MTANZANIA620
Member
- Jun 20, 2023
- 65
- 81
Mbunge wa Jimbo la Vunjo Mheshimiwa Dkt Charles Stephen Kimei ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuwa imeendelea kuwekeza kwenye miundombinu ya vifaa vya uchunguzi na vifaa tiba katika kuboresha huduma kwenye vituo vya kutolea huduma za afya hapa nchini ikiwemo Jimbo la Vunjo.
Ambapo katika kipindi cha miaka takribani minne Jimbo la Vunjo limenufaika kwa kupata mashine ya ultrasound, mashine mpya ya kisasa ya kutolea huduma za kinywa na meno, digital X -Ray na gari la wagonjwa. Kituo cha Afya Himo kitaanza kutoa huduma ya X - Ray baada ya taratibu za ukaguzi toka tume ya mionzi kukamilika.
Aidha, Serikali imeendelea kuboresha huduma za afya ya msingi katika Jimbo la Vunjo kwa kujenga zahanati na vituo vya afya ikiwa ni kuweza kufikia azma ya kumuwezesha mwananchi kupata huduma za afya ndani ya kilomita 5 toka kwenye makazi yake ikiwa ni utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM 2020 - 2025.
Ameongeza kuwa katika kipindi kifupi Jimbo la Vunjo limeshuhudia mabadiliko makubwa kuanzia sekta ya elimu, Afya, Maji Safi, miundombinu ya barabara na umwagiliaji, umeme na ufugaji ikiwa ni dhamira na upendo wa dhati wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.
Dkt Kimei amesema ni kazi nzuri ya maendeleo iliyofanyika kila kona katika Jimbo la Vunjo ambayo itakua nyenzo muhimu ya kukipa ushindi Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi wa serikali za mitaa Novemba 27, 2024.
#VunjoTumechagua
#CCMTeamMaendeleo
#MaendeleoKwaVitendo
#TeamMaendeleo
#HatunaMbadala2025
#KaziIendelee
Ambapo katika kipindi cha miaka takribani minne Jimbo la Vunjo limenufaika kwa kupata mashine ya ultrasound, mashine mpya ya kisasa ya kutolea huduma za kinywa na meno, digital X -Ray na gari la wagonjwa. Kituo cha Afya Himo kitaanza kutoa huduma ya X - Ray baada ya taratibu za ukaguzi toka tume ya mionzi kukamilika.
Aidha, Serikali imeendelea kuboresha huduma za afya ya msingi katika Jimbo la Vunjo kwa kujenga zahanati na vituo vya afya ikiwa ni kuweza kufikia azma ya kumuwezesha mwananchi kupata huduma za afya ndani ya kilomita 5 toka kwenye makazi yake ikiwa ni utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM 2020 - 2025.
Ameongeza kuwa katika kipindi kifupi Jimbo la Vunjo limeshuhudia mabadiliko makubwa kuanzia sekta ya elimu, Afya, Maji Safi, miundombinu ya barabara na umwagiliaji, umeme na ufugaji ikiwa ni dhamira na upendo wa dhati wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.
Dkt Kimei amesema ni kazi nzuri ya maendeleo iliyofanyika kila kona katika Jimbo la Vunjo ambayo itakua nyenzo muhimu ya kukipa ushindi Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi wa serikali za mitaa Novemba 27, 2024.
#CCMTeamMaendeleo
#MaendeleoKwaVitendo
#TeamMaendeleo
#HatunaMbadala2025
#KaziIendelee