AnakwambiaKuna msanii mmoja anitwa Nash Mc(moja ya wasanii ni nao wakubali pia)alikuwa Germany, akapata kuhojiwa na idhaa ya kiswahili DW Bonn-Germany.
Akaulizwa yupi msanii unayekumbali kwamba Unauwezo Tz,akamtaja Baba Malcolm/ Unju bin unuq.
Unju ana-uwezo mzuri sana.
"Usisubiri Mpaka nife ndio unisifu,
Uandike wasifu nizikwe nisahaulike zipite siku"-Usisubiri
Kuna wimbo wake mmoja alichana kama Snoop doggy basi ilikuwa ni full shangwe,alinifurahisha sana.
Huwa na nyimbo zake zaiidi ya 120,Halafu jamaa ana swagger kupitiliza, zile za 2Pac za "and I can make you famous".
VERSE 1
Naitwa kaka meneja mzee wa fitina tangu kale
Mr. Middle Man, boss staff wallet, Babu Talent
Natoka Manzese, Tip Top connection
Huku hatupendi ugumu labda Hip Hop commercial
Madii alikuwa ana rap, nikamwambia hiyo haiuzi
Siku hizi anaimba video anashutia South
Anabang sana Clouds,ngoma kali zinapigwa
Huku Daudi wa kota akiongoza wakali wa media
Nimekuwa mdananda kwenye game before
Enzi hizo brother ndo, anamtoa MB Dog
Na Z Anton,the realer killer,same thing yo
Japo wengi wameflow, from the fame to being broke
Msinilaumu, mlipata pesa mkacheza
KamaTunda Man sijui hata wapi alipowekeza
Nna pesa, nna magari mijengo biashara kubwa
Siwezi bishana na Baghdad wala afande mla msuba
Chorus
BABU TALENT X 4
VERSE 2
Napiga tu mabao, kila mpira wavuni
Nna connection kibao, kwenye kila kampuni
Ukiniletea hasira za Q-Chilla na uhuni
Nakuacha bila bila kapuni mila kanuni
Nikopia kwenye academy, za kuandaa tuzo
Hip Hop nilimpa Neilly (?) hali hazijuinguzo
Aliondoka kwa pozi akarudikwa chozi Dogo Janja
Singeli inabamba sikui hizi uswazi shorwe mwamba
Na Man Fongo, nataka niwachukue
Niwafanyie promomajina yao yakue
Watokezee EATV Cheche za Duwe
Ndoto nifufue, milango ya fursa niifungue
Kifupi nimshika kila media
Muziki ni biashara huwezi bisha bila tija
Nilimpenda Nikki Mbishi kwenye Play Boy Too
Sio nifanye tena playboy, iwe Playboy two?
Chorus
BABU TALENT X 4
VERSE 3
Niko na mwanagu gaidi sela
Allthe way from Temeke tunafaidi hela
Tunataka Yamoto Band wageuke barafu
Chege na Temba TMK, mbombo ni ngafu
Mitaa haiwatakijapo wapo kwa safu
Kichaa hawanipati nipo dampo pachafu
Bundle na surf tu, halafu followers wa kutosha
Nikiwa na Dangote shobo nasi za kutosha
Siunajua tena chama la Wasafi
Hip Hop sio jifanyeni wanaharakati
Harmonize kaja jana na leo anakaa Masaki
Anavaa mashati,siku hizi hafanani kukaa Masasi
Siko talented, ila ndo Babu Talent
Dotto alinibatiza tena mbele za Daz Nalez (?)
Na Mo Technics,Pesa ya Madafuu
Mida inakwenda bro, we soma saa tu
BABU TALENT X 4
Safi sana,Mimi si nawasikiliza tu.
Sisi ndio foundation wao walitusikiliza sisi kabla hawajawa hapa.
I was there when it all started, with Kwanza Unit, Hard Blasters, GWM,O Juice etc.
Back in the early nineties.
Hahaha.Anakwambia
"Harmonize kaja jana na leo anakaa Masaki
Anavaa mashati, siku hizi hafanani kukaa Masasi"
Hahaaaaaa.
Nimecheka saaana hapo.
Huyu jamaa BASATA wangekuwa wanamuelewa angefungiwa hahaa.Hahaha.
Unju anavituko sana,kucheza na maneno na kufanya yalete maana na furaha si kazi ndogo kabisa.
Kuna ngoma moja alikuwa akimdiss Ney wa mitego hiyo ndio inavituko balaa...
Moja ya mashairi yake.
"Kanga moko ndembe-ndembe laki sipesa/
Kila akikatiza mamende wanabaki na presha/
Ahaa Jamani ney ama kweli maanani hakosei/
Massita du mitaani hawaongei/"
Katoboa kitovu katoboa ulimi vikuku miguu yote kope utadhani jini/
Anataka atoke na mimi naogopa tope lakini/
Hizi nyimbo wakati mwingine zipo vizuri zinafikirishi na kuburudisha.
Hahaha.
Unju anavituko sana,kucheza na maneno na kufanya yalete maana na furaha si kazi ndogo kabisa.
Kuna ngoma moja alikuwa akimdiss Ney wa mitego hiyo ndio inavituko balaa...
Moja ya mashairi yake.
"Kanga moko ndembe-ndembe laki sipesa/
Kila akikatiza mamende wanabaki na presha/
Ahaa Jamani ney ama kweli maanani hakosei/
Massita du mitaani hawaongei/"
Katoboa kitovu katoboa ulimi vikuku miguu yote kope utadhani jini/
Anataka atoke na mimi naogopa tope lakini/
Hizi nyimbo wakati mwingine zipo vizuri zinafikirishi na kuburudisha.
Labda BASATA vichwa vyao ni vizito sana.Huyu jamaa BASATA wangekuwa wanamuelewa angefungiwa hahaa.
Bora kawazidi misamiati na flow.
Hahaha,Kwakweli Ubongo wako kama ni mzito, jamaa anakuacha mweupe ka'mkorogo."Kama unatafuta kiki, vuta kiti
Waza "Mbona nna sura mbaya, halafu kufa sifi?""
Jamaa anaweza kuwaharibia watu afya zao za akili.
"Kanisa utachomwa moto nakuapia"ni hisia zako tu mkuu zilizokusukuma kufuta nyimbo za fid q nakuhusu kuwa rapper mahili pia bado anasafar ndefu kidogo aisee.....
ila dizasta vina kwenye wimbo wa kanisa ameongea vitu muhimu kule
Kamanda wangu,Bora hata ungetafuta mtu mwingune.
Si kumlinganisha na Mwanamalundi.
Au unafanya tathmini uone ni jinsi gani Fid Q anakubalika kwenye ulimwengu wa HipHop.
Yaani Sangara unamlinganisha na kidagaa!
Ahsante..Heshima kwake disazta vina.Siwafichi mpaka sasa Dizasta vina anaweza kuwa best real rapper Tanzania....take time umsikilize...Huyu jamaa kanifanya nifute nyimbo zote za wasanii kama kina Fid Q kwenye playlist yangu.
1.anaimba uhalisia hasa vitu ambavyo watu wengi wanaogopa kuvizungumziaAhsante..Heshima kwake disazta vina.
Kwa mtazamo wako na maoni yako vitu gani unaviona au mambo gani au uwezo gani unaouona mpaka kutaka kuhitimisha yakwamba dizasta vina anawaacha mbali wasanii wenzeka..?
Unaweza kuoredhesha vitu vinavyomtengenisha na wasanii wenzake, sio mbaya ukifanya hivyo.
Kuna mtu anaitwa chuma mbeya boy, ni shida....
Dizasta, Ghetto Ambassador, One The Incredible, Baba Malcolm, Algebra
Hawa wapo kwenye replay kwa sasa.
Anajua kucheza na lugha, halafu mara atokee msela kupitiliza, mara katokea meneja anawaeleza wenzake jinsi ya kufanya biashara ya muziki, mara katokea kawageuka wahuni anawaponda wanavuta sana, yani mda wowote anaweza kubadilika tu halafu yupo on key.Nikisilizaga pini za Baba Malcom, huwa naenjoy sana swahili rap. The guy is really talented.
-Kaveli-