sasa hali niliyoiona ya umasikini wa hapo kijijini kwao, nikilinganisha na maisha ya kitajiri na kifahari anayoishi Marekani, ni mbingu na nchi!.

Hivyo huu ni wito kwa serikali yetu kuharakisha mkakati wa uraia pacha, ili Diaspora wa Tanzania waliofanikiwa ughaibuni, waje kuwekeza nyumbani Tanzania na kurudisha shukrani nyumbani Tanzania na sio kupiga tuu mapicha kurungishia mandinga yao makali ya ma G-Wagon na ma Tesla!.

Mtu Mtanzania ana magari matano ya kifahari, nchini Marekani, anaendesha kwa kubadilisha tuu magari, halafu ile hospitali ya Kibon’goto pale Sanya, kuna wamama wajawazito, wanajifungulia chini kwa kukosa, kitanda, ile G-Wagon moja tuu, ingejaza vitanda hospitali nzima, au ma deski shule nzima!.

Nimetembelea maeneo mbalimbali ya Marekani labda nitaona mafanikio ya kuonekanika ya Diaspora wa Tanzania, zaidi ya huyu dada kunikaribisha kwake, sikufanikiwa kuona kitega uchumi chochote cha Mtanzania nchini Marekani, kila rais wetu akija Marekani ni kukutana na Watanzania waishio Marekani, na kubadilisha mawazo tuu, Rais wa Kenya akija Marekani ni anafungua miradi ya Diaspora wa Kenya.

Muda aliokuja Marekani, huyu mdada wa Tanzania, ule mwaka 1999, ni muda huo Mkenya Kevin Onyona, alihamia Marekani, na kuajiriwa na Home Depot, kampuni ya kimataifa ya uboreshaji wa nyumba ya Marekani. Sasa hivi Kevin ni mmiliki ya migahawa ya Swahili Village ambayo ni mojawapo ya mikahawa bora zaidi ya vyakula vya Kiafrika nchini Marekani.

Kevin Onyona alianzisha mlolongo huo mwaka wa 2016, na leo inajivunia migahawa mitatu. Miaka sita baadaye, ametumia migahawa yake kujenga uhusiano halisi kati ya utamaduni wa Kiafrika na dunia nzima. Mkahawa mkuu wa Swahili Village oko Rhode Island Ave, Beltsville. Migahawa mingine miwili iko Washington DC na New Jersey. Mgahawa wa Washington DC ulifunguliwa na aliyekuwa rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, kiongozi gani wa Kitanzania aliwahi kufungua mradi wowote wa Diaspora wa Tanzania nje ya Nchi?

Wito kwa Diaspora wetu, najua kuna uwezekano kuna mambo makubwa mazuri ya kuonekanika Diaspora wa Tanzania wanafanya, lakini hatuyaoni na hatuyajuo, hivyo natoa wito kwa Diaspora wetu, anekanikeni basi, inaumiza kila siku unaona diaspora wa wenzetu, na kujiuliza diaspora wetu wako wapi na wanafanya nini?.

Sasa mimi mwandishi wakp wa habari na mtangazaji wa kujitegemea, Pascal Mayalla, , anayeandaa vipindi vya TV, Redio, makala magazetini na kwenye mitandao ya kijamii, nikifanya kazi kupitia kampuni ya PPR, www.ppr.co.tz, ambayo sasa imetua rasmi nchini Marekani kwa kufungua ofisi, nimejotolea kuandaa vipindi vya mchango wa diaspora wa Tanzania kwa maendeleo ya taifa.

Kipindi Kipya cha TAK
TAK ni kipindi kipya cha TV chenye lengo la kuiangazia Tanzania Kitaifa, Kikanda na Kimataifa kuhusu mambo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii, ambayo yanaihusu Tanzania kwenye medani za kimataifa, kama issues za Umoja wa Mataifa, Jumuiya ya Madola, issues za kikanda na kimataifa, AU, SADC, AfCFTA, Bunge la Afrika, Bunge la EAC, Jumuiya ya Africa Mashariki, EAC na mambo mengine ya kimataifa. Kipindi hiki kitaimulika Tanzania kwenye mikutano ya kimataifa, ukiwemo mchango wa Diaspora wa Tanzania, na wakati huo huo kuangazia fursa mbalimbali za kimataifa kwa Watanzania kuzichangamkia.

Kipindi hiki kitarushwa kwenye local channels za TV za Tanzania, DSTV, Star Times na kwenye online media.

Mimi kama Mtanzania Mzalendo, ninaumia sana kila ninapoona diaspora wa wenzetu wanafanya mambo makubwa ya kuonekanika, na kujiuliza Diaspora wetu wanafanya nini?, mbona hatuwaoni?, hivyo napenda kuona Tanzania tunafaidika na mchango wa wana diaspora wetu wenye exposure kubwa huko walipo, kuitumia kulisaidia taifa letu kisiasa, kiuchumi cha kijamii.

Paskali
Rejea za Mwandishi Kuhusu Diaspora
Tuanze na wewe ng'wanangwa, mke wako ni Diaspora amewekeza nini huku home?
 
Yes Mkuu Kiranga ,kwanza naheshimu sana the right to privacy,ndio maana nimewaandikia desk letu la diaspora pale MFA, kuhusu TAK, wame mute,na mimi sikuwauliza tena kitu。 nikawaandikia DICOTA, nao vile vile, sikuwauliza kitu。 Naheshimu sana the right to privacy, lakini as a journalist,naumia sana ninapoona diaspora wa wenzetu wanafanya vitu vya kuonekanika, kama hawa, Diaspora wa Kenya wafanya makubwa Marekani. Sisi Diaspora Wetu wanafanya nini cha kuonekana huko walipo?
mtu unajiuliza sisi Watanzania vipi?. Angalia picha kama hii View attachment 3153405
Tutaona raha sana kama na sisi Wa TZ, tutakuwa na visibility kama za kihivi, kila kiongozi wa Kenya wakija, menu inapigwa hapo!, its a good RV ya Wakenya, sisi vipi?.

Naamimi wako diaspora wetu, wanafanya vitu vikubwa huku ughaibuni na investments kubwa kubwa nyumbani, lakini wameamua kuwa low profile, hawa hatuwaingilii uhuru wao, na wala mimi kutafuta visibility ya diaspora wetu sio kuingilia maisha binafsi au kuwafuatilia watu, lakini kiukweli its not fair watu kujiselfisha na ma G-Wagon na ma Tesla kuturingishia, ukiwauliza wanasaidiaje nchi yao, wana mute, hatutaki kufuatiliwa!.

P
Diaspora wa kitanzania ni njaa kali tu wengi wanasubiri wafariki watusumbue michango! Sitoi mchango wangu kwa Diaspora! Wenzao Wakenya kila mwaka wanatuma mabilioni nyumbani kusaidia uchumi wa nchi wa kwetu kuzurura tu! Marehemu Le Mutuz alirudi nde.ke.ma tu bila chochote!
 
Labda wanaogopa kuombwa ombwa hela,
Ni kweli,hili la watu kuomba hela ni tatizo, hata cha nilipopeleka hili wazo la kipindi TAK, walitangulia kusema hatuna hela!,nikauliza kwenye proposal yangu, kuna popote nimeomba pesa ?。
vile vile kuna misukosuko ya kisiasa akionekana hajakubaliana na baadhi ya masuala ya kiserikali,
hili ndilo linakwamisha uraia pacha, kuna majinga kule serikalini wanaamini diaspora wote ni wapinzani na wata support the opposition, kumbe kuna diaspora wengi kibao, hawana kabisa interest na local politics。
mfano Mange kimambi aliwahi kufungiwa ofisi za ile app yake
Huyu bidada alizidi,najua unajua bidada ni kichaa kabisa, alikuja kuwa too much!,yeye sio mtu wa av production,akaletewa a doctored video ya kiongozi akifanya mambo flani binafsi, yeye akajitapa atarusha!, hata ningekuwa mimi, nafunga!。
Kuna levels fulani mtu hawezi kurekodi video zile kisha zitue kwa huyo kichaa!
P
 
Kwani ni uongo sasa?
Duh。。。!, Mkuu Manjaga, Manjagata hata wewe?!。 Mtu wao anaweza kuandika haya humu,
P
 
Diaspora wa kitanzania ni njaa kali tu wengi wanasubiri wafariki watusumbue michango! Sitoi mchango wangu kwa Diaspora! Wenzao Wakenya kila mwaka wanatuma mabilioni nyumbani kusaidia uchumi wa nchi wa kwetu kuzurura tu! Marehemu Le Mutuz alirudi nde.ke.ma tu bila chochote!
Mkuu kwa nini huwa mnachuki kiasi hicho ? Kuchangia uchumi kinamna gani ? Lini serikali ya Tanzania ilisaidia watu kupata fursa nnje ya nchi kama inavyofanya kenya ?
 
Kosa kubwa wanalifanya diaspora na kuwafanya wapate ugumu wa uraia pacha ni Kama anavyofanya huyo mdada kudai hawezi kuwekeza huku Hadi uraia pacha uruhusiwe.
Kama wangewekeza nyumbani kwa maswala ya afya, elimu, viwanda, kilimo wangetengeneza ushawishi mkubwa kuanzia kwa wananchi wa kawaida mpaka wanasiasa kupitishwa Sheria ya uraia pacha. Lakini wamewekeza ugenini huku kwao wameacha kwa kisingizio Cha kusubiri Mambo ya uraia pacha. Matokeo ukimwuliza mwananchi wa kawaida faida ya uraia pacha haioni.
 
huyo mama aliyejenga kituo cha polisi na zahanati namfahamu sana. ni wa nyumban kabisa. alikuwa anafanya kazi hosp. na sasa amestaafu ila ukweli ni kwamba amesaidia sana wengi pale kijijini. hyo zahanat ilikuwa haina choo ndo kusaidia kujenga choo cha kisasa pamoja na maji
Amini usiamini diaspora kama huyu atabarikiwa sana, huu ndio utu na uzalendo wa kweli。
P
 
Mkuu kwa nini huwa mnachuki kiasi hicho ? Kuchangia uchumi kinamna gani ? Lini serikali ya Tanzania ilisaidia watu kupata fursa nnje ya nchi kama inavyofanya kenya ?
Onyesheni mfano ili serikali ijione ilikosea! Hata wenzenu Kenya walianza kwanza kwa kutuma kidogo kidogo mpaka ikaona kumbe kuna fursa! Sasa nyie wa kwetu kulilia michango ya kusafirisha maiti tu! Mzikane huko huko msitusumbue sisi!
 
Watu wengi hawana interest kujulikana Bongo. Nchi imewakataa sasa washoboke nayo kwa nini?

Watu wanajulikana na familia zao na kwenye jamii zao huko.

Leo nilikiwa naongea na mtu kajenga zahanati na kituo cha polisi kwao huko kijijini.

Hicho ndicho muhimu kwake.

Kwenye kuwekeza nchi haina sheria rafiki watu hata kusaidia wanaombwa rushwa.

Yani unasaidia halafu unaombwa rushwa ili usaidie.

Nani anataka ujinga huo?
Wazo la maana sana hili.

Hakuna umuhimu wowote wa kujulikana, kila mtu aishi maisha yake tu.
 
Yes Mkuu Kiranga ,kwanza naheshimu sana the right to privacy,ndio maana nimewaandikia desk letu la diaspora pale MFA, kuhusu TAK, wame mute,na mimi sikuwauliza tena kitu。 nikawaandikia DICOTA, nao vile vile, sikuwauliza kitu。 Naheshimu sana the right to privacy, lakini as a journalist,naumia sana ninapoona diaspora wa wenzetu wanafanya vitu vya kuonekanika, kama hawa, Diaspora wa Kenya wafanya makubwa Marekani. Sisi Diaspora Wetu wanafanya nini cha kuonekana huko walipo?
mtu unajiuliza sisi Watanzania vipi?. Angalia picha kama hii View attachment 3153405
Tutaona raha sana kama na sisi Wa TZ, tutakuwa na visibility kama za kihivi, kila kiongozi wa Kenya wakija, menu inapigwa hapo!, its a good RV ya Wakenya, sisi vipi?.

Naamimi wako diaspora wetu, wanafanya vitu vikubwa huku ughaibuni na investments kubwa kubwa nyumbani, lakini wameamua kuwa low profile, hawa hatuwaingilii uhuru wao, na wala mimi kutafuta visibility ya diaspora wetu sio kuingilia maisha binafsi au kuwafuatilia watu, lakini kiukweli its not fair watu kujiselfisha na ma G-Wagon na ma Tesla kuturingishia, ukiwauliza wanasaidiaje nchi yao, wana mute, hatutaki kufuatiliwa!.

P

Kwa sheria na uchawi wa mpaka kufikia rais wa nchi anasema anataka aone matajiri wanaishi kama mashetani nani yupo tayari kubeba risk ya namna hiyo? Hao unaowatolea mfano ni kwa sababu nchi yao ya baba na mama inasupport na kuheshimu mchango wao. Kwa nchi ambayo mawaziri wanatoa macho hadi yanataka kuanguka wakisikia diaspora hamna atakayesema issuez zake kiongozi. Its safe to be low profile as a Tanzanian than showing what are your achievements. Najua habari ndio biashara na maisha yako lakini hamna mtanzania atajitangaza ili awe victim wa kufelishwa na ndugu zake! Tubaki JF kuchitchat tu baba, mengine yabaki personal
 
Watu wengi hawana interest kujulikana Bongo.
Ni kweli kuna watu wako very low profile,ila kuna low profile ya being low humble na kuna low profile ya kuwa discreet,ila kuna low profile ku hide, watu wasijujue, zote hizi tunazijua na tunaziheshimu, ila nyingine ni uchoyo tuu, being secretive, siku hizi kuna watu wanapiga picha na mabulungutu ya mahela, ma dola,ukiwauliza what they do,hawasemi!。Lengo la TAK, is to highlight the sucess stories za diaspora wetu, mfano mzuri ni huu,
Nchi imewakataa sasa washoboke nayo kwa nini?
Sio kweli nchi imewakataa, uraia pacha unakuja。
Watu wanajulikana na familia zao na kwenye jamii zao huko.
Yes,its true,mimi wife ni diaspora amevuta ndugu zake wote,hadi mama yake, siku nakwenda kumsalimia,kanipiga na $1000 ya soda!na huko kwao usipime,ila its not enough,kusaidia ndugu ni wajibu hupati baraka kubwa kama charity ya kusaidia the poor Tanzanians。
Leo nilikiwa naongea na mtu kajenga zahanati na kituo cha polisi kwao huko kijijini.
mtu kama huyo atabarikiwa sana, just imagine kama all successiful Tanzania diaspora all over the world wangekuwa visible,what they do and share their success stories na wengine,na ku streach their helping hand to reach the poor of the poor, it would make a big difference!
Hicho ndicho muhimu kwake.
naunga mkono do what you like,what you love,and what will make you happy, kama mtu umebarikiwa,umefanikiwa una uwezo wa kununua magari 5 ya kifahari,and that is what makes you happy,be happy,but take it from me,the true happyness ni yule aliyejenga hospital na police post。
Kwenye kuwekeza nchi haina sheria rafiki watu hata kusaidia wanaombwa rushwa.
Hili ni tatizo
Yani unasaidia halafu unaombwa rushwa ili usaidie.
duh。。。!
Nani anataka ujinga huo?
Usiite ujinga, mimi kama mtu wa media,nina genuine kuona the visibility of successful diaspora to share their success stories
P
 
Umoja wa Mataifa, Jumuiya ya Madola, issues za kikanda na kimataifa, AU, SADC, AfCFTA, Bunge la Afrika, Bunge la EAC, Jumuiya ya Africa Mashariki, EAC na mambo mengine ya kimataifa. Ki

Umefanya vizuri ila kiwe kipindi katika lugha ya kiingereza, TV za lugha ya kigeni hakuna kabisa, waandishi wa habari waliotayarisha vipindi na mahojiano kwa kiingereza hakuna kabisa labda yule wa Mwananchi digital na The Chanzo. Viongozi na watanzania wa kawaida hatuwaoni.

Waandishi wanejazana ktk vipindi vya lugha moja tu rasmi ya KiSwahili wakati kuna ya Lugha rasmi ya pili Tanzania kiEnglish. Kenya wanapiga lugha zote ndiyo maana inasikika kimataifa na kikanda.

Mwandishi nguli anzisha Mapinduzi katika tasni kwa kuitangaza Tanzania na diaspora ktk vipindi utavyotayarisha katika lugha zote mbili rasmi za taifa la Tanzania. Uzuri una uwanja mpana kama mwandishi wakili msomi.
 
Back
Top Bottom