Dkt. Bashiru awashangaa wapenda ‘Kazi na Bata’. Asema kauli hiyo inachangia kuzorotesha Uchumi

Dkt. Bashiru awashangaa wapenda ‘Kazi na Bata’. Asema kauli hiyo inachangia kuzorotesha Uchumi

Katibu Mkuu CCM Dr.Bashiru Ally amewaomba Wananchi kupuuza sera na kauli zinazotolewa na baadhi ya Viongozi wa Kisiasa Tanzania zikitaka wale bata (starehe) badala ya kazi na kusema jambo hilo lisipokemewa litasababisha Taifa kuwa legelege, tegemezi na kula bata badala ya kazi.
_
“Katika Nchi ambayo Wananchi wanapambana kujikomboa kiuchumi, hasa ktk nchi zetu za Afrika ambazo bado tupo nyuma kimaendeleo ya Mtu mmojammoja na Taifa kwa ujumla, kutokea Kiongozi na kuwaambia watu wafanye kazi kwa starehe ni usaliti mkubwa wa mapambano ya kiuchumi”-Dr.Bashiru
_
“Unaposema kazi na bata, ni kudhalilisha Wanawake na Mama zetu ambao wakati wote wamekuwa wakifanya kazi kusomesha Watoto, wakifanya kazi kulisha familia zao, kuwambia wale bata,ni sawa na kuwataka washinde kwenye starehe huku watoto wakidhalilika kwa kutokwenda shule”-Dr.Bashiru
Dakitare kilaza.. hahaha...

Kazi tunafanya, na bata tunakula..
Kazi na dawa,
Kazi na bata..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bashiru ndiye anakula bata kwa kufanya kazi nyepesi kupita kiasi. Mtu anatoka Dar anaenda songea na kuishia kufungua shina la wakereketwa alafu analala na vidosho hoteli ya kifahari kwa kisingizio cha kuimarisha chama, labda hajui maana ya kula bata, hama alimaanisha kula bata mzinga hau bata maji hau huyu wa kienyeji.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mumuelewe aliyetoa huu msemo au kauli mbiu. Anasema watu wafanye kazi halafu wale bata - yaani wapumzike na kustarehe.
Wenzetu wazungu wamefika hapo kwa sababu ya kufanya hivyo - wanafanyakazi kwa biddi na ikifika kipindi cha holiday wanasafiri mbali kwenda kula bata - kukusanya nguvu na wakirudi wanakuwa wamepata nguvu mpya ya kimwili na kiakili. Huwezi kuwaambia watu wale bata wakati huwaambii kufanya kazi kwa sababu huwagawii fedha za kulia bata na wao wanajua kula bata ni kutoka mfukoni mwao. Mapumziko na kustarehe ni sehemu ya muhimu sana kwenye maisha ya binadamu kwani huchangia ubunifu na ari ya kazi na ndio maana makampuni makubwa ya kimataifa hutoa fedha kwa wafanyakzazi wao kwa ajili ya kwenda kutembelea nchi mbal mbali - ikiwemo kutalii. Tusione kila kitu ni siasa tu nafikiri mtoa hoja ameona kana kwamba hii slogan inapingana na Hapa Kazi Tu akasahau kufikirisha akili yake juu ya umuhimu wa kustarehe baada ya kazi na mchango wake katika productivity na ubunifu.

Wanataaluma wetu wanapopewa vyeo vya kisiasa ndipo wanatuonyesha uhalisia wao. Mi nilikuwa najiuliza miaka karibia sitini tangu tupate Uhuru bado tunaitwa dunia ya tatu. Lakini kwa ujio wa social media nimeelewa chanzo ni nini!
 
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Dkt. Bashiru Ally, amewataka wananchi kupuuza kauli ya kufanya kazi na kula Bata ambayo imeratibiwa na Mbunge wa Kighoma Mjini Zitto Kabwe na kusema kauli hiyo itachangia kuzorotesha uchumi wa Taifa.

Dkt. Bashiru amesema kuwa, katika nchi ambayo wananchi wanapambana kujikomboa kiuchumi, hasa katika nchi zetu za Afrika ambazo bado tupo nyuma kimaendeleo ya mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla, kutokea kiongozi mmoja kuwaambia watu wafanye kazi kwa starehe ni usaliti mkubwa wa mapambano ya kiuchumi.

“nchi hii ambayo tunaongoza mapambano ya kujikomboa kiuchumi, inamuhitaji kila mtu kwa nafasi yake kuhimiza kufanya kazi kwa bidii, na huku CCM kuna kauli mbalimbali za kuhimiza kazi zikiwemo, Hapa Kazi tu, Kazi na Maendeleo, Uhuru na Kazi na Kazi ni Utu, ila kuna baadhi ya Vyama wao wanahubiri kazi na starehe, na huo ndiyo utofauti wa Chama kiongozi na Vyama vya uchaguzi.’’ Dkt. Bashiru

"Unaposema kazi na bata, maana yake ni kudharirisha wanawake na mama zetu ambao wakati wote wamekuwa wakifanya kazi kusomesha watoto wao, wakifanya kazi kulisha familia zao, na sote hapa ni matokeo ya juhudi kubwa za mama zetu, ambao kuwambia wale bata, ni sawa na kuwataka washinde kwenye starehe huku watoto wakidhalilika kwa kutokwenda shule."
Bashiru alimsikia waziri wake katika hilo?
Na je yeye hapendi kazi na bata?
Akitoka kwenye ziara zenye msululu wa v8s hapati msosi mnono na hoteli nzuri ya kulala?

Hapati kinywaji baridi kupooza koo na kusindikizwa na upepo mwanana ufukweni?

Nyumba anayoishi haijazungukwa na ulinzi mkali,viyoyozi lukuki na wasaidizi kibao wa kazibali mbali za nyumbani

Tuseme ukweli tu,kazi na bata ndiyo maisha yanayopendeza,lakini kukandamiza kwa kigezo Cha maendeleo sio poa kabisaaa


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom