Diwani Isaya Doita aliyemtuhumu Godbless Lema afukuzwa Uanachama

Diwani Isaya Doita aliyemtuhumu Godbless Lema afukuzwa Uanachama

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Joined
Jul 5, 2012
Posts
13,171
Reaction score
23,996
Diwani wa Kata ya Ngarenaro kwa tiketi ya CHADEMA, Isaya Doita aliyemtuhumu Godbless Lema kuwa hajui kazi na majukumu yake kama kiongozi wa juu wa CHADEMA na pia kama Mbunge amefukuzwa uanachama kwa kosa la kukiuka kanuni na misingi ya uanachama wa chama.

Kufukuzwa Uanachama kunamfanya kupoteza hata Udiwani wa Kata ya Ngarenaro kwa sababu Diwani lazima awe na udhamini kutoka chama cha siasa.

Ikumbukwe kuwa Juzi kupitia vyombo vya habari, Diwani Isaya alimtuhumu vikali Mbunge Godbless Lema kuwa hajitambui na hajui majukumu yake kama Mbunge, Mwenyekiti wa Kanda na Mjumbe wa Kamati Kuu ambapo imesababisha chama kudhoofika na kukimbiwa na baadhi ya Madiwani wa Jiji la Arusha.

Kufukuzwa kwa Diwani Isaya Doita kunafanya awe Diwani wa 14 katika Jiji la Arusha kwa tiketi ya CHADEMA aliyeondoka CHADEMA baada ya Uchaguzi Mkuu 2015.

Ukitaka kusoma na kuangalia video ya tuhuma unaweza kugonga Link hii:

Link > CHADEMA Arusha ‘’kwafuka moshi’’; Godbless Lema aambiwa hajitambui na hajui majukumu yake


Barua ya kumvua uanachama
EPUVdxeXUAA597w


Video ya tuhuma kwa Godbless Lema
 
Upinzani unatakiwa uwe wa kupigania maendeleo ya wananchi na haki zao sio huu upinzani wa kipuuzi wa kugombania madaraka tuu.

Sijaona kauli za kulaani na kudai serikali itokomeze uhalifu kama vile kuongezeka kwa uvunjaji na vibaka kwenye miji kama Arusha na Dar es salaam.
Wapinzani wanazungumzia masuala yao tu ya kisiasa na sio masuala yanayogusa watu wa chini.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Lema ni sehemu muhimu ya mageuzi Tz, kupitia CDM, wapuuzi wachache kwa njaa na tamaa zao acha wapate wanachostahili.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwamba kwa sababu ni sehemu muhimu ya mageuzi basi hana mapungufu na wakiyasema mapungufu lazima wafukuzwe uanachama!

Hiki kweli ni chama cha Demokrasia na Maendeleo!
 
Video ya alichokisema Diwani Isaya Doita.

Nimemsikia, alichosema ni ukweli mtupu na ukweli mchungu ambao kila uchao ninaendelea kuuzungumza hadi October 2020, haya maneno huyu diwani kayasema jana, leo katimuliwa na kikao gani?.

Kuna utaratibu wa mashitaka kwa mujibu wa katiba ya Chadema, umefutwa?. Hii isije kuwa ni kama kutimuliwa kwa Zitto na Shonza, ni kumpiga teke chura.. Wito: CHADEMA Watendeeni Haki Wanachama Wenu Ili Kuwatendea Haki Watanzania 2015!

Huyu jamaa tayari ameisha jitambua, yuko njia kuu.

P
 
Upinzani unatakiwa uwe wa kupigania maendeleo ya wananchi na haki zao sio huu upinzani wa kipuuzi wa kugombania madaraka tuu.

Sijaona kauli za kulaani na kudai serikali itokomeze uhalifu kama vile kuongezeka kwa uvunjaji na vibaka kwenye miji kama Arusha na Dar es salaam.
Wapinzani wanazungumzia masuala yao tu ya kisiasa na sio masuala yanayogusa watu wa chini.


Sent using Jamii Forums mobile app
wewe uko upande upi kati ya serikalini au upinzani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Upinzani unatakiwa uwe wa kupigania maendeleo ya wananchi na haki zao sio huu upinzani wa kipuuzi wa kugombania madaraka tuu.

Sijaona kauli za kulaani na kudai serikali itokomeze uhalifu kama vile kuongezeka kwa uvunjaji na vibaka kwenye miji kama Arusha na Dar es salaam.
Wapinzani wanazungumzia masuala yao tu ya kisiasa na sio masuala yanayogusa watu wa chini.


Sent using Jamii Forums mobile app
Madaraka kwanza halafu baadaye ndio watazungumzia matatizo ya wananchi waliowapa madaraka!

Godbless Lema wa leo ni milionea kama sio bilionea kutokana na biashara ya siasa!

Selfish politics is the order of the day!
 
Madaraka kwanza halafu baadaye ndio watazungumzia matatizo ya wananchi waliowapa madaraka!

Godbless Lema wa leo ni milionea kama sio bilionea kutokana na biashara ya siasa!

Selfish politics is the order of the day!
Maskini hujui hata billionaire ni kitu gani! Pole sana!
 
Nimemsikia, alichosema ni ukweli mtupu na ukweli mchungu ambao kila uchao ninaendelea kuuzungumza hadi October 2020

P
Kwa mwendo huu wa kuambiwa ukweli watafukuzwa wengi!
 
Tatizo letu ndo hilo tu.

Nazani hata JPM anaiga kwenu tabia ya ukimkosoa unakula kwenzi.

Alafu mnaamtafutia jina baya.
Zitto mlimtimua kwa kesi kama hizi yaani chama hakiitaji kukosolewa wala kushauliwa.

Yaani mnakunywa sumu CCM inaanda kaburi dawa anakufa nayo marehemu.


Timua wasaliti bila huruma kudadeki !
 
Back
Top Bottom