Atomic orbital
JF-Expert Member
- Sep 27, 2020
- 374
- 484
Napenda sana alivokuwa analia kama paka
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hajaweka orodha ya watu wazuri,Bali walioweka recordKwa hyo nayo ni rekodi ya kusema akumbukwe????
Harafu ulivyokuwa huna aibu unawalinganisha hao viumbe vyako na Yesu kundi moja daaah!!!
Mkuu leo umetoa boko!!!
Takataka yako pale juu edit tena.
Umeisha sana mzazi.[emoji1666]Kwenye huu uzi watu mbalimbali wameelezea sababu ya kifo chake..
Salute.
Jana usiku nilikua naangalia muvi ya The Patriot iliyochezwa na Mel Gibson (Director wa muvi ya Apocalypto,Passion of Christ etc) akiwa na Heath Ledger. Ilikua inaonyesha jinsi wamarekani walivypigana kwa uzalendo ili kumuondoa mkoloni ambae ni mwingeleza.
Heath Ledger alinivutia zaidi nafasi alivyoicheza vizuri, lakini nikawa najiuliza kwanini huyu mtu alifariki mapema mnoo? Nikaingia google Nikasoma soma Criminology & Criminal case mbalimbali za mastaa. Nikamalizia na Vifo vya masta.
Kuna vifo mbalimbali vya mastaa vimetokea mpaka leo hii vimetuacha na utata.
Moja kati ya wasanii wenye kipaji kikubwa na waliopendwa sana sana. Ambae alikufa ajili ya Kuzidiwa na madawa ya kulevya wengi wanaamini kua alikua anasumbuliwa na watu wasio julikana kutokana na Nafasi aliyoicheza kama Joker kwenye Muvi ya Batman:The Dark Knight.
- Heath Ledger (Joker)
Kwenye Documentary inayoitwa Too Young to Die iliyoandikwa na mama yake alieleza kua maandalizi ya kucheza nafadi ya Joker Kwenye Dark knight ndio yalisababisha kifo chake. Pia mama yake (Kim) alionyesha Diary ya ledger ambayo alikua anaandika kuhusu muvi anazocheza. Mwisho wa Diary hiyo Ledger alikua ameandika maneno BYE BYE kwa herufi zilizo kolezwa wino (Bolded letters) Inasemekana njia aliyotumia kuipata nafasi ya kucheza kama Joker ilikua inagombewa na wengi.hivyo ilimpelekea akajifungia hotelini na kukutwa akiwa amefariki. Ila huyu jamaa alikua ana bonge la kipaji, kama ulikua hufahamu ile make up ya joker alijifanyia mwenyewe . Ushaona mikono ya joker ina kama unga unga hvi wa rangi? Basi vile alijiwekea makusudi ili watu wajue kua make up alijifanyia mwenyewe.
Bruce lee alipokua na miaka 31 tu tayari alikua mmashakua maarufu dunia nzima kupotia uigizaji wa filamu za mapigano.
- Bruce Lee
Bruce lee kaffariki kwa kifo cha ajabu akiwa na miaka 32. Tarehe 20 mwezi 7 mwaka 1973 Bruce alipewa vidonge vya kutuliza maumivu baada ya kusema anasikia maumivu ya kichwa na aliyekua anahisiwa ni mpenzi wake, mwigizaji Betty Ting pei alipopewa vidonge hivo alienda kulala mpaka leo hii hajaamka tena.Sababu ya kifo chake imekua kitendawili, wapo wanaosema ni mpenzi wake nie aliye muua wengine wanasema ni Wazee wa kichina ndio walio muua (Chinese martial Art) eti kwamba alikua anatoa siri zao za mapigano kwa kupitia muvi zake.
Huyu alikua ni mtoto wa Bruce lee amefariki akiwa na miaka 28, kifo chake pia kilikua ni chaa ajabu. Alikua yupo katika maandalizi ya muvi yake ambayo ndani ya hiyo muvi kulitakiwa apigwe risasi moja, lisasi zilizotakiwa kutumika ni risasi bandia lakini ajabu wakati anapigwa hiyo risasi ilitoka risasi ya ukweli ambayo ilimua hapohapo.
- Brandon Lee
Baada ya kifo chake kuna mambo yalikua yanatokea ambayo yalifanya kifo chske kiwe cha utata zaida. Katika muvi ya mwisho ya Bruce kuna mwigizaji wake mmoja ambae aliuwa kwa kupigwa risasi bahati mbaya, lakini pia kwenye muvi hiyo bruce lee alikua anapambana na Mzimu ambao baadae ulimfuata mtoto wake muvi hii ilishutiwa kabla ya kifo cha Brandon . Matukio hayo yalifanya kesi ya vifo vyao kua ya utata zaidi.
Huyu alikua maarufu zaidi kwa sababu hizi 3. Uhusika wake kama Superman, mahusiano na mke wa Eddie Mannix , Toni Mannix na kifo chake cha ajabu.
- George Reeves(Superman)
Eddie Mannix alikua General manager wa kampuni ya Metro-Goldwyn Mayer.
Moja ya uvimi juu ya kifo cha Reeves watu wanasema Eddie ndie aliyemuua.
Alikutwa amefariki kwenye nyumba ambayo alinunuliwa na mchepuko wake Toni mannix (Wakati anakufa alikua ana mwanamke mwingine) alikutwa amekufa ghorofa ya juu ila chini kulikua kuna wageni.alikutwa na majeraha ya risasi kichwani, risasi 2 zilikua kwenye sakafu bunduki iliyotumika kumuua ilikua imesajiliwa kwa jina la Eddie Mannix. Hakuna aliyeweza kusolve kesi hii mpaka leo hii. Kafariki June 16 1959 (Kipindi hicho Tzania tulikua tunawasha moto kwa mawe huku nyerer akitutafutia uhuru)
Kama umeiona muvi ya First of legend ya Vicent Zhao(Chumanchoko), Kill bill basi utakua umemuona huyo mzee.Alikutwa amefariki ndani ya chumba cha hotel Bangkok Thailand akiwa uchi ananingia juu ya kitanzi. Kesi yake ilikua inachukuliwa kama kesi ya Kujiua. Mke wake annie aliamua kuisimamia kesi ya mume wake akagundua kua aliuwawa. Lakini inasemekana kua aliuwa na watu waliomuuwa Heath Ledger.
- David Caradine
Vifo vingine vya utata ni..
Wengine husema Marylin manroe aliuwa na Boby Kennedy aliwatuma mafia, wengine wanasema doctor wake ndie alimchoma sindano ya sumu.
- Michael Jackson
- Marylin Manroe
- Grace Kelly
- Natalie Wood
Thanks
Tchao.
Da'Vinci
Naona unanijadili,
Salute
Jina Bruce Lee sidhani kama ni jina ngeni kwa mtu yoyote mwenye umri kuanzia miaka 100 mpaka 10, hivyo haiana haja kumzungumzia kua ni nani hasa.! Bruce alikua mwalimu wa kung fu na mgunduzi wa staili za Jet kune-do, muigizaji na mwanafalsafa..Ni moja kati ya binaadamu wachache ambao wameweka rekodi ambazo hazitokuja kuvunjwa baadhi yao ni Leonard Da'Vinci,Yesu wa Nazareth,Genghis khan,Michael Jackson Newton, Paulo wa Tarso (mtume) n.k n.k
Bruce katika maisha yake ya miaka 32 tu aliyoishi hapa Duniani kaacha historia mbalimbali ambayo sidhani kama kuna mtu wa karne hii ya 21 anaweza kuja kuivunja, baadhi ya rekodi alizoaacha amabazo hakuna aatakaye zivunja ni kama vile...
⦁ ●Bruce lee alikuwa anaweza kupiga ngumi karatasi ambazo zinaninginia hewani akazitoboa (Mimi na wewe tukipiga ngumi karatasi tutaichana sio kuitoboa)
⦁ ●Alikuwa na speed kubwa ambapo kipindi anacheza muvi zake walikua wanaweka slow motion ili kuweza kuona apigo yake, inasemekana yeye ndie binaadamu pekee aliyekuwa na spidi kali zaidi kwenye kurusha mateke na ngumi.
⦁ ●Ndani ya sekunde moja alikuwa anaweza kurusha mateke sita.
⦁ Alikuwa anaweza kupiga push-up 1500 kwa mikono miwili bila kupumzika, Push up 400 kwa mkono mmoja, alikuwa anaweza kupiga push up 200 kwa vidole viwili (Mimi sizidi 40 kwa mikono miwili)
Hizo ni baadhi ya rekodi ambazo kaacha Marehemu Bruce tujiulize Bruce alikua anafanya vipi hadi kuweza kuacha alama hizo duniani, pia akaweza kumtengeneza mwanae Brandon nae kiasi chake akafanya makubwa , lengo kuu la kuleta mada hii nimetaka tushee baadhi ya vitu ambavyo alikua anafanya hadi kuweza kufikia kuacha rekodi hizo ambazo zinaishi.
Ukimchunguza Bruce Lee utangundua alikua anatembea na vitu viwili vikuu ambavyo vilimuwezesha kufanikiwa kuacha alama duniani.
1. Bruce alikuwa Integrity Person (Mtu mwadilifu) alihakikisha anafanya kile ananchokifanya kama jinsi kinavyotakiwa kufanyika..kwa kujituma na kwa moyo wake wote.
2. Bruce alikuwa Disciplined Person (Mtu mwenye Nidhamu) alikuwa ana nidhamu ya hali ya juu hasa kwa kile anachokifanya.
Basi lengo la mada yangu ni kuangalia jinsi Nidhamu katika vile vitu tunavyofanya yaweza kutufikisha katika hatua ya kutimiza malengo mbalimbali ambayo tumejiwekea. Bruce alikua na nidhamu katika mchezo wa ngumi ndio maana kafanikiwa kutengeneza historia na rekodi hizi ambazo leo hii twazisoma. Ili kutimiza malengo yake aliweza kutengeneza Formula yake akawa anaiheshimu na kuifuata wote yaweza kutusaidia katika kufanikisha kufikia vile vitu ambavyo tunatamani kuvifikia maishani (Malengo)....Tuipitie.
⦁ ●Je wewe ni Mwanfunzi/ Kuna kitu unajifunza? Kama jibu ni Ndio basi nenda kafanye mazoezi juu ya kitu hicho (kajisomee)...kama jibu ni Hapana basi tafuta kitu ambacho hukiwezi na unapenda kujifunza kisha kakifanyie mazoezi/Kajisome.
⦁ ●Je katika taaluma yako kuna mtu ni bora zaidi yako? Kama jibu ni Ndio basi Endelea kujifunzana kufanya mazoezi... Kama jibu ni Hapana basi nenda katafute mtu ambae ni bora zaidi katika taaluma yako jilinganishe nae kisha kafanye mazoezi/kajifunze zaidi
⦁ ●Je umemaliza kujifunza/kufanya mazoezi? Kama jibu ni Ndio basi nenda kalale upumzike, kisha amka endelea kufanya mazoezi /kujifunza...Kama jibu ni Hapana basi Endelea kufanya mazoezi.
⦁ ●Je Uko unafanya mazoezi/unajifunza muda huu?
Kama jibu ni Ndio basi endelea kujifunza kila kitu kilichoko mbele yako na kamwe usiache kujifunza vitu Vipya.
Hizo hapo juu ni kanuni alizo jiwekea Bruce lee ili kuweza kutimiza malengo yake, hivyo basi kama utaona yanafaa ili kutimiza malengo yako basi yafuate. kama unagonga Code ndelea kujifunza na kufanya mazoezi siku moja utatoboa, kama ni mtu Mechanical endelea kujifunza na kufanya mazoezi siku moja utatengeneza gari lako, kama unataka kuplan Heist (Wizi wa kutumia akili) endelea kujifunza jinsi ya kufanikisha tukio lako siku moja utafanikisha, Kama unatamani siku moja uje kua mwanasiasa na mwandiplomasia bora endelea kujifunza siku moja utaacha historia nzuri kwenye taifa lako...Nidhamu ndio kila kitu katika kufanya kitu ulichokusudia,heshimu unachofanya na ukipendehata kama watu wengine wanakubeza "I assure you brother one Day sun will shine to You" Brothers n Sisters hatukuumbwa kushindwa, mafanikio ndio hatima tuliyopewa ila tutayapata pale tu tutakapo weka nidhamu kwa yale tuyafanyayo. Never Give up! Never stop Learning, Dont Never in anything.
Twaweza ku-Achieve kila tunachotamani kama tutatembea na vitu hivi vitatu..
▪Discipline ▪Integrity ▪Ambition
wake up mate, the future is on your Hand
-Learning Never Exahust Mind!
Leonardo Da Vinci
~Da'Vinci
_ Exclasior
Ndani ya sekunde moja alikuwa anaweza kurusha mateke sita.
Hayo mapambano yalikuwa ya mashindano gani na alipambana na kina nani?Yawezekana ni kweli bruce lee ana rekodi ya kutowahi kupigwa hata siku moja. Pambano ambalo hakushimda alikua anamiaka 13 kama sijasahau..alitoka Draw
Mita 100 kwa sekunde 10 kasoro hii inawezekana. yaani kwa kila sekunde 1 alikuwa anaruka mita 1 na point kadhaa tufanye mita 1.2 hivi.Mbona Usain bolt alikua anakimbia kwa sekunde 9. Mita za kutosha
Najaribu kucalculate hilo suala jibu haliji, Mateke 6 kwa sekunde 1, nimeapply logarithim hola, nimepiga mpaka integration by part lakini sipati jibu 😂Sasa jamani kwahiyo walimsemea uongo??
Sekunde moja taa mateke sita.its imposibbleHa Ha ha unajua Sekunde ni ndogo sana ndio maana inatia mashaka