Dini ni kwa ajili ya "Low minded people", Genius can't be trapped!

Dini ni kwa ajili ya "Low minded people", Genius can't be trapped!

Hakuna wanasayansi anakataa kuwa vitu vyote vimeumwa na nguvu ya asili ila wanasayanyi wanachosema ni kwamba hiyo nguvu aijitambui
Wapo wanaokataa...wapo wanasayansi ambao hawaamini katika uumbaji na wapi wengi tu acha uwongo...
 
Mimesoma andiko la mpumbavu mmoja hivi leo.
Nasikitika andiko hili kuandikwa na mtu wa viwango vya chini vya uwezo wa akili.Umeshindwa kujenga hoja kabisa ingawa inaonesha hujui vitu vingi kuhusiana na unayozungumza

Sent from my Infinix X626 using JamiiForums mobile app
Pole...we andika vitu vyenye mantiki kulipinga bandiko! the rest na wewe unakua ni wale wale!
 
Skia mkuu tusipotezeane mda...yaishe umeshinda
Sipo hapa kushindana na mtu, bali nataka kuwaonyesha ni jinsi gani mlivyo vilaza, mbawasumbua watu na kuwapoteze muda hoja hamna mmekalia ujinga na uvivu wa kufanya utafiti.
 
Wapo wanaokataa...wapo wanasayansi ambao hawaamini katika uumbaji na wapi wengi tu acha uwongo...
Wewe aujaelewa wao wanakataa kuwa vitu vimeumbwa na mungu ila awakatai kuwa vitu vimeumbwa ..ndiyo maana unasikia wakisema bigbang yaani mlipuko wa uumbaji
 
Hujakanusha mantiki niliyoiandika.

Kumuamini Mungu unaruhusiwa, hiyo ni haki yako ya kikatiba.

Katiba ya Tanzania ina kipengele cha uhuru wa kuabudu ama kuchagua kutoabudu. Siwezi na sitaki kukuingilia kwenye uhuru huu kama mimi nisivyotaka uniingilie.

Katika Universal Declaration of Human Rights ya UN, una haki ya kuamini Mungu utakavyo. Hili limepitishwa na Umoja wa Mataifa tangu December 10 1948.

Hili hata mimi nisiyeamini Mungu, nitatetea haki yako ya kuamini Mungu utakavyo.

Kuamini Mungu si issue hapa, after all kuamini Mungu ni issue personal wala sielewi kwa nini ifanyiwe mjadala hapa JF.

Jambo linalojadilika JF ni kutafuta facts, ukweli, si imani tu, je, Mungu yupo kweli?

Ukweli ni zaidi ya imani, kwa sababu, kwenye imani, unaweza kuamini hata uongo. Ukweli upo tu, ukiuamini, usipouamini, upo tu.

Naomba tutenganishe habari za imani tu, na habari za facts.

Hizi habari za Mungu kuwapo ni fact Mungu yupo? ni ukweli Mungu yupo? Au ni imani tu?

Mpaka sasa, hakuna aliyethibitisha Mungu yupo.

Hakuna aliyeweza kuiweka habari ya uwepo wa Mungu kwa misingi ya facts, kwa kuiondoa kwenye imani tupu, kwa kutumia mantiki ya kutafuta ukweli.

Na zaidi, ukizichambua habari za kuwepo kwa huyo Mungu, unaona contradictions na inconsistencies zinazoonesha Mungu huyo hayupo, Mungu huyo ni wa hadithi za kiimani tu zilizotungwa na watu.

Ndiyo maana mpaka leo hakuna mtu aliyethibitisha Mungu huyo yupo.

Hayupo, hivyo huwezi kuthibitisha kwamba yupo.

Ukibisha, thibitisha Mungu yupo.
Sawa, Nakuuliza swali


Maisha ni nini ? Lipi lengo la uwepo wetu duniani kwa mujibu/mtizamo wako ?
 
Yaani bado unaandika ujinga na uongo, ndio maana hata maswali madogo yanakushinda. Unakuja na ujinga mwingine kwamba Musa Myahudi mara Nuhu Myahudi. Hivi unaakili kweli kijana ?

Mpaka Musa anaondoka hapakuwepo Uyahudi, hivi huwa mnasoma na kufanya utafiti au mnaandika andika tu ilimradi ?

Ukijadiliana na Mimi hakikisha kila nukta unayo iandika unaijua na uweze kuitolea ushahidi. La Muhammad hujalimaliza unakuja na lingine tena ambalo huliwezi.

Nani alikwambia mitume na manabii wanatoea tokea tu, pasi na sababu ? Kwanza malizia hilo la kwanza, kisha tuje katika huu ujinga na uongo mpya uliouweka tena hapa.
Mkuu unajua maana ya uyahudi kweli?
Au umeongea kwa sababu uliyemwambia pengine haelewi hicho ulichoongea?
Uyahudi imetokana na kabila la Yuda walipoungana na baadhi ya makabila ya Israel na yuda au Yehudah (Au mmezoea kuita Yuda)..

Sasa unasemaje musa hakuwa Myahudi.. Kati ya Musa na Yuda (Yehudah) nani ancestor wa mwenzake...
 
Sawa, Nakuuliza swali


Maisha ni nini ? Lipi lengo la uwepo wetu duniani kwa mujibu/mtizamo wako ?
Maisha ni mfumo wa kuendelea kwa viumbehai kufanya mambo kama kula, kufanya metaboli, kutoa uchafu, kupumua, kusogea, kukua, kuzaana na kuzijibu stimuli za kutoka nje.

Unapotumia neno "lengo" unatoa picha kwamba kuna kitu maalum kimelengwa kwa sisi kuwapo, huu ni mtizamo wa kidini, kwamba, kuna muumbaji, muumbaji ana lengo, na katuweka hapa duniani kutimiza lengo.

Ama pia unaweza kuwa ni mtizamo wa kwamba kuna special design, mambo yamepangwa, sasa unatafuta kujua mpango umepanga kwenda wapi?

Ukiondoka kwenye habari za dini/ special design, ambako mimi sipo, hakuna lengo maalum la sisi kuwapo hapa.

Evolution is driven by random mutations. There is no special direction it is taking, other than natural selection.

Baiolojia inaweza kufanya mambo fulani yawe kama malengo. Kwa mfano, kuzaana ni kitu ambacho kibaiolojia kimekuwa kama lengo. Ubongo na mwili wako umefanywa kibaiolojia kupenda kufanya mambo ambayo yatahakikisha tutaendelea kuzaana. Unapenda kula, unapenda kufanya mapenzi, unasikia maumivu ukiunguzwa na moto, na inevitably ukiishi sana kwa kula na kufanya mapenzi, na kuepuka kuunguzwa na moto, chances are, utapata mtoto na kizazi kitaendelea.

So, hapo utaona mazingira yetu yametuwekea malengo ya kiasili kama hayo ya kuzaana, lakini huwezi kusema kwamba lengo la sisi kuwapo ni kuzaana, kwa sababu kuna watu wengi wanaishi vizuri tu bila kuzaana na wame adopt watoto, au wanaishi bila watoto.

Maisha hayana lengo, hii habari ya lengo ni habari ya kidini.

Ila, hilo halikuzuii wewe binafsi kuyapa lengo maisha yako. Kwa mfano, mtu anayezaliwa katika nchi inayotawaliwa kidhalimu au kikoloni, akayapa maisha yake lengo la kuikomboa nchi yake ijitawale, akapigania hilo mpaka kulifanikisha, anakuwa kaishi maisha yenye maana sana kwa watu wengi sana.

Mtu aliyeona jamii yake haina madaktari wa kutosha, inasumbuliwa na mambo ya afya, akasoma ili kuongeza madaktari, akafanya lengo la maisha yake ni kupunguza matatizo ya afya, akafanikiwa sana kwenye hilo, anakuwa kayapa maisha yake maana kubwa sana.Tunao hawa wengi sana.

Hivyo, maisha hayana lengo, wewe mtu unayeishi ndiye unayapa maisha yako lengo.

Maisha ni kama gari. Wewe ni dereva. Gari halina pahali linapokwenda. Wewe dereva ndiye una safari, una sehemu unataka kwenda, wewe ndiye unaamua gari liende wapi, au hata kusema hutaki safari, unataka kupumzika tu.

Ndiyo maana hata hiyo evolution iliyokuwa inaenda kwa random mutation na natural selection, siku hizi watu wanaiingilia kwa gene editing/ CRISPR, tunaenda kwenye cybernetic organism na artificial intelligence.

Tunaamua baiolojia yetu iweje, maisha yetu yaweje.

Tunayapa maana na malengo tunayotaka maisha yetu, hatuulizi lengo la maisha ni nini.
 
Mkuu unajua maana ya uyahudi kweli?
Au umeongea kwa sababu uliyemwambia pengine haelewi hicho ulichoongea?
Uyahudi imetokana na kabila la Yuda walipoungana na baadhi ya makabila ya Israel na yuda au Yehudah (Au mmezoea kuita Yuda)..

Sasa unasemaje musa hakuwa Myahudi.. Kati ya Musa na Yuda (Yehudah) nani ancestor wa mwenzake...
Ngoja nikufundishe jambo. Uyahudi una maana nne. Katika maana hizo nne ni maana Moja pekee inayo rejea katika kabila.

Uyahudi sio kabila sababu uzao wa mtoto wa Yakubu aloyeitwa Yahudha (Yuda) haipo tena sababu ulisambaratika katika yale mapigano ya dola mbili zilizo anzishwa na mtoto wa Suleyman aliye itwa Yarbiam na mwenzake aliyeitwa Rahbiam. Hawa walikuja kuanzisha dola mbili zama hizo kwa kukusanya dhuria wa nabii Yakubu, na kilikuwa kimepita kitambo kirefu sana.

Maana nyingine ya tamko Yahudi, ni kurudi nyuma kwa kumtaka msamaha Allah kutokana na matendo maovu waliyo yafanya watu, kadhalika katika maana za tamko hilo ni kurudi kwa sauti za kughuna na kupinga Ngoma, haya yalikuwa yakifanywa na viongozi wa kidini wa zama hizo. Maana ya nne, imenitoka. Ila kwa maelezo zaidi ya Historia ya watu Hawa rejea kitabu kolochoandikwa na mwanachioni aitwae Abdulkaadir Shibatulhamd.

Uyahudi ni dini, na itikadi zao ambazo kwazo zinawatofautisha na wengine, na si nasaba au kabila. Mpaka Musa anaondoka hapakuwepo Uyahudi katika ardhi hii, na hii ni kwa makubaliano ya wanachuoni wote wa Historia, na haijulikani lini kwa hakika Uyahudi ulianza.

Kwahiyo hata huyo Yahudha kipindi wanaunganishwa tena dhuria wake yeye hakuwepo, na hili limefanyika hata nabii Suleyman hakuwepo.
 
Kwahyo Mkuu sitaki kukupinga Imani yako ila nilitaka kuuliza kitu...
Kwahyo Uthibitisho wako kwamba Mungu Yupo ni Wewe Kuwepo?
Mungu ni energy hata mimi na wewe ni energy ...even matter is the ENERGY
 
Hiyo quantum physics ni kithibitisho cha kuwepo mwenyezi mungu kwa wale wenye akili
Hujathibitisha Quantum Physics ni kithibitisho cha kuwapo mwenyezi Mungu.

Huelewi Quantum Physics ni nini.

Quantum Physics inakataa mambo kuwa na uhakika, inaenda na probability, inakataa vitu kuwa na mwanzo mmoja yakini.

Mungu wako ni wa probability?

Mungu wako ni Mungu asiye chanzo yakini?
 
Back
Top Bottom