Jambo hata liwe jema likigubikwa na nia ovu si jambo jema tena. Mwaka 2018 Mwakyembe akiwa kwenye baraza la Mawaziri swala la vita ya ushoga lilipamba moto baada ya Paul Makonda aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam kutangaza vita kali sana dhidi ya watu wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja.
Pamoja na vita kupamba moto serikali yetu chini ya Rais Magufuli ilijitenga na Makonda na kampeni yake kwa kile ilichokiita si msimamo wa serikali bali ni mawazo binafsi ya Makonda na kwamba serikali bado inaheshimu katiba na mikataba ya kimataifa iliyoiingia.
Rejea
Serikali: Kampeni ya kupambana na Ushoga ya RC Makonda sio msimamo wa nchi
Katika kipindi hiki Dr Mwakyembe na wenzake wote waliokuwa vipenzi wa Magufuli walikaa kimya hakuna mtu aliyejitokeza kumuunga mkono Paul Makonda kwenye vita ya ushoga. Walimwacha Paul Makonda akikaangika kimataifa akipata kibano cha vikwazo mbalimbali mpaka sasa Paul Makonda haruhusiwi kukanyaga Ulaya. Kwa kauli hiyo ya serikali, serikali iliweza kupata misaada na mikopo mbalimbali kimataifa pamoja na kwamba uhusiano wa serikali ya awamu ya Tano kimataifa haukuwa mzuri sana.
Baada ya Rais Samia Suluhu kuingia ikulu ni wazi kwamba ushirikiano wa kimataifa umeimarika sana, serikali yetu inaweza kushirikiana na kupata Wawekezaji kutoka mataifa mbalimbali nje ya bara la Afrika. Sasa kumeibuka tena hili swala la vita ya ushoga watu walewale Mwakyembe, Majaliwa, Mpango, Ndugai etc waliomshauri Rais Magufuli amkane Makonda na kampeni ya vita dhidi ya watu wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja wanaibuka kama vinara wa vita dhidi ya ushoga ni nini kimebadilika?
Watu hao ni vipenzi wa mwendazake bila shaka hawafurahii kuona Mama Samia akifanya vizuri katika ushirikiano wa kimataifa na kuvutia Wawekezaji hivyo hii vita ya ushoga ni kama kichaka tu, lengo Lao Mama Samia aingie katika mtego huo ili nchi sasa ipate vikwazo kabambe sifa yake kimataifa iharibike, uwekezaji ushuke aweze kufeli. Hii ni vita ya madaraka inaonekana ndani ya CCM bado ni mbichi. Ukiangalia hata timing ya hizi press conference za Mwakyembe ni siku moja kabla ya ujio wa Makamu wa Rais wa Marekani. Ni kweli hili swala limeibuliwa na Uganda lakini hawa kina Mwakyembe wameona ni vyema wapite na upepo huu maana hakuna nafasi nyingine watapata ya kumharibia Mama Samia.
Chonde Chonde Mama Samia wakati kama huu ni wa kuwa makini sana na maamuzi yako, maadui zako wanakusubiri mitego yao inashawishi na kutamanisha sana