Dini zote naomba mnijibu maswali yangu

Dini zote naomba mnijibu maswali yangu

Mhafidhina07

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2014
Posts
3,340
Reaction score
4,659
Naomba nieleweke mimi ni muislamu sijaleta swali kwa lengo la kukejeli ila nataka ufahamu zaidi sitaki kubakia kweny kuta moja kweny hoja hzi.

1, Kwanini mungu hakuleta dini tunazotetea toka kuumbwa kwa huyu adamu?

2, Inakuwaje amewaacha binadamu katika sitonfamu ya imani?

3, Kwanini mitume yenyew haikukusanya na kuandika vitabu badala yake wafuasi ndiyo wamekusanya hadithi na maneno kutoka kwa watu?

4, Maisha/historia ya manabii iweje yawe ni machache kwa maelezo na iweje ya udogoni mwao ikiwemo makosa waliyofanywa hayajaandikwa?

Nimemaliza
 
Naomba nieleweke mimi ni muislamu sijaleta swali kwa lengo la kukejeli ila nataka ufahamu zaidi sitaki kubakia kweny kuta moja kweny hoja hzi.1,kwanini mungu hakuleta dini tunazotetea toka kuumbwa kwa huyu adamu?2,inakuwaje amewaacha binadamu katika sitonfamu ya imani?3,kwanini mitume yenyew haikukusanya na kuandika vitabu badala yake wafuasi ndiyo wamekusanya hadithi na maneno kutoka kwa watu?4,maisha/historia ya manabii iweje yawe ni machache kwa maelezo na iweje ya udogoni mwao ikiwemo makosa waliyofanywa hayajaandikwa?.nimemaliza

Heri ndugu,

Muumba hana dini wala dhehebu ila zilianzishwa na watu,Ibrahimu hakuwa na dini ila baada ya kufa wanae Ishmael na Isaka hawakuongea tena kila mmoja alifata upande wa mama yake na hivyo kupelekea utengano uliozalisha Uislam(uzao wa ishmael) na Ukristo(uzao wa Isaka)

Na pia lazima ujue kwamba Muumba alishasema hata uwe na imani ya kuhamisha milima kama huna upendo si kitu, na katika imani, tumaini na upendo lililokuu ni UPENDO.
Hivyo muumba wetu ambaye ni mmoja yeye ni Upendo.

Lakini ili uweze kuelewa zaidi inabidi ulijue KUSUDI la uumbaji ni lipi? Je ni wengine wawe maskini na wengine matajiri au wengi waumwe na wengine wawe wazima au kifo na mauti ni KUSUDI la Muumba?

Maana ukisoma

Hosea 13:14 Nitawakomboa na nguvu za kaburi; nitawaokoa na mauti; ewe mauti, ya wapi mapigo yako? Ewe kaburi, ku wapi kuharibu kwako? Kujuta kutafichwa na macho yangu.

1korintho 15:26 Adui wa mwisho atakayebatilishwa ni mauti.


Kwa mistari iyo unapaswa kujua Mauti na kifo halikuwa KUSUDI lake na mengine mengi ambayo ndio yanayounda dunia na ulimwengu.
 
Ma mimi nakujibu kama ifuatavyo

1. Kwanza MUNGU hana Dini, Dini zimeletwa na Binadamu, Musa hakuhubiri kuhusu Dini ya kiyahudi, Yesu hakuhubiri kuwa tuwe wakristo, Mohamad kidogo historia yake ndio inachanganya yeye kwenda na kurudi na kusema MUNGU kasema Dini ni uislamu, japo mbali na yeye hakuna shahidi wa kama ni kweli Mungu alihimiza Dini ni uislamu... Ukitizama vizuri Dini ni mapokeo ya utofauti wa kiimani kwa wanadamu wenyewe, ila kwa Mwenyezi MUNGU wote ni wake, na hana DINI. Na DINI haiwezi kukupeleka Peponi kamwe, bali ni matendo mema ya hapa Duniani.

2. Hajawaacha katika sintofahamu, kawaachia neno litakaloishi milele, katika Biblia kuna mstari unasema kama umpendi Jirani yako unayemuona, utampenda vipi MUNGU husiyemuona. Imani ni kuamini katika MUNGU uwepo wake na neno lake, ukiweza kufata neno kwa ufasaha utampendeza MUNGU, imani kali sio mapenzi ya Mungu. Unaweza kudhani Imani kali ndio wanaompendeza Mungu, lakini ukashangaa wanaoingia mbinguni wakawa wale watu uliowaona hawafai kwenye jamii. Hajatuacha tusumbuane kiimani bali anataka tujue ukweli juu yake, anataka tumtafute, tutafute neno lake la kweli basi hapo nasi tutakuwa pamoja nae.

3. Wapo mitume walioandika kwa mikono yao neno la MUNGU, na wapo ambao wanafuasi wao ndio waliandika neno la mungu. Mfano Suleimani (Solomon) inasemekana aliandika baadhi ya maandiko kwenye biblia wakati Yesu yeye maandiko yake yaliandikwa na wanafunzi wake waliokuwa wanatembea nae kila mahali.

4. Maisha ya hawa manabij hayakuweza kuandikwa yote tokea utotoni kwasababu manabii wengine walichaguliwa na MUNGU wakiwa tayari watu wazima mfano Ibrahim, hivyo maandiko ambayo yatakayo kuwa na mashiko ni kuanzia hapo alipochaguliwa na MUNGU. Na maandiko yote katika vitabu vya Dini yameanza kuandika mara moja pale MUNGU alivyoanza kugusa maisha ya hawa manabii. Mfano kina Jeremia, Samwel, Yusufu, Musa, Daudi, Samson, Isaka, Yosia, Yesu hawa maandiko yao yalianza kuandikwa tangu wakuwa wadogo au watoto na kuendelea kwa sababu MUNGU alianza kusema nao tangu wakiwa wadogo. Maandiko yako hayawezi kuandikwa wakati hukusemezana na MUNGU, ukianza kusemezana nae ndipo maandiko yanaanza kuandikwa.
 
Back
Top Bottom