TANZIA Dida Shaibu, mtangazaji wa Wasafi FM afariki Dunia

TANZIA Dida Shaibu, mtangazaji wa Wasafi FM afariki Dunia


Inadaiwa alikuwa amelazwa kwa Matibabu Muhimbili.

Amefariki usiku wa leo.
---
TANZIA: Aliyekuwa Mtangazaji wa Kipindi cha Mashamsham cha Wasafi FM, Khadija 'Dida' Shaibu, amefariki dunia usiku wa leo Oktoba 4, 2024 wakati akipata matibabu katika Hospitali ya Muhimbili

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na mtangazaji mwenzake, Maulid Kitenge, kupitia mtandao wa X, Dida alikuwa amelazwa Hospitalini hapo baada ya kuugua.
Inna li Llahi wa inna Ilayhi rajiun.
 


Heeey, maamboo...!!!?

Long kitambo sio, miss you more and too.

Miss the labydaby of JF shenanigans 😉.

Nice to meet you again here, still counting 2024 and the number is going on....

Let's keep counting and rolling....

Weeeh, hebu niweke kalamu chini maana nikianzaga kuandika naunga tuu kama behewa la kwenda kwetu Tabora.

Adios 👋.
 
Mwendo kaumaliza na uke wake kautendea haki kwa ndoa za kutosha.

Ikitokea waliokuwa waume zake tu waamue wote kwenda, wanatosha kubeba jeneza na kuchimba kaburi.

Apumzike kwa amani.
Duh inaonekana unamjua snaaaa
 
Ndugu zanguni duniani hakuna mkamilifu na hakuna mtimilifu....Sisi sote kila mmoja wetu kwa namna moja au nyingine tuna upande wetu mweusi wa maisha yetu........

Si vyema kuwananga kwa sifa mbaya wenzetu waliotangulia mbele za haki bali iwe kama ukumbusho kwetu kwani sote safari yetu ni moja na hakuna ajuaye siku wala saa......

Mapungufu ni maumbile yetu lakini tumuombe mola tuwe na mwisho mwema.....kwani umbali uliopo baina ya kifo na mwanadamu ni karibu zaidi ya umbali wa kiatu na unyayo wake......

Tujitahidi kufanya stara kwa binadamu mwenzetu huku tukizidi kumuomba Mungu atupatie mwisho mwema na moyo wa kuyaacha mabaya ya wazi na yale ya sirini........

Hatupaswi kuogopa kifo bali tunapaswa kujiandaa na maisha baada ya kifo.....kwani hofu na mashaka haviondoi siku ya kufa bali matendo yako mema ndivyo vitakuweka Pema.........

Sisi sote ni wa mwenyezi Mungu na kwakwe tutarejea........
 
Si vyema kuwananga kwa sifa mbaya wenzetu waliotangulia mbele za haki bali iwe kama ukumbusho kwetu kwani sote safari yetu ni moja na hakuna ajuaye siku wala saa......
Kikubwa wewe uliyehai ishi kws wema. Huo ndio ulinzi pekee.....la utasemwa kwa yale uliyotenda nakuishi.

Kama hutaki kusemwa vibaya ukifa basi tenda wema usemwe kwa hayo.
 
Back
Top Bottom