Diwani Athumani Msuya atenguliwa Ikulu

Diwani Athumani Msuya atenguliwa Ikulu

Naona baada ya Diwani kutenguliwa kila mtu anakuja na dhana yake na kuipa uhalali . WABONGO NI WAZUSHI JAMANI!!! Halafu ukiwa lofa unaweza kuamini kila UJUAJI unaoletwa humu.

Halafu akili za wengi zinatafsiri negatively kwa kila jambo. Yaani mtu hawezi kuiruhusu akili yake ikawaza kuwa ni mabadiliko ya kawaida baada ya Mhe Rais kubaini au kushauriwa kuwa hastahili pale kutokana na nafasi aliyokuwepo awali ya DGIS.
Kesho atakapopewa nafasi nyingine utasikia FIX za wana JF humu. Wengine watasema NILIJUA TU
 

Breaking: Rais Samia Atengua Uteuzi wa Kamishna Diwani​





Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ametengua uteuzi wa Kamishna Diwani Athumani Msuya, aliyemteua tarehe 03 Januari, 2023 kuwa Katibu Mkuu Ikulu

Amemteua Bw. Mululi Majula Mahendeka kujaza nafasi hiyo. Hapo awali Bw. Mahendeka alikuwa Afisa Mwandamizi wa Ofisi ya Rais, Ikulu.
 
Yaani nikutoe kwenye taasisi nyeti nije kukuweka kutongoza kasehemu ambako ndiko kanakoratibu mambo yangu. Yaani Washauri wa Rais sijui niwaambie nini. Yaani mtu demoted to such a junior position mnamuweka hapo kweli? Huyo kiutaratibu anapangiwa Ubalozi au kuwa nyumbani maana popote atakapopelekwa nchini ni Sawa na junior position kwake. Yaani kifupi Wakurugenzi wakitoka huko Idarani iwe kustaafu au kustaafishwa wanabaki nyumbani kwao au kupelekwa nje. No more.
 
Huko ubalozini unazani ana ripoti mbinguni??

Sio kila anae ondolewa ktk teuzi amemgomea Mh.

Kumgomea ni kosa la uhaini... Uhaini sio kupindua nchi pekee...

Fahamu tafsiri sahihi ya kosa la uhaini na adhabu yake​


Fahamu tafsiri sahihi ya kosa la uhaini na adhabu yake
Uhaini ni kosa la jinai, kwa tafsiri nyepesi ina maana kwamba ni kosa kubwa ambalo mtu analifanya dhidi ya nchi yake na mtu anyefanya kosa hili anajulikana kama msaliti, mfano wa watu wasaliti wanaojulikana duniani ni Yuda ambaye kidini alimsaliti Yesu, mwingine ni Benedict Anold huyu jamaa aliisaliti nchi yake ya Marekani dhidi ya Mbritishi, wengine ni Vidkun Quisling, na Marshall Pe’tain.
Kisheria ukubwa wa kosa hupimwa kwa adhabu yake, kosa likiwa kubwa mtuhumiwa hutumikia adhabu kubwa vivyo hivyo kosa likiwa dogo mtuhumiwa huadhibiwa kiasi.


Kwa mujibu wa sheria ya Tanzania, mtu akifanya yafuatayo huhesabiwa kama amefanya kosa la jinai la uhaini hivyo huadhibiwa kulingana na ukubwa wa kosa hilo.

Kifungu cha 39 ( 1 ) cha kanuni za adhabu kinasema kuwa mtu yeyote ambaye yumo ndani ya Jamhuri ya Muungano au popote, kujaribu kumuua Rais, kuanzisha vita dhidi ya Jamhuri ya Muungano, kusababisha, kuwezesha, kuchochea, kushawishi, kushauri kuhusu kifo, kumlemaza, kumzuia, kufungwa kwa Rais. kumwondolea Rais heshima na jina la mkuu wa nchi, amiri jeshi mkuu, au kiongozi wa serikali, kupindua serikiali iliyo madarakani, kutishia serikali, bunge au mahakama kwa makosa haya na yale yaliyotajwa hapo juu mtu wa namna hiyo atakuwa ametenda kosa la jinai ambalo ni kosa la uhaini

Aidha ifahamike kuwa kwa mtu yeyote atakayekutwa na hatia ya kutenda kosa la uhaini adhabu yake ni kifo na sheria hiyo ya kifo imeelezwa katika kifungu cha sheria namba 39 na 40 cha kanuni za adhabu.
Hivyo watanzania kwa umoja wetu tunapaswa kuzijua sheria za nchi yetu ili kuweza kujiepusha kutenda makosa ya jinai dhidi ya nchi yetu.



Iwe kwa faida yako na wengine kama wewe ambao una hisi kila mtu akitenguliwa basi amekataa nafasi hiyo...

Jitahidi kusoma kwa makini kila mstali uweze kupata uelewa...

Wenzio wakina Mbowe, Lema nk walipanda ndege kutoka dar kwenda ktk sherehe mwanza kwa Magufuli, walikuwa wana elewa haya. Wangeweza kusema wana umwa lakini ndio hivyo haikuwezekana
Kwa jinsi Magufuli alivyokuwa nafikiri angetumia hicho kifungu kuwateua wapinzani waliokuwa wanamsumbua
Na kama wangegoma wangetiwa ndani kirahisi tu
 
Mtu unaweza elewa raisi kutofikiria sana kwenye teuzi huko kwenye serikali za mitaa. Asijali sana wateule wanaleta nini mezani so it’s OK watu kama kina ‘mama totoo’, Nikki wa Pili na ghasia wengine kujikuta wameulamba.

Lakini kukosea teuzi sensitive na kuwafuta watu kazi kabla ya ata kuanza ni kielelezo tosha ‘the lady is not serious on the job’ and doesn’t understand most roles serikalini as yet anateua akiambiwa roles za watu anapangua tena huko ni ofisini kwake. Sasa huko kwenye wizara si ndio balaa katujazia vilaza wala aoni shida kisa hayamuhusu.
Kiukweli alimkosea heshima Diwani Athuman! Hivi unajua majukumu ya katibu mkuu wa ikulu (Mnikulu)? Yani atoke kuwa DG akasimamie usafi kweli?
 
Diwani Athman atenguliwa ikulu.

View attachment 2469855

=========

Rais Samia ametengua uteuzi wa Kamishna Diwani Athumani Msuya kuwa katibu Mkuu Ikulu

Aidha, Rais Samia amemteua Bw. Mululi Majula Mahendeka kuwa Katibu Mkuu Ikulu.
Nawaza tu Hata ningekuwa mm Diwani ningeshusha kofia chini maana naujuwa ukweli ambao wengi hawajuwi pale ikulu nitapotea kama alivyopotea Kijazi na siri naijuwa why nisiwe kama akina Mangula? Taifa lina majitu yana akili jamani.
 
Hawa wakuu wa hiki chombo miaka ya karibuni wamelambishwa sana sakafu sababu ya kutosimama kwenye msingi wa kile taasisi imepangiwa kufanya.

Wanafanya kazi kwa upepo wa wanasiasa, Mwisho wa siku zigo la misumari linawadondokea wao.
What he could have done better?
 
That was likely to happen.

Wala haishangazi, Athuman angepaswa kustaafu. Siyo kushushwa cheo kiasi kile ambapo sehemu ya maelekezo atapokea kutoka kwa aliyekuwa Junior kwake.
You haven't noticed trend ya utendaji wa mwenye nchi, he frustrates you kabla hajakumwaga ili ku justify
 
Nawaza tu Hata ningekuwa mm Diwani ningeshusha kofia chini maana naujuwa ukweli ambao wengi hawajuwi pale ikulu nitapotea kama alivyopotea Kijazi na siri naijuwa why nisiwe kama akina Mangula? Taifa lina majitu yana akili jamani.

Huyo kaondolewa baada ya kukataa kuonesha alipo Been Saanane maana kwenye majadiliano Hilo jambo limeongelewa Sana. Wamfukue alipo ili familia imzike kwa heshima.
 
Back
Top Bottom