Crocodiletooth
JF-Expert Member
- Oct 28, 2012
- 20,561
- 24,428
Unamdanganya mwenzako, mashoga wapo kibao miaka na miaka.tanzania haisapoti ushoga kamwe, inafahamika upo inashughulika nao kimya kimya bila kuropoka hovyo na hatimaye kuharibu diplomasia ya nje, Tanzania inaulaani ushoga, lakini kupiga kelele na matamko hakusaidii endapo hakuna actions za kiakili zinazoendelea chini chini, mwizi wetu atakamatwa kimya kimya!
WametumwaJambo hata liwe jema likigubikwa na nia ovu si jambo jema tena. Mwaka 2018 Mwakyembe akiwa kwenye baraza la Mawaziri swala la vita ya ushoga lilipamba moto baada ya Paul Makonda aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam kutangaza vita kali sana dhidi ya watu wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja.
Pamoja na vita kupamba moto serikali yetu chini ya Rais Magufuli ilijitenga na Makonda na kampeni yake kwa kile ilichokiita si msimamo wa serikali bali ni mawazo binafsi ya Makonda na kwamba serikali bado inaheshimu katiba na mikataba ya kimataifa iliyoiingia.
Rejea Serikali: Kampeni ya kupambana na Ushoga ya RC Makonda sio msimamo wa nchi
Katika kipindi hiki Dr Mwakyembe na wenzake wote waliokuwa vipenzi wa Magufuli walikaa kimya hakuna mtu aliyejitokeza kumuunga mkono Paul Makonda kwenye vita ya ushoga. Walimwacha Paul Makonda akikaangika kimataifa akipata kibano cha vikwazo mbalimbali mpaka sasa Paul Makonda haruhusiwi kukanyaga Ulaya. Kwa kauli hiyo ya serikali, serikali iliweza kupata misaada na mikopo mbalimbali kimataifa pamoja na kwamba uhusiano wa serikali ya awamu ya Tano kimataifa haukuwa mzuri sana.
Baada ya Rais Samia Suluhu kuingia ikulu ni wazi kwamba ushirikiano wa kimataifa umeimarika sana, serikali yetu inaweza kushirikiana na kupata Wawekezaji kutoka mataifa mbalimbali nje ya bara la Afrika. Sasa kumeibuka tena hili swala la vita ya ushoga watu walewale Mwakyembe, Majaliwa, Mpango, Ndugai etc waliomshauri Rais Magufuli amkane Makonda na kampeni ya vita dhidi ya watu wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja wanaibuka kama vinara wa vita dhidi ya ushoga ni nini kimebadilika?
Watu hao ni vipenzi wa mwendazake bila shaka hawafurahii kuona Mama Samia akifanya vizuri katika ushirikiano wa kimataifa na kuvutia Wawekezaji hivyo hii vita ya ushoga ni kama kichaka tu, lengo Lao Mama Samia aingie katika mtego huo ili nchi sasa ipate vikwazo kabambe sifa yake kimataifa iharibike, uwekezaji ushuke aweze kufeli. Hii ni vita ya madaraka inaonekana ndani ya CCM bado ni mbichi. Ukiangalia hata timing ya hizi press conference za Mwakyembe ni siku moja kabla ya ujio wa Makamu wa Rais wa Marekani. Ni kweli hili swala limeibuliwa na Uganda lakini hawa kina Mwakyembe wameona ni vyema wapite na upepo huu maana hakuna nafasi nyingine watapata ya kumharibia Mama Samia.
Chonde Chonde Mama Samia wakati kama huu ni wa kuwa makini sana na maamuzi yako, maadui zako wanakusubiri mitego yao inashawishi na kutamanisha sana
Mtafute Dr. Mariposa atakutetea kizimbani.[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]sina mwanasheria mie.
Sawa mkuu tupe code tutafungua wenyewe[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]sina mwanasheria mie.
Dr. Mariposa unaitwa huku daktariMtafute Dr. Mariposa atakutetea kizimbani.
Ila mbon wanatajwa sana hao mabwana kwenye hii issue imekuaje kuna kaukweli au wanapakaziwa? Eti mkuu[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] waache watu na maisha yao bhanaa.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] kwahiyo wapakaziwe wao tyuuhIla mbon wanatajwa sana hao mabwana kwenye hii issue imekuaje kuna kaukweli au wanapakaziwa? Eti mkuu
Ningekuwa moderator ushakula life ban kitambo sana na mashoga wenzio.Mtakapojua lengo kuu la hizi promo za ushoga mnaojifanya kuzipinga, mtakua msha chelewa.
Kaeni kwenye vimbwetaa vya wanafunzi wa chuo, jinsi wanavyohamasika kuingia huko, hata wasiojua wanajisemea "tukashuhudie kwann unazungumzwa sana" wanaishia kugeuzana zamu zamu.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Tunaomba kufahamu ni chuo gani? Na sehemu wanayo kwendaMtakapojua lengo kuu la hizi promo za ushoga mnaojifanya kuzipinga, mtakua msha chelewa.
Kaeni kwenye vimbwetaa vya wanafunzi wa chuo, jinsi wanavyohamasika kuingia huko, hata wasiojua wanajisemea "tukashuhudie kwann unazungumzwa sana" wanaishia kugeuzana zamu zamu.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Wewe nawe ni wq upinde? Inamaana tatizo mtaani kwako hujaliona? Badala umsifie mwanaume katoka hadharani kulaani wewe unamuaattack!? Una akili wewe?Nimejaribu kutafakari taarifa ya mwakyembe siielewi.
1. Ni mbinu Zipi alizotumia kubaini hawa mashoga, serikali haikuweza?
2. Ana mantiki gani Kuja hadharani kujimwabafai yeyé kama yeyé. Kwa Nini asingeyapeleka hayo majina mapema. Kimyakimya.?
3. Nilitegemea nisikie akisema alishawasilsha majina Mda mrefu lakini hayajafanyiwa Kazi.
4. Je agenda ya ushoga imekuja kufifisha madai ya msingi ya wananchi na kuficha mazaifu makubwa ya serikali Awamu ya sita?
Alilosema ni kweli kabisa usimshambulie Mkuu, ukifahamu mambo yanayofanywa na vikundi vya vijana wa vyuo unaweza ukachoka kuishi kabisaNingekuwa moderator ushakula life ban kitambo sana na mashoga wenzio.
NGO yake itakuwa imetajwa na MwakyembeWewe nawe ni wq upinde? Inamaana tatizo mtaani kwako hujaliona? Badala umsifie mwanaume katoka hadharani kulaani wewe unamuaattack!? Una akili wewe?
Mnageuzana kwa raha zenu [emoji3]Mtakapojua lengo kuu la hizi promo za ushoga mnaojifanya kuzipinga, mtakua msha chelewa.
Kaeni kwenye vimbwetaa vya wanafunzi wa chuo, jinsi wanavyohamasika kuingia huko, hata wasiojua wanajisemea "tukashuhudie kwann unazungumzwa sana" wanaishia kugeuzana zamu zamu.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]