Dkt. Dorothy Gwajima: Kama unataka nitumbuliwe ili uchukue nafasi yangu, fanya kazi zaidi yangu sio ufitini

Dkt. Dorothy Gwajima: Kama unataka nitumbuliwe ili uchukue nafasi yangu, fanya kazi zaidi yangu sio ufitini

Kama mpaka leo hujui anayeiba dawa au zinakwenda wapi,huwezi kuwa Mtanzania.
Kule Ikwiriri wananchi Watanzania wanajua dawa zinaibiwa,wanajua wanaoziiba na wanajua zinapelekwa wapi,lakini cha ajabu wameripoti PCCP, Polisi na mpaka kwa DSO,lakini hamna hatua njema iliyochukuliwa.
Ukiona hivyo ujue hayo ni majungu
 
Acha maza aendelee kutuburudisha kwa vichambo.

Nampenda huyu mama kwa staili yake ya kuongea.

Madaktari mtanyooka tu na mimi nasema awanyooshe tu cumamae zenu😂😂😂 maana hakuna namna nyingine.

Lugola alikua ananinyooshea polisi, huyu mama amekuja kuwanyoosha madaktari. Safi sana.
Kwa akili fupi kama hizi Tanzania itachukua miaka mingi kupata maendeleo
 
Maneno meengi hayatazuia watu kuiba dawa. Ni mabadiliko ya taratibu na kanuni ndio huleta mabadiliko mahali popote penye watu wengi. Atapiga kelelee mwishowe ataondoka bila mabadiliko yoyote.
She must come with solutions not noises.
Aje na mikakati mipya ya kudhibiti wizi wa dawa
 
Kuna priority Mkuu, una Paracetamol chache mtu anakuja na mild pain ukimwangalia unamuona kbs akipumzika maumivu yanaweza isha sasa kwanini usizitunze ili akija mwenye maumivu makali ndo umpe
Hoja kuntu labisa na ukiangalia zile dawa zilikuwa kwa dirisha la bima ni inbox 30 tu ambaozo ni sawa na makopo matatu
 
Mkuu kaa utulie, matatizo makubwa kwenye sekta ya afya nchi hii ni idadi ndogo ya watumishi, dawa hazitoshi, miundombinu mibovu, vifaa tiba ni tatizo, bima ya afya yenyewe majanga matupu, seminars zote zimefutwa siku hizi. Kwahiyo yote anayoyazungumza mzizi mkuu upo kwenye matatizo hayo hapo juu, yeye hajikiti kwenye kutatua hayo anajikita kwenye matokeo ya hayo matatizo, ukimchunguza sana anatafuta KiKi kutoka kwa mkulu...
kwa hiyo wabadhirifu wa mali za umma waachwe waendelee na ujanja wao?! huyu waziri ni muwazi na ni mtu mkweli hapindishi hata kidogo, alipigwa majungu sana kwaajili ya misimamo yake, walaji kama kawaida wakampiga jungu na fitina, lkn alhamdulilai JPM ni mtu asiye endekeza wala kusikiliza majungu kampa uwaziri, sasa watu walewale wanaliazisha jungu tena

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa kwanini daktari amwandikie mgonjwa paracetamol kwenye prescription note. Si angemwambia akapumzike hayo maumivu yake sio makubwa yatapoa.

Kama ni uhaba pia kuna swala la uzembe ambalo alishalizungumzia kwenye ziara yake nyingine wanatakiwa kuelewa maswala ya inventory control sio unakaa mpaka dawa zinaisha kabisa ndio maana anataka appraisal system sasa ya wafanyakazi kwenye hivi vituo vya afya inaonekana kuna watu wana nafasi huko mahospitalini wakati hawana qualification nor training za health management.

Kilichotokea hapo japo akijaonyeshwa walitaka kumuongopea dawa hakuna yeye akatumia auditing skills zake ikabidi waseme ukweli ndio maana akawaambia angekuwa mwanasheria si wangemuongopea because you don’t think they would do know how to go about to uncover the truth.

Hiyo wizara imepata kiboko yake, sema anaonekana mama ana akili na watu wenye akili wanatabia ya dharau wanapoongea hiyo kidogo ndio inaweza onekana kama weakness yake kwa watu wengine, but me like it.
Unangeea utopolo tu wew uanfikiri watu wananunua dawa mda wote kwamba hela ya kufanya hivyo ipo tu MDA wote
 
Anawaita afya officers wezi wa dawa [emoji23][emoji23][emoji1787][emoji1787]
 
Hauko sawa hata kidogo nikuulize tu kama ushawahi kufuatilia huduma za afya kwenye Hospitali yoyote ile ya Serikali, Hakuna hata moja utanikuta salaam yaani haina malalamiko kutoka kwa wagonjwa kwa hivyo Waziri lazima apambane nap kadri ya uwezo wake mbali na taaluma kwakuwa Watanzania wengi wakiwa kwenye majukum yao hujisahau Sana . Mama Dr. Dorothy yupo sawa na katika kufanya mambo yaende mda mwingine lazima umpeleke mtu mchakamchaka ndio aelewe nini anatakiwa kufanya kazi ifanyike kama inavyotakiwa.
 
Ukimfuatilia vizuri wala hata hakuna anayemnyoosha hadi sasa. Yeye ni full kubwabwaja tu. Yaani hata haeleweki kama kweli yupo serious au labda anafanyia mzaha hiyo kazi. Huyu waziri utendaji wake haueleweki kabisa.
Tangu niifahamu id hii nimesoma bonhe la point
 
Uongozi ni hekima. Sio ku"rap".

Kwa mfano, kama yeye hadanganyiki na anawajua wezi wa dawa, anatakiwa aweke mtego awakamate kisha wapelekwe mbele ya sheria, sheria ichukue mkondo wake.

Tunataka vitendo, sio maneno!


YESU NI BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU.
 
Wana uhusiano gani na Askofu Gwajima? Wte wawili wana kipaji cha kuongea (good oraters).
 
Wakuu habari za mchana.
Naomba walio karibu na huyu mama waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na watoto, wampe semina ya ku-behave kama top government official. Naona hilo linamshinda. Mama atulize ubongo aje na solutions. Aache majungu na malalamiko kila kukicha.

Hizi clip tunazoziona hazimpi heshima kabisa. Anajiita Field Marshall wa wizara lkn mimi namuona bado sana.
Kama ana vinyongo na maumivu ya huko nyuma, asahau. Ajulishwe majukumu yake kama waziri. Aache kuleta viswahili kama vya vijiwe vya kina mama wakiwa peke yao.
Acha watu mnyooke! Wizara ya Afya ni wizara ya hovyo kabisa! Ukiwachekea hawa, kesho tu utasikia wanaingiza maji kwamba ni chanjo ya polio. Walishafanya hawa. Halafu wanadhani hawaguswi kwa makosa yao. Wizi ni wizi tu!
 
Tahadhima kwenu wajumbe wa bodi huru!

KWA muda sasa nimekuwa nikimfuatilia kwa karibu Waziri huyu toka alipoteuliwa na Rais Magufuli kuwa Waziri wa Afya. Namzungumzia Dk. Dorothy Gwajima.

Kila ofisi zilizochini yake anapoingia huwadhalilisha sana madaktari wenzake. Dk. Gwajima anamtazama kila mtu kuwa ni mwizi na kujitapa kuwa hakuna anayejua kila kitu katika wizara hiyo kama yeye.

"Hivi mnajua mimi ni Field Marshal wa sekta ya afya?" anawafokea madaktari Bingwa zaidi yake na kuongeza, "kama ningekuwa Mwanasheria mngenidanganya sana" kuonesha kuwa mtangulizi wake Mwanasheria, Ummy Mwalimu alikuwa akidanganywa sana. Huku ni kumdharau Waziri mwenzie aliyeaminiwa na Rais Magufuli.

Lakini hata "body language" ya mama huyu inaonesha kuhemka mno kiasi Cha kufanana na kina mama "ndala ndefu" wa huko Tandale wanaochambana bombani huku ameshika kiuno.

Cha ajabu, kama alivyowahi kufanya Dk. Hamisi Kigwangala "mzee wa kukurupuka" naye kila anapotaka kuwadhalilisha wahudumu wa sekta hiyo ni lazima awe mbele ya kamera ili aonekane. Huyu mama ameenda mbali kiasi Cha kutorokwa hata na haiba na staha ya mwanamke wa Kitanzania mbele ya wanaume.

"Field Marshal" ni cheo Cha juu na Cha mwisho jeshini. Hivi, Dk. Gwajima anadhani ni Bingwa wa afya kuliko maprofesa wote wa tiba nchini? Kwani kuongoza ni lazima kudhalilisha wenzako hadharani?

Wakati yule "mkata viuno" aliyetembea na Ilani ya CCM akijiita "ninja" huyu kaja na skafu ya bendera akijiita "Field Marshal". Mwendo uleule wa kukurupuka na kujipendekeza.

My Take: Napendekeza madaktari wafuatilie faili lake la matibabu anakotibiwa kuona anasumbuliwa na ugonjwa gani? Yapo baadhi ya magonjwa ambayo humfanya mtu ku-react ukichaa kama mama huyu.

Lakini pia wadadisi wachunguze mahusiano yake ya ndoa. Je, ana familia au ni mtalikiwa? Maana mahusiano ya ndoa na familia yakiwa salama pia huleta utulivu katika uongozi wenye staha, hekima, busara na maarifa. Huwezi kukufanya kuwa wizara hiyo imeoza kiasi kwamba waliopita kabla yake hawakufanya chochote. By the way, si tunaambiwa utawala wa Magufuli umeondoa ufisadi na uzembe kazini?

Nawasilisha.
Leo hii ndo unashangaa majina ya Field Marshal? Hukuwahi kusikia Komando? Hukuwahi kusikia Maji marefu? Naona kama wewe ndo mende tu! Wizara hiyo tunawajua. Miaka yote munajidai ni wizara ya kitaalamu mnooo!! kumbe wapi! Wizi tu! Tangu wizarani hadi dispensary ni wizi tu. Ndo mulichosomea? Lazima mtu ahangaike nanyi.
 
Back
Top Bottom