Dini ya Uislam iliwezaje kuenea kwa wingi "Sub Saharan Africa" ilhali waarabu hawakuwa na makoloni huko? Ni biashara pekee ama kuna njia nyingine?

Asante sana kwa maelezo
 
Mh! Kusadikika
 
sasa namimi ndo nashangaa watu wanavolikuza na kuniita mzushi natafuta chokochoko sijielewi etc.
Wakati kitu kidogo tu na ni fact tena isiyo hata ya aibu sasa zile za aibu si nitatukaniwa mama kabisa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Wewe umesema alikuwa akiitwa Al amini = muaminifu.

Hatujakataa kama hajafanya biashara lkn mfanyabiashara gani aitwe muaminifu halafu avamie misafara na kupora kama ulivosema.
 
Umesoma vizuri historia ya waarabu Zanzibar au umejisikia tu kuchangia mjadala
 
Tukubali aliwanunua ikisha ikawaje? Aliwatumikisha?
Hii hadithi ilikuja kwa mnasaba gani? Maana ninachojua hadithi huhadithia jambo.
 
Tukubali aliwanunua ikisha ikawaje? Aliwatumikisha?
Hii hadithi ilikuja kwa mnasaba gani? Maana ninachojua hadithi huhadithia jambo.
[emoji38]The p in Islam stands for 'peace'[emoji18]
Wewe jamaa unaonekana una chuki na waarabu tu. Lkn hujui kama hao waarabu ndio waliokuleteeni vitambaa huko kijijini kwenu na hawakumshurutisha hata mtu mmoja asilimu.
Lkn wamishionari walikuwepo kwa miaka mingapi na walikubatizeni mfuate dini yao huku wakikuacheni na mavazi ya ngozi za wanyama.

Ameeleza hapo Hammaz mbona huweka neno umeshikilia Muhammad alikuwa mfanyabiashara kwani nani alikuwa hajui hilo.
 
Point of correction,Mtume Muhammad saw,aliikomboa mecca iliyokuwa chini ya utawala wa kikurayshi(washirikina)waliokuwa wanaabudu masanamu.
 
Point of correction,Mtume Muhammad saw,aliikomboa mecca iliyokuwa chini ya utawala wa kikurayshi(washirikina)waliokuwa wanaabudu masanamu.
Unanicorrect kitu ambacho hata sijakiongelea...Anyways naomba kujua Kabila la Muhammad
Plot twist:Hao wapagani waliperform Tawaf na kuzunguka Al marwa na al Safa mara 7 maana waliamini kuna Sayari 7 na miungu 7 inazunguka dunia...Muhammad Kaja akawaiga akaiga na kufunga Ramadan Akaiga na Kaaba ya wapagani akaitwist iwe ya kiislam.

Mwanzoni hakuikubali kaaba na aliorder watu kibla iwe Jerusalem lakini wayahudi walipomkataa mtume akageuza kibla ikawa kaaba la wapagani mpaka leo.
 
Wewe umesema alikuwa akiitwa Al amini = muaminifu.

Hatujakataa kama hajafanya biashara lkn mfanyabiashara gani aitwe muaminifu halafu avamie misafara na kupora kama ulivosema.
Alipora baada ya kupata Jeshi...Al amini kipindi icho alikuwa ndezi tu anatumwa tumwa
 
Nani alimfunga breki Ottoman kiasi cha kuanguka!?
 
Baada ya kifo cha Muhammad mwanzoni mwa 630s CE hapo ndo wale majemedari waloachwa walianza kuutanua uislam nje ya mipaka ya uarabuni na kufikia africa ya kaskazin (misri, Libya(Cyrenaica),Tunisia (carthage), Algeria,morroco(Maghreb) na kuteremka kusini mpka Sudan (Nubia), na Kush (Eritrea na Ethiopia).
Kwa sub-sahara Africa uislam ulienea kwa njia zifuatazo.
1:BIASHARA
baada ya kuiteka africa ya kaskazin , kuna misafara ya biashara ilikuwepo kutoka falme za waafrica wa kusin mwa jangwa la sahara (mfano Ghana,Mali na Songhay) ambapo waarabu walikuwa wanapata bidhaa kama chumvi na madini, ngoz za wanyama, meno ya tembo etc. Na kupeleka uarabuni, walijenga misikiti kwenye maeneo mengi na kuwa silimisha wafalme na kupelekea raia nao kusilim.

Huku africa mashariki: Uislam ulifika mapema sana mwanzoni mwa karne ya 8 CE ambapo wafanyabiashara wa kiarabu na kiajemi walifika ufukwe wa pwani ya A.masharik, walijenga misikiti taratib na kusilimisha watu . Licha ya kwamba uislam uliingia Africa mashariki toka karne ya 8CE, ila uliendelea kubaki maeneo ya pwani tuu kwa zaidi ya karne 11 mpaka 1840 ambapo zanzibar ilipokuwa Soko kuu la Biashara ndipo uislam ukaanza kupenya ndani (interior) ya Africa mashariki kutokana na misafara ya biashara (trade routes) iliyokuwepo kama vile Kusini (pwani, lindi, mtwara,ruvuma mpk malawi),kati: bagamoyo, morogoro,dodoma, singida, tabora, kigoma) na Kaskazini: Tanga, k'njaro, mpk kenya. NB: hizi misafara sio kwamba zilkuwa zinapita mkoa mzima, ni baadh tu ya maeneo.

2:VITA VITAKATIFU (JIHAD)
hasa hasa kule Africa magharib kwa leo hii maeneo yalopiganwa vita hivyo ni nchi kama Nigeria, Senegal, Gambia, Mali,Niger. Na watu mashuhuri waloongoza vita hivyo ni Othman Dan Fodio, Al hadj Umar na wengineo. Jamii nyingi zilijikuta zinaacha dini za asili(kumbuka ukristo wakat huo haukuwepo ktk jamii hizo) na kusilim mfano Wahausa. Vita hivi vilianza mwishoni mwa karne ya 18 na mwanzon mwa karne ya 19

3:MAFUNDISHO YA UISLAM
baada ya watu kusilim, hao hao waligeuka kuwa chachu ya kufundisha wenzao. Yaan walim waliendelea kutoa elimu ya kiislam kwa wenzao na kuwashawish wasilim. Unadhifu pia ulichangia uislam kuenea kwa kasi , kwakuwa watu walijiona fahari sana kuvaa KANZU.
Yapo mengi ya kuelezea ila hayo machache yanatosha!!
 
Asante sana mkuu kwa ufafanuzi wako wa kina na wenye kubeba maana kubwa kwangu na kwa wasomaji wengine.
 
Uzi ulikuwa mzuri sana huu tatizo wajinga wameingiza masuala yao ya dini.
 
Hapo zanzibar umeishia kusema soko kuu, Sema hivi soko kuu la watumwa unavyotaka kuwatetea mabwana zako wa kiarabu unaona aibu kusema ukweli kuwa Wali kuwa wanauza waafrika japo wanajikuta dini ni yao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…