FortJeasus
JF-Expert Member
- Jan 19, 2012
- 604
- 402
Na kwa lipi haupo upande wa jiwe?Kwa hili,mimi nipo upande wa serikali.
Sasa ukiona mtu kama Sarungi na Fatuma Karume wanavyojishaua na wengine kule twitter huwa nashangaa sana!Kuna mambo ambayo lazima kama jamii yenye upekee wake tuyasimamie hata kwamba tunatofautiana kiitikadi.
Moja ya jambo hili ni mimba kwa wanafunzi. Siafiki mwanafunzi apate Ujauzito kurudi katika mfumo rasmi wa elimu kama wenzake ambao hawajapata.
Hapa tutahalalisha umama, baba na hata ushemeji katika shule/darasa na ile dhana ya uanafunzi kufa kifo cha kawaida.
Kila kitu kinautaratibu wake. Tutambue pia kuwa shule ni ni chombo ambacho jamii inawatengeneza wanajamii wa baadae katika kuiendeleza jamii husika kwa siku za usoni. Na kwamba, ni unapokuwa shuleni basi uzingatie ile miiko ambayo jamii imeona haipaswi kuvunja na watoto wake ndio maana wakapelekwa shule.
Sasa kama huyu aliyepelekwa shule ameona hawezi kufata misingi hiyo ya jamii ya nini kumuendeleza katika jambo ambalo hakulizingatia?
Shule zibaki kuwa shule na taratibu, sheria, utamaduni na majuzi zake zisimamiwe. Ikiwa ikatokea mwanafunzi akapata Ujauzito basi, apelekwe katika mfumo mbadala usio rasmi na ule aliokengeuka ili shule na malengo ya shule katika jamii yabaki kama ambavyo jamii inapenda iwe.
Sio kila atakalo mfadhili ni jambo jema ktk mfadhiliwa.
Duh......!Hao wote wanasimamia misimamo ya maboss zao, suala la hizo pesa ni la kimkataba na sio zawadi Tz tumekubali masharti you tuliyopewa na WB kuhusiana na wanafunzi wenye mimba kurudi kusoma ktk mfumo rasmi au usio rasmi, kinachosema kwenye mkataba ndicho kitafuatwa na sio maneno ya Hawa wanaosifu mabwana zao bila kuangalia uhalisia was mkataba.
Akalee mtoto... Mtoto akikua naye atakua amekua.. Atachagua mfumo atao ona unafaa akajiendeleze. Ipo mingi...mkuu, una binti nyumbani kwako ?
alafu mbona hata hawa wanaosoma mfumo rasmi wanabeba sana mimba na wanazitoa, kuna jamaa yangu tulipokuwa high school demu wake alitoa mimba 3
hili swala mnabidi mtoe maamuzi like parents,
Sent using Jamii Forums mobile app
Naona umekuwa muumini wa pascal mayalla😂, anyway mzee mgaya anasemaje kuhusu hili? Afu ana kadi namba ngapi chamani kwetu??Duh......!
Yapo mengi;kwa mfano kuminya
Hapa tunamzungumzia Abbas na Nondo!Naona umekuwa muumini wa pascal mayalla😂, anyway mzee mgaya anasemaje kuhusu hili? Afu ana kadi namba ngapi chamani kwetu??
Je watoto wakiume wanaowabebesha mimba wafanyweje?
Dr Abbas ambaye ni msemaji mkuu wa serikali anasema wanafunzi wanaopata mimba shuleni hawatarudi kuendelea na masomo katika mfumo rasmi bali wataruhusiwa kupitia mfumo usio rasmi yaani private candidates.
Abdul Nondo boss wa vijana pale ACT wazalendo anapinga vikali yeye anataka wanafunzi hawa baada ya kujifungua warudi katika mfumo rasmi wa masome ili wawe na sifa ya kukopesheka na Bodi ya mikopo watakapochaguliwa kujiunga na vyuo vya elimu ya juu.
Mjadala ni mkali kweli kweli ndani ya kipindi cha Tuongee asubuhi. Star tv.
Nani yuko sahihi?
Maendeleo hayana vyama!
Kweli kabisa maana dogo kapwaya sana, alikuwa anaongea kama amekaririshwa maneno na ZZK. Alikua anag'ag'ana tu ubaguzi ubaguzi. Haangalii hata hoja ya msingi kama mwanafunzi anatakiwa asome katika mazingira ya saikolojia nzuri,sio mazingira yanayompa fikra kuwa ngono na mimba ni jambo la kawaida.Kiitifaki, huyo bwana mdogo alitakiwa akutanishwe na Mwenyekiti wa UVCCM; Katibu Mkuu ni nafasi kubwa katika Utumishi wa Umma. Waandaji wa kipindi hawajatenda haki kwa Katibu Mkuu.
Katika mjadala huu, baadhi ya wanaharakati, asasi za kiraia na wapinzani wanakusudia kuhujumu elimu yetu na taifa kwa ujumla kwa kushirikiana na Benki ya Dunia.
Katika hili, msimamo wa serikali uungwe mkono.
Hujapita kwake akakupa msimamo wake ktk hili?, Hao unawaojadili hapa hawana maamzi juu ya hizo pesa. Kinachoamua ni Nini mkataba unamtaka afanye nini mkopaji.Hapa tunamzungumzia Abbas na Nondo!
Hizo nafasi tu, hata Waitara ni N/waziri lakini huwezi mweka meza Mona na Nondo kihoja.Kweli kabisa maana dogo kapwaya sana, alikuwa anaongea kama amekaririshwa maneno na ZZK. Alikua anag'ag'ana tu ubaguzi ubaguzi. Haangalii hata hoja ya msingi kama mwanafunzi anatakiwa asome katika mazingira ya saikolojia nzuri,sio mazingira yanayompa fikra kuwa ngono na mimba ni jambo la kawaida.
Ujinga Upo kwa mtoto wa kike ana miaka 15 anashndwaje kujua namna ya kuzuia mimba,mbona style za kugegedana wanazjuaJe watoto wakiume wanaowabebesha mimba wafanyweje?
Wewe ni mojawao?Umefahamuje ni makusudi wanafanya?Huwa wanabebeshwa mimba kama ndoo ya Maji?Hukumu ya wanaowapa ujauzito nayo iwe kuhasiwa,maana hiyo ndiyo angalau italingana na hukumu Kali ya kifungo cha ujinga kwa maisha yao yote.Watoto wa kike hawatakiw kusamehewa hata kidogo wanafanya makusudi
johnthebaptist, Huyu Nondo ni mweupe kichwani, kwanza aliwahi kuona bodi ya mikopo inabagua kutoa mikopo kwa kigezo hicho, kimsingi bodi ya mikopo inakooesha Mtanzania yeyote vigezo vidogo ni kwa sababu ya kiwango kidogo cha pesa iliyopo.
Kingine anaposema warudi shule baada ya kujifungua pia afikirie hao si watoto pekee ata hao waliozaliwa na hao wazaziwatoto ni watoto na wanahizaji matunzo nani atawajibika nao?
Mimba nyingi za utotoni ni maisha duni na ukosefu wa elimu ya uzazi kwa watoto wetu, watoto wanaozaa mara nyingi huingia katika majukumu ya kuwalea watoto wao sasa hayo majukumu watayawezea wapi?
Huyu Nondo atakuwa kashikwa na kutu hafikirii ubishi wa watu wa kigoma poor him.
Sent using Jamii Forums mobile app