Diaspora Wetu Wanafanya Nini cha Kuonekanika Huko Ughaibuni?. Diaspora Mliofanikiwa, Onekanikeni Kupitia TAK na Rudisheni Tanzania Japo Kidogo!

Diaspora Wetu Wanafanya Nini cha Kuonekanika Huko Ughaibuni?. Diaspora Mliofanikiwa, Onekanikeni Kupitia TAK na Rudisheni Tanzania Japo Kidogo!

Huyu bidada alizidi,najua unajua bidada ni kichaa kabisa, alikuja kuwa too much!,yeye sio mtu wa av production,akaletewa a doctored video ya kiongozi akifanya mambo flani binafsi, yeye akajitapa atarusha!, hata ningekuwa mimi, nafunga!。
Kuna levels fulani mtu hawezi kurekodi video zile kisha zitue kwa huyo kichaa!
P
Mange ana matatizo yake tatizo kwenye kushughulikia haya mambo kunakuaga na double standard kiasi kwamba watu wanaanza kufikiri ni kama kukomoana tu.

Kuna watu wengi sana wanavunja sheria, wanadhiaki wengine na mbaya zaidi wapo mpaka wanatashia maisha ya watu lakini kwa sababu ni watu wa system au machawa wa chama tawala huwa hawaguswi.

Kosa alilolifanya Mange ni dogo sana ukilinganisha na kitemdo alichofanya Bashite cha kuvamia studio za clouds na silaha za kivita lakini hakuchukuliwa hatua zozote. Nakubaliana na wewe Mange ni kichaa lakini izo sheria za kushughulikiana ziwe msumeno kwa wote angalao italeta picha kwamba hakuna conflict of interest za kisiasa
 
Wazo la maana sana hili.

Hakuna umuhimu wowote wa kujulikana, kila mtu aishi maisha yake tu.
Wabongo wengi na serikali yao wana tabia ya kuwapuuza watu, halafu watu wana fight kivyao mpaka wanaitoa huko nje, halafu wakishaitoa ndiyo utawasikia "huyu Mtanzania".

Abdulrazak Gurnah kaondoka Zanzibar zamani sana in the 1960s huko. Kaenda Uingereza, kasoma kivyake, kafundisha vyuoni. Serikali ya Uingereza imekuwa na mchango mkubwa kwake kuliko Zanzibar/Tanzania.

Alivyoshinda nishani ya Nobel tu, watu wakaanza kum claim "huyu Mtanzania".

Hawajamsoma, hawamjui, hawajamsaidia, wamemzingua mpaka kaamua kuishi nje kama mkimbizi asiye na kwao.

Halafu aliposhinda nishani ya Nobel mpaka rais wa Zanzibar kajiweka karibu naye akisema huyu Mzanzibari.

Leo kuna mshikaji alikuwa anakaa Canada karudi Zanzibar miaka kadhaa, mpaka sasa kitambulisho cha ukazi Zanzibar wanamzingua, anasema hata uchaguzi ujao wa 2025 inaonekana hataweza kupiga kura, kwa sababu ya huu ujinga. Wakati wenzetu wa nchi nyingine wanapiga kura hata wakiwa nje ya nchi.

Sasa kwa figisu hizi unategemea vipi watu wenye uelewa wa mambo washobokee habari za Utanzania?
 
Ni kweli kuna watu wako very low profile,ila kuna low profile ya being low humble na kuna low profile ya kuwa discreet,ila kuna low profile ku hide, watu wasijujue, zote hizi tunazijua na tunaziheshimu, ila nyingine ni uchoyo tuu, being secretive, siku hizi kuna watu wanapiga picha na mabulungutu ya mahela, ma dola,ukiwauliza what they do,hawasemi!。Lengo la TAK, is to highlight the sucess stories za diaspora wetu, mfano mzuri ni huu,

Sio kweli nchi imewakataa, uraia pacha unakuja。

Yes,its true,mimi wife ni diaspora amevuta ndugu zake wote,hadi mama yake, siku nakwenda kumsalimia,kanipiga na $1000 ya soda!na huko kwao usipime,ila its not enough,kusaidia ndugu ni wajibu hupati baraka kubwa kama charity ya kusaidia the poor Tanzanians。

mtu kama huyo atabarikiwa sana, just imagine kama all successiful Tanzania diaspora all over the world wangekuwa visible,what they do and share their success stories na wengine,na ku streach their helping hand to reach the poor of the poor, it would make a big difference!

naunga mkono do what you like,what you love,and what will make you happy, kama mtu umebarikiwa,umefanikiwa una uwezo wa kununua magari 5 ya kifahari,and that is what makes you happy,be happy,but take it from me,the true happyness ni yule aliyejenga hospital na police post。

Hili ni tatizo

duh。。。!

Usiite ujinga, mimi kama mtu wa media,nina genuine kuona the visibility of successful diaspora to share their success stories
P
Mimi nilikuwa na idea kama yako.

Ila ilikuwa kwenye engagement ya social media. Niliona Watanzania wajinga wanaongea sana, halafu wenye akili wako kimya.

Nikaanza kuwatafuta hao waliofanikiwa, wanaofanya mambo ya maana.

Nikamtafuta mmoja anaongoza foundation yenye budget ya $5 billion dollars hapa New York City at that point. Jamaa yuko vizuri kapita Harvard, Tanzania nako yuko well connected kuanzia Ikulu (alikuwa mshauri wa rais) mpaka mtaani.

Nikamwambia nakuomba uje tuongee na Watanzania, mambo ya career, uzoefu wako, matatizo ya Tanzania, fursa za kuyatatua, na chochote utakachopenda. Vijana watapata mengi ya kujifunza kwako.

Jamaa aliniambia yuko tayari kuongea on a small scale setting na watu wachache anaowajua lakini social media ya Bongo ni toxic space. Watu wanapenda fitna na kubishana kuliko kuelimika. Na yeye hapendi ubishi wa kijinga. Na zaidi ana high visibility akianza kubishana bishana na watu mitandaoni inaweza hata kumuharibia kazi yake.

Kuna wakati nilimuona kama selfish lakini kadiri muda unavyoenda na ninavyoangalia mazungumzo ya Wabongo nimemuelewa sana.
 
Jaribu kumcheki Ernest Makuliro wa EBM scholars . Au Kibonde. Au Kada mwenzio loveness mamuya wa.kijani wataku.connect na diaspora.

Wengi wanachoka na sheria. Yanayosemwa sio yanayotendwa kikwete aliwaahidi mengi ila yote yalikuwa siasa. Hata hili la dual citizenship.

Halafu.watu.wanaogopa majungu majungu wakishajulikana basi majungu kwao yanahamia.

Mbona Tundu lissu akienda marekani ana watu.kibao wana msupport kama Ohio wanajitahidi sana kina.Rwabutaza
 
Mange ana matatizo yake tatizo kwenye kushughulikia haya mambo kunakuaga na double standard kiasi kwamba watu wanaanza kufikiri ni kama kukomoana tu.
true,kuna vitu akifanya mburu matata,is not a big deal,lakini akifanya mtu mwenye jina ni issue!
Kuna watu wengi sana wanavunja sheria, wanadhiaki wengine na mbaya zaidi wapo mpaka wanatashia maisha ya watu lakini kwa sababu ni watu wa system au machawa wa chama tawala huwa hawaguswi.
true!
Kosa alilolifanya Mange ni dogo sana ukilinganisha na kitendo alichofanya Bashite cha kuvamia studio za clouds na silaha za kivita lakini hakuchukuliwa hatua zozote.
Kuvamia mahali ni mtu asiye na access ya mahali hapo, media zote ni public access places,RC ni president of regional,has all the rights to Access to all public places including Clouds media, hivyo hakuvamia。
Nakubaliana na wewe Mange ni kichaa lakini izo sheria za kushughulikiana ziwe msumeno kwa wote angalao italeta picha kwamba hakuna conflict of interest za kisiasa
naunga mkono hoja。
Kwa sheria na uchawi wa mpaka kufikia rais wa nchi anasema anataka aone matajiri wanaishi kama mashetani nani yupo tayari kubeba risk ya namna hiyo?
naunga mkono hoja
Hao unaowatolea mfano ni kwa sababu nchi yao ya baba na mama inasupport na kuheshimu mchango wao.
Tanzania tunathamini sana diaspora,hadi wana kitengo pale MFS, na soon tunakwenda kupitisha uraia pacha
Kwa nchi ambayo mawaziri wanatoa macho hadi yanataka kuanguka wakisikia diaspora
is this true?
hamna atakayesema issuez zake kiongozi.
tunaheshimu sana the right to privacy
Its safe to be low profile as a Tanzanian than showing what are your achievements.
tunaheshimu hili pia, lakini kwasababu diasporas wa jirani zetu wako open and transparent,watu wanaona the visibility yao and what they do, kwasababu Watanzania,lie low, ni low profile,watu hatuoni diaspora wetu wanafanya nini, seeing is believing, then tuna conclude kuwa diaspora wa Tanzania, they do nothing!。
Najua habari ndio biashara na maisha yako
its true huu ni mwaka wa 34 kwenye habari,na tangu 2007, niliikwaa LL。B from UDSM, na sasa ni pia ni mwanasheria na wakili wa kujitegemea,lakini bado niko kwenye habari。
lakini hamna mtanzania atajitangaza ili awe victim wa kufelishwa na ndugu zake!
naunga mkono hoja
Tubaki JF kuchitchat tu baba, mengine yabaki personal
Japo jf ni ukumbi wa chat tuu, lakini I'll keep fighting for TAK, ili wazo hili lisije likafa kama wazo hili Vipindi Maalum vya JF kwenye TV: Naomba Maoni Yako!
P
 
Umefanya vizuri ila kiwe kipindi katika lugha ya kiingereza, TV za lugha ya kigeni hakuna kabisa, waandishi wa habari waliotayarisha vipindi na mahojiano kwa kiingereza hakuna kabisa labda yule wa Mwananchi digital na The Chanzo. Viongozi na watanzania wa kawaida hatuwaoni.
My target viewers na audience ni the locals,hivyo ni vipindi vya lugha ya Kiswahili,kwenye mainsteam media。
Waandishi wanejazana ktk vipindi vya lugha moja tu rasmi ya KiSwahili wakati kuna ya Lugha rasmi ya pili Tanzania kiEnglish.
Mimi ni mzalendo, na vipindi vyangu ni vya kizalendo kwa kutumia lugha ya kizalendo ya Kiswahili ambayo ndio lugha yetu adhimu, ila PPR, tunafanya documentaries za English za wateja kama hizi

Kenya wanapiga lugha zote ndiyo maana inasikika kimataifa na kikanda.
ni kweli
Mwandishi nguli anzisha Mapinduzi katika tasni kwa kuitangaza Tanzania na diaspora ktk vipindi utavyotayarisha katika lugha zote mbili rasmi za taifa la Tanzania. Uzuri una uwanja mpana kama mwandishi wakili msomi.
Asante naipokea changamoto hii
P
 
My target viewers na audience ni the locals

Local imekuwa saturated sasa inatakiwa uende kimataifa, habari za Tanzania kimataifa ni chache tena zinatolewa na waandishi wakiwa Nairobi au Johannesburg.

Kazi hii ya kuhabarisha kimataifa kwa kiEnglish tunakupatia wewe maana ni kama hakuna waandishi wote kwa kiswahili wameshamaliza mchezo yamebaki manyoya, ila ukijikita kwa KiEnglish utakuwa Millard Ayo, SnS, Michuzi n.k kwa ujio wa kiingereza kwa soko la nyumbani na kimataifa pia.
 
Wanabodi,

Bado niko hapa nchini Marekani kwa ziara binafsi, nimejitahidi kujichanganya na baadhi ya wana diaspora wa Tanzania walioko nchini Marekani, na kujiuliza jee wana Dispora wetu, wanafanya nini cha kueleweka na cha kuonekanika?.

Nimejitahidi kuwasiliana na kile chama cha DICOTA, sikubahatika kupata ushirikiano mzuri, ila nitaendelea kuwatafuta Diaspora wetu waliofanikiwa Marekani, wanafanya nini, na hayo mafanikio yao, yanaifaidia vipi nchi yao ya Tanzania?.

Kwa kupitia juhudi binafsi, nimefanikiwa kumuona dada mmoja wa Kitanzania, aliyehamia Marekani, mwaka 1999, na yuko kule mpaka leo. Huyu dada, naomba nisimtaje jina kwasababu sikumwambia kuwa nitaandika. Nime note Diaspora wa Tanzania waliofanikiwa hapa nchini Marekani, hawapendi kutajwa au kuandikwa wanafanya nini Marekani.

Huyu Dada ni mmiliki wa kampuni inayo fanya biashara ya huduma, services industry, ameajiri watu zaidi ya 50, kila mwezi anawalipa mishahara ya zaidi ya milioni 500.

Dada kanikaribisha kwake, ana kaa mtaa wa kitajiri, anamiliki nyumba, kubwa ya ghorofa tatu na ana magari 5 ya kifahari, ikiwemo Benzi ya G Wagon na gari ya Kimarekani ya Tesla inayotumia umeme. Hesabu ya haraka haraka ya thamani ya magari ni zaidi ya Shilingi Bilioni 1 ya Kitanzania.

Huu ni mfano mmoja tuu wa Mtanzania aliyefanikiwa Marekani, ametoa ajira kwa watu, na kutengeneza faida kubwa. Nilipomuuliza kwanini asiwekeze Tanzania, alinijibu anasubiria uraia pacha, ndipo aje kuwekeza Tanzania.

Imetokea tuu mimi ninamfahamu huyu Dada, mpaka kule kijijini kwao, Sanya Juu Moshi, ambako mimi nimefika, na kabla sijakwenda Marekani, nilipita hapo kwao Sanya, sasa hali niliyoiona ya umasikini wa hapo kijijini kwao, nikilinganisha na maisha ya kitajiri na kifahari anayoishi Marekani, ni mbingu na nchi!.

Hivyo huu ni wito kwa serikali yetu kuharakisha mkakati wa uraia pacha, ili Diaspora wa Tanzania waliofanikiwa ughaibuni, waje kuwekeza nyumbani Tanzania na kurudisha shukrani nyumbani Tanzania na sio kupiga tuu mapicha kurungishia mandinga yao makali ya ma G-Wagon na ma Tesla!.

Mtu Mtanzania ana magari matano ya kifahari, nchini Marekani, anaendesha kwa kubadilisha tuu magari, halafu ile hospitali ya Kibon’goto pale Sanya, kuna wamama wajawazito, wanajifungulia chini kwa kukosa, kitanda, ile G-Wagon moja tuu, ingejaza vitanda hospitali nzima, au ma deski shule nzima!.

Nimetembelea maeneo mbalimbali ya Marekani labda nitaona mafanikio ya kuonekanika ya Diaspora wa Tanzania, zaidi ya huyu dada kunikaribisha kwake, sikufanikiwa kuona kitega uchumi chochote cha Mtanzania nchini Marekani, kila rais wetu akija Marekani ni kukutana na Watanzania waishio Marekani, na kubadilisha mawazo tuu, Rais wa Kenya akija Marekani ni anafungua miradi ya Diaspora wa Kenya.

Muda aliokuja Marekani, huyu mdada wa Tanzania, ule mwaka 1999, ni muda huo Mkenya Kevin Onyona, alihamia Marekani, na kuajiriwa na Home Depot, kampuni ya kimataifa ya uboreshaji wa nyumba ya Marekani. Sasa hivi Kevin ni mmiliki ya migahawa ya Swahili Village ambayo ni mojawapo ya mikahawa bora zaidi ya vyakula vya Kiafrika nchini Marekani.

Kevin Onyona alianzisha mlolongo huo mwaka wa 2016, na leo inajivunia migahawa mitatu. Miaka sita baadaye, ametumia migahawa yake kujenga uhusiano halisi kati ya utamaduni wa Kiafrika na dunia nzima. Mkahawa mkuu wa Swahili Village oko Rhode Island Ave, Beltsville. Migahawa mingine miwili iko Washington DC na New Jersey. Mgahawa wa Washington DC ulifunguliwa na aliyekuwa rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, kiongozi gani wa Kitanzania aliwahi kufungua mradi wowote wa Diaspora wa Tanzania nje ya Nchi?

Wito kwa Diaspora wetu, najua kuna uwezekano kuna mambo makubwa mazuri ya kuonekanika Diaspora wa Tanzania wanafanya, lakini hatuyaoni na hatuyajuo, hivyo natoa wito kwa Diaspora wetu, anekanikeni basi, inaumiza kila siku unaona diaspora wa wenzetu, na kujiuliza diaspora wetu wako wapi na wanafanya nini?.

Sasa mimi mwandishi wakp wa habari na mtangazaji wa kujitegemea, Pascal Mayalla, , anayeandaa vipindi vya TV, Redio, makala magazetini na kwenye mitandao ya kijamii, nikifanya kazi kupitia kampuni ya PPR, www.ppr.co.tz, ambayo sasa imetua rasmi nchini Marekani kwa kufungua ofisi, nimejotolea kuandaa vipindi vya mchango wa diaspora wa Tanzania kwa maendeleo ya taifa.

Kipindi Kipya cha TAK
TAK ni kipindi kipya cha TV chenye lengo la kuiangazia Tanzania Kitaifa, Kikanda na Kimataifa kuhusu mambo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii, ambayo yanaihusu Tanzania kwenye medani za kimataifa, kama issues za Umoja wa Mataifa, Jumuiya ya Madola, issues za kikanda na kimataifa, AU, SADC, AfCFTA, Bunge la Afrika, Bunge la EAC, Jumuiya ya Africa Mashariki, EAC na mambo mengine ya kimataifa. Kipindi hiki kitaimulika Tanzania kwenye mikutano ya kimataifa, ukiwemo mchango wa Diaspora wa Tanzania, na wakati huo huo kuangazia fursa mbalimbali za kimataifa kwa Watanzania kuzichangamkia.

Kipindi hiki kitarushwa kwenye local channels za TV za Tanzania, DSTV, Star Times na kwenye online media.

Mimi kama Mtanzania Mzalendo, ninaumia sana kila ninapoona diaspora wa wenzetu wanafanya mambo makubwa ya kuonekanika, na kujiuliza Diaspora wetu wanafanya nini?, mbona hatuwaoni?, hivyo napenda kuona Tanzania tunafaidika na mchango wa wana diaspora wetu wenye exposure kubwa huko walipo, kuitumia kulisaidia taifa letu kisiasa, kiuchumi cha kijamii.

Paskali
Rejea za Mwandishi Kuhusu Diaspora
Diasporas wetu ni ma atheists tu na kazi ya kutumia maneno magumu ya kiingereza hapa JF na X tofauti na hapo kujisifia tu wapo mtoni. Hongera kwa huyo Dada!
 
Local imekuwa saturated sasa inatakiwa uende kimataifa, habari za Tanzania kimataifa ni chache tena zinatolewa na waandishi wakiwa Nairobi au Johannesburg.

Kazi hii ya kuhabarisha kimataifa kwa kiEnglish tunakupatia wewe maana ni kama hakuna waandishi wote kwa kiswahili wameshamaliza mchezo yamebaki manyoya, ila ukijikita kwa KiEnglish utakuwa Millard Ayo, SnS, Michuzi n.k kwa ujio wa kiingereza kwa soko la nyumbani na kimataifa pia.
Asante kwa ushauri,habari inafanywa na waandishi wanaoitwa reporters,mimi stage hiyo nimeipita kitambo,sasa nafanya tuu programs, TAK sio program ya news ,ni program ya analysis,hili eneo bado halina watu wa kutosha。Vyombo Vya Habari Vya Tanzania, Havina Uwezo wa Uchambuzi wa Habari, News Analysis-Jicho Letu
P
 
Kaka Mimi naomba tu kupata fursa huko nje ya kazi hata za kufanya usafi, nk cz nataka kuachana na kazi yangu ya Media Producer & Graphics designer. Asante
Nafungua Bureau huku,nitaajiri Watanzania,hivyo muda muafaka ukifika,huna haja ya kubeba box, utaendelea na media production yako, the only problem ni it takes time。
P
 
Shida kubwa ni siasa za chama chako pendwa, acha kutupia lawama na maswali yasiyojibika kwa hao diaspora waliokimbia nchi kwasababu za kisiasa na hali ngumu ya uwekezaji.
sio diaspora wote wameikimbia nchi kwasababu za kisiasa,au hali ngumu ya uchumi,wako diaspora kibao walikwenda kimasomo,wakawa porched for brain drains na kupewa decent jobs。
p
 
Kuvamia mahali ni mtu asiye na access ya mahali hapo, media zote ni public access places,RC ni president of regional,has all the rights to Access to all public places including Clouds media, hivyo hakuvamia。
Kwa maelezo ya wale vijana wa clouds walishurutishwa kurusha hewani maudhui ambayo RC alikuja nayo pale studio, huo ni uvamizi
 
Back
Top Bottom