Dini ya Simba na Yanga inavyodhoofisha maisha ya Watanzania

Dini ya Simba na Yanga inavyodhoofisha maisha ya Watanzania

niliona andiko linalofanana na hili juzi,nikatafakari sana kwakuwa na mm ni shabiki wa timu mojawapo kwakweli simba na yanga imepumbaza raia wengi sana wa taifa hili kiasi kwamba hali inazidi kuwa mbaya na hatuna habari sisi ni mayele,aziz ki.chama na phiri.Saa mbili asubuhi vijana wanadamkia kwenye vilinge vya magazeti wakizozana kuhusu simba na yanga,hao hao saa sita mchana utawakuta kwenye mabanda ya kubeti wakiendeleza mabishano yao mpk jioni.HII NI HATARI SANA KWAKWELI,
 
niliona andiko linalofanana na hili juzi,nikatafakari sana kwakuwa na mm ni shabiki wa timu mojawapo kwakweli simba na yanga imepumbaza raia wengi sana wa taifa hili kiasi kwamba hali inazidi kuwa mbaya na hatuna habari sisi ni mayele,aziz ki.chama na phiri.Saa mbili asubuhi vijana wanadamkia kwenye vilinge vya magazeti wakizozana kuhusu simba na yanga,hao hao saa sita mchana utawakuta kwenye mabanda ya kubeti wakiendeleza mabishano yao mpk jioni.HII NI HATARI SANA KWAKWELI,
Hali ni mbaya sana.

Sent from my CPH1923 using JamiiForums mobile app
 
Kwani Tanzania ndo nchi pekee inayo jadili mpira tu au acheni watu wale raha yao kama wewe hupendi mpira tulia kwako
 
Inasikitisha na kushangaza sana.

Miaka zaidi ya 60 ya Uhuru,nchi ambayo inasemekana tuna utajiri wa maji kuliko nchi yoyote ukanda huu wa maziwa makuu na pengine Afirka nzima,leo tunajadili swala la mgao wa maji.Tena Kuna wengine wameenda mbali zaidi kwa kuandika makala za kuwasifia Waislamu jinsi walivyo na ukarimu kiasi Cha nyumba zao za ibada kutoa maji ya bure.Yani Tanzania leo karne ya 21 tunalia kuhusu uhaba wa maji Safi ya kunywa?

Mwaka 2013 gazeti Moja maarufu liliandika makala "Sasa Tanzania uhaba wa umeme basi.Kuuza nje ya nchi jirani pia" .

Leo mwaka 2022 tukiwa tunaumaliza tukiwa tunakaribia 2023,miaka 10 baada ya kuisoma ile makala ya siasa ila bado umeme Ni kizungumkuti,majenereta yanaunguruma kila sehemu,umeme unakatika kila saa.

Katika Dunia hii ambayo matumizi ya internet yamepelekea kuajiri vijana wengi hapa nchini,maana ajira ni kitendawili,wao wanazidi kupunguza matumizi ya data(mb) kila siku na serikali hakuna kitu inafanya.Ukiuliza unajibiwa gharama za uendeshaji zimeongezeka. Siku hizi kila siku najiunga kifurushi cha wiki.Kila siku napata meseji za hongera tu kutoka Airtel na Voda. "Hongera, umefanikiwa kujiunga kifurushi cha wiki, umepata mb 350 kwa TSH 1000" baada ya masaa mawili bando limekata,unajiunga tena Kisha tena unaambiwa hongera!!!

Mambo mengi sana,ila Kuna kitu huwa najiuliza..

Hivi ile nguvu ya watanzania , mashabiki wa club ya Simba kuandamana pale uwanjani siku wanatoka droo na timu ya KMC (narudia siyo Simba walifungwa ila ilikuwa draw),ile wanaandamana kuanzia uwanjani tena usiku "hatumtaki Matola" inatoka wapi? Au yanga juzi tu hapo kutolewa club bingwa wakaangukia shirikisho,huko clabuni ilikuwa mshike mshike nusura kocha afukuzwe.Droo na Simba ikamwokoa,ila timu ngefungwa ingekuwa balaa kwake. Mashabiki na viongozi linapokuja swala la timu hizi za kariakoo hawataki mchezo!! Wanalala mbele na wewe.

Kuna ambao hawajanielewa point yangu kwa nini nimechanganya Simba na Yanga hapo.

Ni hivi; ule uchungu ambao timu za Simba na Yanga zinapopitia misukosuko kwa nini hawa watanzania hawana uchungu Kama huu linapokuja swala la kitaifa/nchi pale mambo ya hovyo yakifanyika?

Yale maandamano Tena ya bila kulazimishwa ya hawa watanzania katika hizi timu mbili kwa nini hatuoni yanajitokeza pale viongozi wakifanya mambo ya hovyo?

Ukiangalia juu juu unaweza sema Watanzania Wanapenda michezo ndiyo maana hutokea hayo mambo,ila ukweli watanzania Wanapenda Simba na Yanga na siyo michezo.

Hapa Tanzania Simba na Yanga ni dini kamili.

Watanzania Wanapenda Simba na Yanga kuliko wanavyoipenda nchi yao.

Mpaka najiuliza;Au CCM ndiyo wametuletea Simba na Yanga ili tuwe mazezeta,huku wao wanakula kiulaini na familia zao,sisi tuwe bize na dini hii ya Simba na Yanga?

Ukipita kwenye vijiwe vyote kuanzia vya kahawa,machinga,daladala hadi vya maofisini mjadala Ni Simba na Yanga tu .."Wewe mwaka huu huna timuuu".."Nakuambiaje kesho ukitetema nite mbwa nimekaa pale"..Ukiwa kwa mbali unaweza dhani wanajadili mambo ya maana labda maisha yamekuwa magumu lakini Kuna watu wanalamba asali na kula kwa urefu wa kamba kiulaini.Kumbe wapi,ni Simba na Yanga.

Alafu ni CCM Kama wameshatujulia, media houses zote kuanzia asubuhi hadi jioni vipindi vikubwa vinavyopewa airtime Ni michezo na zaidi Sana kuzijadili Simba na Yanga.Watu hawana mijadala na gharama za bando,mchele umefika buku 3,chapati jero, na maji ya mgao.Kwake Simba ikshinde Kisha akimbilie redioni kusikiliza uchambuzi wa Edo kumwembe pale wasafi FM.

Maumivu ya kuibisa bando ashayasahau. Anasahau Kama dakika 10 zilizopita alikuwa anajibizana na mheshimiwa Nape Twitter kuhusu kupungzwa kwa kifurushi alafu hakuna taarifa.Mtwnie tu basi tuandamane kupinga huu uonevu. Thubutuuu. Subiri Sasa Yanga wafungwe leo na club africaans ya Tunisia ndiyo utawajua wabongo akili zao. Dakika 0 wamejaa saramander tower wanamtaka engineer Hersi ajiuzulu. Ukiuliza nani aliwaambia waandamane hadi pale,jibu hakuna ila uchaguzi CCM wanaiba kweupe wote tumeweka masikio yetu majumbani kwetu tukifatilia maandamano Jf.Tukimsubiri Lisu aandamane kwa niaba yetu kudai katiba mpya.

Aliyetuletea dini ya Simba na Yanga ametuweza Sana watanzania.Nadhani hata maisha yawe magumu Kama ya Afganistan au tuwe na ukame kuliko Somalia na Ethiopia, CCM wanaweza kuongea na TFF wapange mechi ya dharura Kati ya Simba na Yanga, Kisha wakaongea na media houses zote wiki nzima mjadala uwe mpira ili wapoze malalamiko ya maumivu ya maisha magumu na ukame. Na hakuna kitu tutafanya.

Hii dini ya Simba na Yanga inadhoofisha Sana maisha ya watanzania kwa kweli.

NB: Huu siyo uzi wa michezo mods wasije kuhamisha
Kuna uwezekano mkubwa hukuwahi kulizingatia somo la ufahamu na ufupisho, wakati unasoma. Siyo kwa maelezo yote haya.
 
1-Kwahyo tukiacha kujadili simba na yanga ndio maendeleo yatakuja?
2-Kwani kuanzia tuanze kuzijadili simba na yanga miaka nenda rudi ni club gani imeleta ubingwa wa afrika?
3-simba na yanga zimejibrand miaka nenda rudi ndio maana leo hii zinazungumziwa sana. Kwanini na wengineo wasijibrand?
4-uwanja wa mkapa ukijaa full house sio mapato kwa serikali?
5-hivi vilabu viwili hujiulizi vimetoa ajira ngapi mpaka sasa je sio maendeleo?
 
1-Kwahyo tukiacha kujadili simba na yanga ndio maendeleo yatakuja?
2-Kwani kuanzia tuanze kuzijadili simba na yanga miaka nenda rudi ni club gani imeleta ubingwa wa afrika?
3-simba na yanga zimejibrand miaka nenda rudi ndio maana leo hii zinazungumziwa sana. Kwanini na wengineo wasijibrand?
4-uwanja wa mkapa ukijaa full house sio mapato kwa serikali?
5-hivi vilabu viwili hujiulizi vimetoa ajira ngapi mpaka sasa je sio maendeleo?
Mkuu adriz kosa langu Mimi liko wapi hasa,?

Mvona mtu anatoka povu hivi?
 
Inasikitisha na kushangaza sana.

Miaka zaidi ya 60 ya Uhuru,nchi ambayo inasemekana tuna utajiri wa maji kuliko nchi yoyote ukanda huu wa maziwa makuu na pengine Afirka nzima,leo tunajadili swala la mgao wa maji.Tena Kuna wengine wameenda mbali zaidi kwa kuandika makala za kuwasifia Waislamu jinsi walivyo na ukarimu kiasi Cha nyumba zao za ibada kutoa maji ya bure.Yani Tanzania leo karne ya 21 tunalia kuhusu uhaba wa maji Safi ya kunywa?

Mwaka 2013 gazeti Moja maarufu liliandika makala "Sasa Tanzania uhaba wa umeme basi.Kuuza nje ya nchi jirani pia" .

Leo mwaka 2022 tukiwa tunaumaliza tukiwa tunakaribia 2023,miaka 10 baada ya kuisoma ile makala ya siasa ila bado umeme Ni kizungumkuti,majenereta yanaunguruma kila sehemu,umeme unakatika kila saa.

Katika Dunia hii ambayo matumizi ya internet yamepelekea kuajiri vijana wengi hapa nchini,maana ajira ni kitendawili,wao wanazidi kupunguza matumizi ya data(mb) kila siku na serikali hakuna kitu inafanya.Ukiuliza unajibiwa gharama za uendeshaji zimeongezeka. Siku hizi kila siku najiunga kifurushi cha wiki.Kila siku napata meseji za hongera tu kutoka Airtel na Voda. "Hongera, umefanikiwa kujiunga kifurushi cha wiki, umepata mb 350 kwa TSH 1000" baada ya masaa mawili bando limekata,unajiunga tena Kisha tena unaambiwa hongera!!!

Mambo mengi sana,ila Kuna kitu huwa najiuliza..

Hivi ile nguvu ya watanzania , mashabiki wa club ya Simba kuandamana pale uwanjani siku wanatoka droo na timu ya KMC (narudia siyo Simba walifungwa ila ilikuwa draw),ile wanaandamana kuanzia uwanjani tena usiku "hatumtaki Matola" inatoka wapi? Au yanga juzi tu hapo kutolewa club bingwa wakaangukia shirikisho,huko clabuni ilikuwa mshike mshike nusura kocha afukuzwe.Droo na Simba ikamwokoa,ila timu ngefungwa ingekuwa balaa kwake. Mashabiki na viongozi linapokuja swala la timu hizi za kariakoo hawataki mchezo!! Wanalala mbele na wewe.

Kuna ambao hawajanielewa point yangu kwa nini nimechanganya Simba na Yanga hapo.

Ni hivi; ule uchungu ambao timu za Simba na Yanga zinapopitia misukosuko kwa nini hawa watanzania hawana uchungu Kama huu linapokuja swala la kitaifa/nchi pale mambo ya hovyo yakifanyika?

Yale maandamano Tena ya bila kulazimishwa ya hawa watanzania katika hizi timu mbili kwa nini hatuoni yanajitokeza pale viongozi wakifanya mambo ya hovyo?

Ukiangalia juu juu unaweza sema Watanzania Wanapenda michezo ndiyo maana hutokea hayo mambo,ila ukweli watanzania Wanapenda Simba na Yanga na siyo michezo.

Hapa Tanzania Simba na Yanga ni dini kamili.

Watanzania Wanapenda Simba na Yanga kuliko wanavyoipenda nchi yao.

Mpaka najiuliza;Au CCM ndiyo wametuletea Simba na Yanga ili tuwe mazezeta,huku wao wanakula kiulaini na familia zao,sisi tuwe bize na dini hii ya Simba na Yanga?

Ukipita kwenye vijiwe vyote kuanzia vya kahawa,machinga,daladala hadi vya maofisini mjadala Ni Simba na Yanga tu .."Wewe mwaka huu huna timuuu".."Nakuambiaje kesho ukitetema nite mbwa nimekaa pale"..Ukiwa kwa mbali unaweza dhani wanajadili mambo ya maana labda maisha yamekuwa magumu lakini Kuna watu wanalamba asali na kula kwa urefu wa kamba kiulaini.Kumbe wapi,ni Simba na Yanga.

Alafu ni CCM Kama wameshatujulia, media houses zote kuanzia asubuhi hadi jioni vipindi vikubwa vinavyopewa airtime Ni michezo na zaidi Sana kuzijadili Simba na Yanga.Watu hawana mijadala na gharama za bando,mchele umefika buku 3,chapati jero, na maji ya mgao.Kwake Simba ikshinde Kisha akimbilie redioni kusikiliza uchambuzi wa Edo kumwembe pale wasafi FM.

Maumivu ya kuibisa bando ashayasahau. Anasahau Kama dakika 10 zilizopita alikuwa anajibizana na mheshimiwa Nape Twitter kuhusu kupungzwa kwa kifurushi alafu hakuna taarifa.Mtwnie tu basi tuandamane kupinga huu uonevu. Thubutuuu. Subiri Sasa Yanga wafungwe leo na club africaans ya Tunisia ndiyo utawajua wabongo akili zao. Dakika 0 wamejaa saramander tower wanamtaka engineer Hersi ajiuzulu. Ukiuliza nani aliwaambia waandamane hadi pale,jibu hakuna ila uchaguzi CCM wanaiba kweupe wote tumeweka masikio yetu majumbani kwetu tukifatilia maandamano Jf.Tukimsubiri Lisu aandamane kwa niaba yetu kudai katiba mpya.

Aliyetuletea dini ya Simba na Yanga ametuweza Sana watanzania.Nadhani hata maisha yawe magumu Kama ya Afganistan au tuwe na ukame kuliko Somalia na Ethiopia, CCM wanaweza kuongea na TFF wapange mechi ya dharura Kati ya Simba na Yanga, Kisha wakaongea na media houses zote wiki nzima mjadala uwe mpira ili wapoze malalamiko ya maumivu ya maisha magumu na ukame. Na hakuna kitu tutafanya.

Hii dini ya Simba na Yanga inadhoofisha Sana maisha ya watanzania kwa kweli.

NB: Huu siyo uzi wa michezo mods wasije kuhamisha
Na siku hizi kukikucha tu asubuhi, huku kuna George Ambangile kule kuna Bin Kazumari yaani ni mwendo wa vipindi vya michezo asubuhi kabla hata ya watu kunywa chai
 
Picha nimepiga mtaa dukani hivi maeneo ya Yombo Vituka hiko kijiwe mijadala yao siku zote Simba na Yanga tu ,unaweza pita ukasikia watu wanavyobishana kwa nguvu kubwa utaweza kudhania kuna jambo muhimu sana linajadiliwa.
IMG_20220915_091317.jpg
 
Picha nimepiga mtaa dukani hivi maeneo ya Yombo Vituka hiko kijiwe mijadala yao siku zote Simba na Yanga tu ,unaweza pita ukasikia watu wanavyobishana kwa nguvu kubwa utaweza kudhania kuna jambo muhimu sana linajadiliwa.View attachment 2405971
Ila mkuu huu ukuda sasa.😂😂

Poker njoo ushuhudie hii.Watu utadhani wanazindua mtaro happy chini Kumbe ukumbusho wa mechi ya shirikisho.
 
1-Kwahyo tukiacha kujadili simba na yanga ndio maendeleo yatakuja?
2-Kwani kuanzia tuanze kuzijadili simba na yanga miaka nenda rudi ni club gani imeleta ubingwa wa afrika?
3-simba na yanga zimejibrand miaka nenda rudi ndio maana leo hii zinazungumziwa sana. Kwanini na wengineo wasijibrand?
4-uwanja wa mkapa ukijaa full house sio mapato kwa serikali?
5-hivi vilabu viwili hujiulizi vimetoa ajira ngapi mpaka sasa je sio maendeleo?
Serikali inabweteka kwa kuona wananchi mazombi kwa sababu ya kuyapa mgongo mambo ya msingi na kuwekeza muda mwingi katika kujadili Simba na Yanga , hata ukichunguza kwa bongo ni raia wachache sana wanaojua mambo muhimu kuhusu nchi yao na ulimwengu kwa ujumla hata kwa uchache .

Ndio maana vijiweni wakianza kuongolea habari muhimu utakuta chai nyingi kwa sababu watu wengi uelewa mdogo sana kuliko wanavyozijua na kufuatilia Simba na Yanga . Muhimu kubalance kama wenzetu Misri wale machizi mpira lakini kwenye masuala ya msingi hawayapa mgongo na huwakuti wakiuabudu mpira kama huku tunavyoabudu Simba na Yanga.
 
Serikali inabweteka kwa kuona wananchi mazombi kwa sababu ya kuyapa mgongo mambo ya msingi na kuwekeza muda mwingi katika kujadili Simba na Yanga , hata ukichunguza kwa bongo ni raia wachache sana wanaojua mambo muhimu kuhusu nchi yao na ulimwengu kwa ujumla hata kwa uchache .

Ndio maana vijiweni wakianza kuongolea habari muhimu utakuta chai nyingi kwa sababu watu wengi uelewa mdogo sana kuliko wanavyozijua na kufuatilia Simba na Yanga . Muhimu kubalance kama wenzetu Misri wale machizi mpira lakini kwenye masuala ya msingi hawayapa mgongo na huwakuti wakiuabudu mpira kama huku tunavyoabudu Simba na Yanga.
Michezo ni tasnia ambayo inatoa ajira za kutosha kupitia wachezaji, media, viongozi n.k Na ndio tasnia kubwa kwa sasa Tanzania sasa kwanini watu wasijadili?
 
Michezo inawaweka na kuwaleta watu karibu..

Siasa ya maendeleo inabagua kati ya masikini na tajiri..

Simba sc & Yanga sc wanawaunganisha masikini na matajiri, CHADEMA & Ccm, vipofu wanaona na viziwi wanasikia.

Ukiona mtu haongelei budle kupanda, mgawo wa maji / umeme ujue ameshakubaliana na matokeo.
 
Michezo ni tasnia ambayo inatoa ajira za kutosha kupitia wachezaji, media, viongozi n.k Na ndio tasnia kubwa kwa sasa Tanzania sasa kwanini watu wasijadili?
Naona bado unakaza fuvu kaka.😁
 
Back
Top Bottom