Dkt. Abbas na Abdul Nondo watofautiana namna watoto wa kike wanaopata mimba shuleni watakavyoendelea na masomo

Akalee mtoto... Mtoto akikua naye atakua amekua.. Atachagua mfumo atao ona unafaa akajiendeleze. Ipo mingi...

ukiwemo mfumo huu rasmi wa elimu, kama binti amepata mimba akiwa kidato cha 5, akajifungue na arudi shule badae aendelee alipoishia


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wote wako sahihi kulingana na mtazamo na malengo ya mitazamo yao. Wapo wanaowafikiria wanyonge, wakipata mimba wataingiaje private schools? wataendeleaje Vyuo vya elimu ya juu. Wapo Wanafiki wasiojali wengine wanaishije, wanakula nini wajisifiao kutetea wanyonge. Hawa wanakariri maandiko 'kila mtu ataubeba mzigo wake mwenyewe, kila mbuzi atakula kulingana na urefu wa kamba yake'. Tuombe mungu atupe busara yasitutokee yaliyowatokea wenzetu pale maskini walipozidi kuwa maskini na matajiri walipozidi kuwa matajiri halafu wakaanza kunyang'anyana.>vita
 
Ulichosema ni sahihi na ndio ulivyokuwa msimamp Wa serikali. Tatizo ni shinikizo la wafadhili. Nadhani umeshaona humu makubaliani ya kupatiwa mkopo Wa eliimu takriban trilioni moja. Moja ya masharti ni watoto Wa kike kuendelea na masomo kwrnye mfumo rasmi baada ya kujifungua. Naomba serikali itafasiri upya maana ya mfumo rssmi. Iwe kwamba kila anayefanya mtihani wa necta ahesabiwe kuwa katika mfumo rasmi. Hao wanafunzi wamama wafanyemtihani wa necta kama private candidate! Hapo hatutakuwa tumekiuka masharti ya mkopo wa wazungu.
 
Hana maana hiyo,akili zenu huwa zinakwama wapi?Anazungumzia kama mtoto kapewa mimba na mtoto mwenzake!Je,huyo mtoto wa kiume naye anafukuzwa aende mfumo usio rasmi?

Hakuna mtoto anampa mimba mtoto mwenzake, tumia akili sawa, mimba inawekwa na mtu aliekomaa kutoa mimba, awe na umli mdogo hata kama anasoma ataenda jela tu, au hilo nalo hujui?
 
WHERE COMMON SENSE STOPS TO BE COMMON
 
Waruhusiwe kupata Elimu, haijalishi mfumo, upo, na mfumo wa Elimu kisiwe kigezo Cha mtu kupata Mkopo chuo kikuu. Mifumo yote imewekwa kwa mujibu wa Sheria. Sasa kwanini Sheria ianze kubagua. Waliobebeshwa mimba watajiunga mfumo wa Elimu ya watu wazima, pamoja na aliyembebesha. Hapa tusibague, maana wote Ni wakosaji hapa, na wote Ni wazazi. Akitajwa ahusishwe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndugu yangu hawatakuelewa hata kidogo. Wao na JPM wao! Wangekuwa wanaunga mkono maagizo ya Mungu hivyo hii nchi ingekuwa ya walokole! Tangu tupate uhuru hizo mimba zipo. Waathirika wapo wengine ni wakurugenzi katika mashirika ya umma na kampuni binafsi. Hilo hushughulikiwa kwa busara. Wote wanaopata ujauzito kwa sababu tofauti tofauti, mimba huwafukuza shule! Haiwekani kuhudhuria masomo na mimba. Hilo haliingii akilini. Wengi wao baada ya kujifungua hurudi shule. Hapa ndipo hutumika busara. Mhusika ataendelea na shule wapi na kivipi halikuwa tatizo.
Ile tu kusema sitasomesha mzazi ina maana walikuwa wanasoma! Huyo anayekataa alikuwa mbunge na kwenye baraza la mawaziri miaka 20. Miaka yote hiyo asijifunze hekima iliyokuwa inatumika! Tatizo la nchi za vita ya wenyewe kwa wenyewe huwa ni hilo la kukosa maarifa. Kila mmoja anasema yeye 'mwanaume bwana' Hapo ni risasi au panga tu! Huyu ukimkalisha chini ukamuuliza tatizo kwani liko wapi? Jibu utalopata: kwenye utawala wangu sahau kitu kama hicho. Nimeishasema. Mimi sio wachezomchezo. Kama hunifahamu uliza!
 
Hawa watoto hii sheria ya miaka 30 jela ndiyo wameamua kuifanya ngao ya kuendelea kufanya ushenzi wao, wanajua hawaguswi wakikutwa ni balaa kwa mwanaume tu. Hawa feminist waliyoipigia debe ipite, walifikiria kutetea jinsia yao na si kuzuia tatizo. Wanatongoza badala ya kutongozwa

Hizi mimba ndiyo zinazidi na ukisema umrudishe alozaa, ndiyo ataenda shawishi wengine nao waendeleze huo mchezo. Mwishowe darasa litakuwa na wazazi watupu, watoto wanamaliza shule ni wazazi.

Kuwakataza wasirudi, inawapa somo wengine kuwa hiko kitu siyo na wakiepuke. Ila kuruhusu warudi kutaongeza mfumuko wa mimba, maana ile sheria ndiyo imewapa go ahead ya kufanya ujinga wao.
 
Ndugu sidhani kama katika hili kuna U CCM na Upinzani, ni swala la Cultural and values za jamii yetu.

Hili sio swala la Mh. Rais wala CCM, ni swala sheria za nchi toka awali.

Kama umepita pita kwenye sekta ya elimu unaweza ukawa na mtizamo tofauti na hisia zako.

Sheria za shule, miongozo inayotolewa kuhusu mimba mashuleni ikiwa ni pamoja kitabu cha Kiongozi cha Mkuu wa Shule na Vyuo (1997) kilichotolewa na Wizara ya Elimu na Utamaduni zinasema wazi wazi makosa yanayoweza kumfukuzisha shule mwanafunzi ni pamoja KUMPA MTU MIMBA au Kupata Mimba wala si swala lililoasisiwa na JPM wala CCM ni swala la sheria za nchi.


Kama kutakuwa na mapungufu basi ni swala la wizara husika kurekebisha na si kumbebesha mtu au chama flani.

Umeuliza kama "tumepima madhara kama akirejea darasani ikishakaa na ananyonyesha" kutakuwa na madhara gani. Ni vema ukatambua kwamba sheria zinapotungwa zinakuwa zimezingagia si tu Falsafa inayoongoza nchi katika eneo hilo Bali pia huwa utafiti wa kina umefanyika. Je unaweza kumuadhibu mama mwenye kichanga cha miezi mitatu pale anapokosea kama ukiwa mwalimu?...he unajua atapata utulivu upi darasani wa kuzingatia masomo akiamua mume wake, mtoto na cha kumnyonyesha mwanae?...sasa kwa nini tusiwaruhusu wazee na wabibi waliokosa elimu kusoma katika madarasa ya kawaida na bint yako ambaye hajavunja ungo darasa moja?....he unajua umuhimu wa Peter peer grps katika kusoma?

Namba tatu unauliza vipi kwa mwanafunzi mwenzake aliyempa mimba? ...he unajua juvenile court unakazi gani?

Kifupi huna hoja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…