Diwani Athumani Msuya atenguliwa Ikulu

Diwani Athumani Msuya atenguliwa Ikulu

Itakuwa jamaa kachomoa. Huu ndio uanaume. Huwezi kuwa DGIS kisha ukakubali kwenda kuwa Katibu Ikulu. Kudharirishana na upuuzi tu.
Hawezi kukataa acheni uzushi na uongo jpm alishawahi kumtoa kipilimba tiss akiwa high level akamshushaa na jamaa akaenda kufanyakazi
 
Ajabu Rais bado anaendeleza tabia yake ya kuteua na kutengua baada ya muda mrefu, inaonekana mteuliwa amekataa uteuzi kitu ambacho kinaonesha Rais huteua wasaidizi wake bila kuwasiliana nao kabla, au Rais ndie ameona hana sababu ya kuendelea na Diwani Athumani kama msaidizi wake.

Sababu ya kwanza naamini ndio inaelekea kuwa kubwa zaidi, kwani ni tabia kwetu kuzichukulia hizi teuzi kama kulamba asali, hivyo kwa akili ya kawaida inategemewa mteuliwa lazima akubali nafasi anayopewa, kumbe kwa wengine hali inaweza kuwa tofauti.

Naandika hayo nikiamini kwamba, kama Rais angekuwa na nia ya kumuacha Diwani kwenye uteuzi wake ili asafishe serikali yake, basi asingemteua kabisa, lakini kitendo cha kumteua na kumuacha baada ya muda mfupi, kinaonesha something is not right somewhere...

Inawezekana kabisa Diwani aliona post mpya aliyopewa ni kama ameshushwa cheo, hivyo akaona hana sababu ya kuendelea na hiyo nafasi mpya, dawa ni kumuandikia mamlaka ya uteuzi na kumjulisha juu ya uamuzi wake, akakubaliwa ombi lake.

Samia hana nongwa, au kama ule uteuzi ulikuwa ni kumtega Diwani ili ajikaange kwa mafuta yake mwenyewe, ajiondoe kwenye serikali ya Samia kwa kuona amepewa cheo kidogo, basi hapo Samia atakuwa amezicheza karata zake vizuri sana.
Umeandika manenoooo kibao lakini pumba tupu kwani jpm hajawahi kuteua na kutengua
 
Huko ubalozini unazani ana ripoti mbinguni??

Sio kila anae ondolewa ktk teuzi amemgomea Mh.

Kumgomea ni kosa la uhaini... Uhaini sio kupindua nchi pekee...

Fahamu tafsiri sahihi ya kosa la uhaini na adhabu yake​


Fahamu tafsiri sahihi ya kosa la uhaini na adhabu yake
Uhaini ni kosa la jinai, kwa tafsiri nyepesi ina maana kwamba ni kosa kubwa ambalo mtu analifanya dhidi ya nchi yake na mtu anyefanya kosa hili anajulikana kama msaliti, mfano wa watu wasaliti wanaojulikana duniani ni Yuda ambaye kidini alimsaliti Yesu, mwingine ni Benedict Anold huyu jamaa aliisaliti nchi yake ya Marekani dhidi ya Mbritishi, wengine ni Vidkun Quisling, na Marshall Pe’tain.
Kisheria ukubwa wa kosa hupimwa kwa adhabu yake, kosa likiwa kubwa mtuhumiwa hutumikia adhabu kubwa vivyo hivyo kosa likiwa dogo mtuhumiwa huadhibiwa kiasi.


Kwa mujibu wa sheria ya Tanzania, mtu akifanya yafuatayo huhesabiwa kama amefanya kosa la jinai la uhaini hivyo huadhibiwa kulingana na ukubwa wa kosa hilo.

Kifungu cha 39 ( 1 ) cha kanuni za adhabu kinasema kuwa mtu yeyote ambaye yumo ndani ya Jamhuri ya Muungano au popote, kujaribu kumuua Rais, kuanzisha vita dhidi ya Jamhuri ya Muungano, kusababisha, kuwezesha, kuchochea, kushawishi, kushauri kuhusu kifo, kumlemaza, kumzuia, kufungwa kwa Rais. kumwondolea Rais heshima na jina la mkuu wa nchi, amiri jeshi mkuu, au kiongozi wa serikali, kupindua serikiali iliyo madarakani, kutishia serikali, bunge au mahakama kwa makosa haya na yale yaliyotajwa hapo juu mtu wa namna hiyo atakuwa ametenda kosa la jinai ambalo ni kosa la uhaini

Aidha ifahamike kuwa kwa mtu yeyote atakayekutwa na hatia ya kutenda kosa la uhaini adhabu yake ni kifo na sheria hiyo ya kifo imeelezwa katika kifungu cha sheria namba 39 na 40 cha kanuni za adhabu.
Hivyo watanzania kwa umoja wetu tunapaswa kuzijua sheria za nchi yetu ili kuweza kujiepusha kutenda makosa ya jinai dhidi ya nchi yetu.



Iwe kwa faida yako na wengine kama wewe ambao una hisi kila mtu akitenguliwa basi amekataa nafasi hiyo...

Jitahidi kusoma kwa makini kila mstali uweze kupata uelewa...

Wenzio wakina Mbowe, Lema nk walipanda ndege kutoka dar kwenda ktk sherehe mwanza kwa Magufuli, walikuwa wana elewa haya. Wangeweza kusema wana umwa lakini ndio hivyo haikuwezekana
Wanafurahisha genge tu huyo diwani hata angepelekwa mtendaji kata angeenda
 
Kiukweli kumtoa mtu kwenye position ya DGIS na kumwacha popote nchini is a mistake!. Position stahiki kwa DGIS mtumbuliwa ni kumpeleka ubalozini. Rais nae ni binadamu na sio malaika, hivyo anaruhusiwa kufanya human mistakes. Hili nililizungumza hapa Rais Samia, sio malaika ni binadamu anaweza kukosea. Tusimlaumu, kumshutumu na kumponda kwa makosa ya kukoseshwa. Tumvumilie tumpe muda

Kuhusu hizi appointments nyeti na very strategic tusimwachie mtu mmoja tuu, she is human hivyo sometimes human mistakes caused by human weaknesses zinaweza kutokea ukajikuta unamtumbua mtu mzuri kwa issues ndogo tuu zikingine za ... Should We Demand More Right to Information Kwenye Teuzi za Key Posts? Ziwe Endorsed na Bunge With Security of Tenure? Mawaziri Wasiwe Wabunge?
P
Apson Mwang'onda alikuwa balozi wapi ? au wastaafu wanakaa hawana athari?
 
Ajabu Rais bado anaendeleza tabia yake ya kuteua na kutengua baada ya muda mrefu, inaonekana mteuliwa amekataa uteuzi kitu ambacho kinaonesha Rais huteua wasaidizi wake bila kuwasiliana nao kabla, au Rais ndie ameona hana sababu ya kuendelea na Diwani Athumani kama msaidizi wake.

Sababu ya kwanza naamini ndio inaelekea kuwa kubwa zaidi, kwani ni tabia kwetu kuzichukulia hizi teuzi kama kulamba asali, hivyo kwa akili ya kawaida inategemewa mteuliwa lazima akubali nafasi anayopewa, kumbe kwa wengine hali inaweza kuwa tofauti.

Naandika hayo nikiamini kwamba, kama Rais angekuwa na nia ya kumuacha Diwani kwenye uteuzi wake ili asafishe serikali yake, basi asingemteua kabisa, lakini kitendo cha kumteua na kumuacha baada ya muda mfupi, kinaonesha something is not right somewhere...

Inawezekana kabisa Diwani aliona post mpya aliyopewa ni kama ameshushwa cheo, hivyo akaona hana sababu ya kuendelea na hiyo nafasi mpya, dawa ni kumuandikia mamlaka ya uteuzi na kumjulisha juu ya uamuzi wake, akakubaliwa ombi lake.

Samia hana nongwa, au kama ule uteuzi ulikuwa ni kumtega Diwani ili ajikaange kwa mafuta yake mwenyewe, ajiondoe kwenye serikali ya Samia kwa kuona amepewa cheo kidogo, basi hapo Samia atakuwa amezicheza karata zake vizuri sana.
Ni chanzo gani ninakitafuta mie kinachoeleza kuwa: "Diwani ameukataa uteuzi"lakini nakikosa!

Kila thread inayozungumzia hili, ukiifuatilia unaona ni dhana tu!

Kwanini tuandike habari za mambo yaliyotokea kwa kufikiri tu na si kwa kuthibitisha?
 
Hakuna mtu anayehudumu TISS na ambaye ni Member wa TISS akateuliwa kazi yoyote na Rais akagoma.

Rais atakuwa amestuka kuwa kumuweka Ikulu karibu yake mtu aliyekuwa anaendesha mission za kuonea wapinzani kutaathiri mipango yake ya zile R nne

R nne zipi mkuu? ufafanuzi kidogo?
 
Naona masalia ya Dikteta Magufuli yananyonyolewa na kupukutishwa kwa kwenda mbele.

Pole Diwani kwa kutimuliwa kwa aibu.
Hongera Mama kwa kuupiga mwingi.
 
Apson Mwang'onda alikuwa balozi wapi ? au wastaafu wanakaa hawana athari?
Apson, Kombe, na Rashid wamestaafu at full term!, Kipilimba, na Diwani ni wameondolewa kabla ya full terms. Full terms za constitution officers ni 65 years.
Hawa ni Rais wa JMT, Spika, Jaji Mkuu na Majaji Rufani, CAG, CDF, Gavana wa BOT, Wenyeviti wa NEC, Maadili, Msajili vyama, CS na Staff Officers, Wakuu wa vyombo vya Ulinzi.

Kama wakati wanateuliwa kushika wadhifa huo, watakuwa na umri wa chini ya miaka 50, then full term yao ni two terms za 5 years then wanastaafu kwa mujibu wa katiba.
P.
 
Kumbuka vijana wa jkt walivyogoma waliitwa nani sasa wale kuruta tu wamegoma order
Uhaini ni kosa na sheria inayolizaa imelipa maana yake na ni kitendo gani kinaweza kuhesabiwa kuwa uhaini, acheni maneno ya mtaani.

Nyie ndio wale wale mnamkamata mtu Aishi Hotel anapanga mikakati ya kushinda uchaguzi halafu mnaenda kumshtaki kwa ugaidi.
 
Uhaini ni kosa na sheria inayolizaa imelipa maana yake na ni kitendo gani kinaweza kuhesabiwa kuwa uhaini, acheni maneno ya mtaani.

Nyie ndio wale wale mnamkamata mtu Aishi Hotel anapanga mikakati ya kushinda uchaguzi halafu mnaenda kumshtaki kwa ugaidi.
Mamlaka ndio imeamua iwe hivyo na jicho la mamlaka ni kubwa sana
 
Back
Top Bottom