Dkt Faustine Ndugulile ashinda kinyang'anyiro cha ukurugenzi Mkuu wa WHO kanda ya Afrika

Dkt Faustine Ndugulile ashinda kinyang'anyiro cha ukurugenzi Mkuu wa WHO kanda ya Afrika

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
166770147_10158884573395901_6487832966852889114_n.jpg

Mbunge wa Kigamboni na Naibu Waziri wa Afya wa zamani Dkt. Faustine Ndugulile, ameshinda uchaguzi wa kiti cha Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani Kanda ya Afrika.

Katika Uchaguzi uliofanyika leo jijini Brazzaville nchini Congo, wajumbe 25 kati ya 46 wa Mkutano Mkuu wa 74 wa WHO uliofanyika leo wamemchagua Ndugulile na hivyo kuwashinda wagombea wengine kutoka Niger na Senegal.

Tayari Ndugulile ameeleza wazi kuwa vipaumbele vyake ni kuhakikisha Watu wanapata haki ya kupata huduma bora za afya, kuboresha utayari wa nchi za Afrika katika kukabiliana na majanga ya magonjwa ya mlipuko, kuimarisha uwajibikaji ndani ya WHO kanda ya Afrika pamoja na kuimarisha mawasiliano baina ya nchi wanachama katika masuala ya Afya.

Soma Pia: Kama Dkt. Ndugulile atateuliwa kuwa Mkurugenzi wa WHO (Afrika) basi Komredi Makonda atakuwa na Nafasi ya kugombea Ubunge Kigamboni
 

Attachments

Ndugu zangu Watanzania,View attachment 3080893View attachment 3080895

Kazi iendelee , Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Kazi iendelee, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Kwahiyo mama nae kapiga kura au kama kawaida yako mkuu? Kama kuna walio bubujika na machozi ya furaha tuambie pia.
 
Watu kama hawa ndio wanatakiwa wadumu kwenye wizara za afya na mambo yote yahusuyo wizara hiyo.

The richest man in tge babylon kitabu kile kinasema ili ufanikiwe ni lazima upate mtaalamu wa jambo hilo ndio afanye kwa ufanisi jambo hilo.
 
Ndugulile kama Ndugulile namkubali.

Alivyokuwa Teknolojia alikuwa na mipango mingi mizuri, halafu aliji mix vizuri na watu.

Hii position inahitaji mtu makini na itamfaa sana.
Impact yake ni ipi? Kwahiyo wizara na taifa kwa jumla.
 
Impact yake ni ipi? Kwahiyo wizara na taifa kwa jumla.
Watu wengi wenye uwezo wanashindwa kuwa na impact kwa sababu za kimfumo.

Sasa Waziri unataka kuweka impact kwa chanjo harafu rais Jiwe hataki chanjo, hapo utaletaje impact?

Sasa Waziri una madini kibao ya kuweka impact lakini rais boya, na kila kitu kazima kipitishwe na rais, hapo Waziri akikosa impact utamlaumu?

Ndiyo hao wajanja wanaona hawawezi kuwa na impact ndani wanaenda kufanya kazi UN huko kutoa maagizo Afrika nzima yamewaruka marais wote.
 
Back
Top Bottom