Dkt. Bashiru awashangaa wapenda ‘Kazi na Bata’. Asema kauli hiyo inachangia kuzorotesha Uchumi

Dkt. Bashiru awashangaa wapenda ‘Kazi na Bata’. Asema kauli hiyo inachangia kuzorotesha Uchumi

Naona unakuja na matusi, muungwana huongea lugha iliyojaa busara! Anyway, tatizo linaloonekana hapo ni msisitizo wa kula bata, ikimaanisha watu wafanye starehe! Sasa kula bata iwe kauli mbiu, unafikiri jamii inachukuliaje? Wapo watakaofikiri kuwa kumbe kufanya starehe ni lazima hata kama uchumi hauruhusu kufanya hivyo (hii ndio maana ya kauli mbiu, in other words we can say it is a command).

Mtu akifanya kazi, akichoka, atahitaji kupumzika, kula, au hata kunywa (it is a natural phenomenon), huhitaji kumwambia ‘nenda kale’. Hata Nyerere alipojenga hizo kumbi alijuwa kuwa kuna wakati watu watachoka na watahitaji kupumzika, lakini kamwe hakuwalazimisha kula bata, maana alijuwa kungekuwa na mapokeo ambayo yangeleta impact mbaya kwenye uchumi aliouanzisha.
Hakuna kulazimishana hapa ila ni kukumbushana kuwa KAZI NA BATA kama ilivyo HAPA KAZI TUU ambavyo siyo kulazimisha kwamba watu wafanye kazi tuuuuuu.
Upande wa lugha niseme samahani sana kama sijaleweka maana matusi siyo sitahili yangu ya uhandishi.
 
Dr yuko sahihi sana. Anachomaanisha hapa ni kuwa kipaumbele ni kujenga uchumi na sio kudumaza uchumi. Ukihubiri kazi na bata (sijuwi kama na yenyewe ni kauli mbiu), tafsiri yake ni kuwa ‘fanya kazi na kipato upatacho tumia kwa starehe’ (no saving). Sasa huu ni uchumi wa aina gani?

Nakumbuka wakati fulani tulipokuwa shuleni kuna msemo tulikuwa tunasema ‘work done equal to zero’ pale ikionekana mtu amejitahidi kufanya jambo fulani lakini hakuna matokeo, hili nalifananisha na kazi na bata, maana kipato unachopata unakitumia kwa starehe, kesho huna kitu. Tupige kazi, tupate kipato, and then we save for future investment!

Hayo mawazo ya kizamani Kazi na kulabata ndio inayotakiwa wao wanatembelea magari ya V8, wanaenda likizo za sabbatical leave ulaya, wakija huku wanasema tusile bata! Land cruiser V8 ni sawa na Ambulances [emoji603] ngapi? Hapo mnakuza uchumi?
 
CCM ITASHINDA KWA KISHINDO kuna jamaa zangu ni wabunge wa upinzani huwa nawaambia kabisa watafute shuguli ya kufanya
True tena Wa 300% si mnamiliki fingerprints na data base za majina ya watz,mtashindwa vipi sasa,
 
Huwezi kula bata bila kazi ajatembea huyu aende ulaya akaone bata linavoliwa tena na manyoya yake na kazi wanapiga balaa.Mimi nimewaelewa first world huwezi ukawa masikini ukapewa uongozi wanaogopa utawaletea kansa ya umasikini.Umasikini uletwa na watu wenye mawazo ya ukale,bata is a personal life pia ni hobby
 
Hicho kimsemo ndio kinawakosesha raha kina Bashiru et el bora wakajinyonge kwa kutumia uzi kama vipi!...Membe mbele kwa mbele.!,Jiandaeni kisaikolojia。
 
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Dkt. Bashiru Ally, amewataka wananchi kupuuza kauli ya kufanya kazi na kula Bata ambayo imeratibiwa na Mbunge wa Kighoma Mjini Zitto Kabwe na kusema kauli hiyo itachangia kuzorotesha uchumi wa Taifa.

Dkt. Bashiru amesema kuwa, katika nchi ambayo wananchi wanapambana kujikomboa kiuchumi, hasa katika nchi zetu za Afrika ambazo bado tupo nyuma kimaendeleo ya mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla, kutokea kiongozi mmoja kuwaambia watu wafanye kazi kwa starehe ni usaliti mkubwa wa mapambano ya kiuchumi.

“nchi hii ambayo tunaongoza mapambano ya kujikomboa kiuchumi, inamuhitaji kila mtu kwa nafasi yake kuhimiza kufanya kazi kwa bidii, na huku CCM kuna kauli mbalimbali za kuhimiza kazi zikiwemo, Hapa Kazi tu, Kazi na Maendeleo, Uhuru na Kazi na Kazi ni Utu, ila kuna baadhi ya Vyama wao wanahubiri kazi na starehe, na huo ndiyo utofauti wa Chama kiongozi na Vyama vya uchaguzi.’’ Dkt. Bashiru

"Unaposema kazi na bata, maana yake ni kudharirisha wanawake na mama zetu ambao wakati wote wamekuwa wakifanya kazi kusomesha watoto wao, wakifanya kazi kulisha familia zao, na sote hapa ni matokeo ya juhudi kubwa za mama zetu, ambao kuwambia wale bata, ni sawa na kuwataka washinde kwenye starehe huku watoto wakidhalilika kwa kutokwenda shule."
Bila shaka huyo msomi hakuielewa vema kauli ya ZZK; au amechagua kuipa tafsiri hasi ili impe kiki ya kisiasa. Hakika si kila aliyesoma sana kaelimika; kinyume chaweza kuwa ukweli!


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Nanza kupata picha ya kauli ya (WANYONGE)
Katibu Mkuu CCM Dr.Bashiru Ally amewaomba Wananchi kupuuza sera na kauli zinazotolewa na baadhi ya Viongozi wa Kisiasa Tanzania zikitaka wale bata (starehe) badala ya kazi na kusema jambo hilo lisipokemewa litasababisha Taifa kuwa legelege, tegemezi na kula bata badala ya kazi.
_
“Katika Nchi ambayo Wananchi wanapambana kujikomboa kiuchumi, hasa ktk nchi zetu za Afrika ambazo bado tupo nyuma kimaendeleo ya Mtu mmojammoja na Taifa kwa ujumla, kutokea Kiongozi na kuwaambia watu wafanye kazi kwa starehe ni usaliti mkubwa wa mapambano ya kiuchumi”-Dr.Bashiru
_
“Unaposema kazi na bata, ni kudhalilisha Wanawake na Mama zetu ambao wakati wote wamekuwa wakifanya kazi kusomesha Watoto, wakifanya kazi kulisha familia zao, kuwambia wale bata,ni sawa na kuwataka washinde kwenye starehe huku watoto wakidhalilika kwa kutokwenda shule”-Dr.Bashiru

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom