Dkt. Damas Ndumbaro amekutana na kufanya mazungumzo na Uongozi wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania na Uongozi wa Jumuiya ya Mabohora Tanzania

Dkt. Damas Ndumbaro amekutana na kufanya mazungumzo na Uongozi wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania na Uongozi wa Jumuiya ya Mabohora Tanzania

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

WAZIRI DKT. DAMAS NDUMBARO AMEJADILI MCHAKATO WA KATIBA MPYA NA TAASISI ZA DINI MBALIMBALI

Waziri wa Katiba na Sheria, Mheshimiwa Dkt. Damas Ndumbaro amekutana na kufanya mazungumzo na Uongozi wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania na Uongozi wa Jumuiya ya Mabohora Tanzania tarehe 13 Mei, 2023 jijini Dar es Salaam.

Mhe. Dkt. Ndumbaro amepata wasaa wa kujadili masuala mbali mbali yakiwemo masuala ya Mchakato wa Katiba Mpya, Marekebisho ya Sheria ya Ndoa na Kampeni ya Kitaifa ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia “Mama Samia Legal Aid Campaign”.

Katika mazungumzo hayo uongozi wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania uliongozwa na Mufti na Shekh Mkuu wa Tanzania Sheikh Aboubakari Zuberi na upande wa Jumuiya ya Mabohora uliongozwa na Sheikh Taiyebali Patanwala, Mwakilishi Mkazi wa Jumuiya hiyo na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Mabohora nchini Tanzania.

Aidha, Waziri wa Katiba na Sheria, Mheshimiwa Dkt. Damas Ndumbaro ameshiriki Mkutano Mkuu wa Chama cha Mawakili Tanganyika tarehe 11 Mei,2023 jijini Arusha katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Arusha. Mkutano huo umefunguliwa na Mheshimiwa Dkt. Philip Isdor Mpango, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

WhatsApp Image 2023-05-14 at 10.28.10(2).jpeg
WhatsApp Image 2023-05-14 at 10.28.10.jpeg
WhatsApp Image 2023-05-14 at 10.28.09(2).jpeg
WhatsApp Image 2023-05-14 at 10.28.09(1).jpeg
WhatsApp Image 2023-05-14 at 10.28.09.jpeg
 
Waongelee na kuhusu vipaza sauti mitaani.
 
Hivi kuna Waafrica weusi ambao wanafuata madhehebu ya Uislam wa Kibohora
 
Back
Top Bottom