Dkt. Abbas na Abdul Nondo watofautiana namna watoto wa kike wanaopata mimba shuleni watakavyoendelea na masomo

Hujataka tu kuzitambua hoja zangu!
1.Rejea ilani ya CCM 2015,Pia rejea hotuba ya Mama Samia suluhu akiwa huki kaskazini akizungumza jukwaani kuwa serikali itawapa fursa watoto watakaozaa kurudi shuleni na baada ya kauli hiyo ndipo JPM akatoka hadharani na kusema kwenye serikali yake hatasomesha mtoti atakaye zaa!So hiyo ni yake!
2.Unazungumzia Juvenile court lakini hapo ni ni kwa criminal case!Mtoto wa miaka 15 kumpa mimba mtoto wa miaka 15 unasema wa kiume anapelekwa juvenile court na wa kike anafukuzwa shule,hapa huna hoja maana hakuna criminal case hapo!Hakuna kosa la kumpa mtu mimba bali kuna makosa kama kumbaka mtu!Sasa watoto wamekubaliana,wakafanya ngono na mmoja akapata ujauzito,hapo hakuba ubakaji!Ubaki unatoke kwa namna hizi tu
-Mtu mzima kufanya mapenzi na mtoto!
-Kufanya mapenzi na mtu bila ridhaa yake!
So kwenye pointi hiyo huna hoja!

3.Eti tukiruhusu watoto waliojifungua unasema basi vikongwe warudi kusoma na watoto maana ni kitu hicho hicho!
Hivi mtoto akipewa mimba ndio umri unaongezeka na anakuwa mtu mzima?Mtoto akibakwa na ikapelekea kupata mimba akijifungua akiwa na miaka 12,baadaye na mimi mtu mwenye miaka 30 nikamtongoza binti huyo akiwa na miaka 13,nikafanya naye ngono,nakuwa sijambaka kwa scenario yako ya kujifungua tayari ni mtu mzima??Mbona sheria inamtambua mtoto kwa umri na sio kama amezaa au la?
4.Huko nyuma mabinti ambao walikuwa wakijifungua,kama wazazi wanauwezo walikuwa wanafanya mpango na akijifungua anaenda kusoma shule nyingine,na wengi tumewaona wanaweza kuwa mashuhuda!
5.Hoja ya kwamba itakuwa ngumu kumuadhibu nayo ni mfu!Anaweza kuadhibiwa vizuri tu kutokana na kosa alilotenda lakini kuna mazingira akasamehewa bila wenzake kujua!Mfano hakumaliza honework,unaweza kumwita ofisini na kumwuliza kwanini, labda akakueleza kuwa mtoto alikuwa anaumwa basi unamwelewa kutokana na mzigo alionao!Kuna watoto wengi tu wenye matatizo mbalimbali na wanapewa excuse kwenye baadhi ya mambo,sio lazima wenzake wajue!Nayasema haya kwasababu nimeona baadhi ya cases!
6.Nimekupa mfano wa Kenya na Uganda,tungeenda kujifunza huko pengine tungepata kitu!
Tamaduni hubadilika kulingana na wakati!Mfano kwenye makabila mbalimbali mtoto wa kike alikuwa hapaswi kwenda shule,kwingine ilikuwa wanakeketwa wasiwe malaya,kwingine hawakuruhusiwa kula baadhi ya vyakula NK!Mambo yamebadilika sana,hatupaswi kuwa sehemu ya kutengeneza wajinga bali kuwakomboa!Huko katika mfumo usio rasmi ni kwa kupunguzia ujinga tu,ni dumping area!

Narudia,sijaona sababu yoyote significant ya kumzuia mtoto wa kike kurudi shule kama ikitokea akajifungua!
 
Kabisa mkuu,umeandika jambo kubwa sana ila hawa watu hawawezi kufungua akili zao!Kipindi cha nyuma walikuwa wanaondolewa shuleni kutokana na hali zao za Mimba,ila baadaye walirejea na mambo yalienda vizuri tu!Hakukuwa na mgogoro wowote,nini kimemkumba JPM mpaka kuliibua hili?Taifa hili si familia,unaweza kukuta kwenye familia mtu ndio msimamo wake huo,mtoto anapewa nafasi moja tu,akiharibu ndio basi!Sasa mambo kama hayo kuyaleta kwenye kutawala nchi inakuwa tatizo!
 
Haya ni mawazo yako and as long as you have an identity huwezi kusema ukweli wako. Ukisema kinyume, UNAO!
 
.Eti tukiruhusu watoto waliojifungua unasema basi vikongwe warudi kusoma na watoto maana ni kitu hicho hicho!
Hivi mtoto akipewa mimba ndio umri unaongezeka na anakuwa mtu mzima?
takataka zingine usibishane nazo
 
Hakuna mtoto anampa mimba mtoto mwenzake, tumia akili sawa, mimba inawekwa na mtu aliekomaa kutoa mimba, awe na umli mdogo hata kama anasoma ataenda jela tu, au hilo nalo hujui?
Kijana wa kiume mwenye miaka 15 kampa mimba mtoto wa kike mwenye miaka 15!Inamaana wa kike anakuwa mtoto na wa kiume anakuwa mtu mzima?
Akili yako hujaitumia vizuri,hakuna kosa la kumpa mtu mimba bali kuna kosa la kubaka!Mimba ni matokeo tu!
Sasa nenda kwenye sheria ya ubakaji ukajifunze ili mtu awe amebakwa inatakiwa kuwe na mazingira gani!Kwa kukusaidia ni hivi
1.Mtu mzima kufanya ngono na mtoto(haijalishi kama wamekubaliana au lah)
2.Kufanya mapenzi na mtu bila ridhaa yake!

Sasa hapo,watoto wawili wenye miaka 15 wamekubaliana kufanya ngono,utasema nani kamlaghai mwenzake?Wote hawajakomaa kiakili!
Usiwe unakurupuka!
 
Hapo ndio kumaanisha wametofautiana? Au msimamo wa serikali upo palepale? Maana Abdul Nondo anataka warudi shuleni baada ya kujifungua kama nani?
Inashangaza....
Abdul Nondo πŸ˜€ πŸ˜€ ni nani mpaka anachosema kwa jazba kikubalike na msemaji wa serikali??
Anajifananisha na mtoto wa baba, Naibu Raisi...

Everyday is Saturday.....................😎
 
Hili tatizo ni gumu kuisha kwa kumuazibu mwanaume aliefanya hvyo njia pekee ni kuwapatia dawa za uzazi wa mpango wasichana wa shule
 
Je watoto wakiume wanaowabebesha mimba wafanyweje?
Sheria ile ile inayotumika kwa mtoto wa kike ndio inayotumika kwa mtoto wa kiume iwapo itathibitika ndiye aliyempa ujauzito mtoto wa kike. Tatizo mara nyingi linakuja kwenye "kuthibitisha".
 
hili la kurudisha wazazi darasani kwakweli hapana!
 
Hili tatizo ni gumu kuisha kwa kumuazibu mwanaume aliefanya hvyo njia pekee ni kuwapatia dawa za uzazi wa mpango wasichana wa shule
Dawa zinaweza kuwa one of the solutions,je kuna utafiti wa kisayansi kuonyesha sababu za mimba za utotoni?Huwezi kutatua tatizo bila kufahamu asili yake.
Hatua Kali kwa watoto wa kike kuachishwa masomo katika mfumo rasmi na kutokuwa na uhakika wa kupatiwa hata hiyo isiyo ya mfumo rasmi siyo sawa.Ni uvunjifu wa haki ya msichana/mwanafunzi/mtoto kupata ulinzi,elimu,afya bora na uhakika wa maisha yao.Tena wakati huo huo lazima kama Taifa tuweke utaratibu bora wa malezi watoto wanaozaliwa na wasichana/watoto/wanafunzi maana hawa ni innocent Tanzanians. Tusikubali kuwa sehemu ya ukatili dhidi ya watoto kwa kutokufahamu/kukusudia.
 
Hili tatizo ni gumu kuisha kwa kumuazibu mwanaume aliefanya hvyo njia pekee ni kuwapatia dawa za uzazi wa mpango wasichana wa shule
Dawa zinaweza kuwa one of the solutions,je kuna utafiti wa kisayansi kuonyesha sababu za mimba za utotoni?Huwezi kutatua tatizo bila kufahamu asili yake.
Hatua Kali kwa watoto wa kike kuachishwa masomo katika mfumo rasmi na kutokuwa na uhakika wa kupatiwa hata hiyo isiyo ya mfumo rasmi siyo sawa.Ni uvunjifu wa haki ya msichana/mwanafunzi/mtoto kupata ulinzi,elimu,afya bora na uhakika wa maisha yao.Tena wakati huo huo lazima kama Taifa tuweke utaratibu bora wa malezi watoto wanaozaliwa na wasichana/watoto/wanafunzi maana hawa ni innocent Tanzanians. Tusikubali kuwa sehemu ya ukatili dhidi ya watoto kwa kutokufahamu/kukusudia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…