Dkt. Kigwangalla kushauri "Herd Immunity" dhidi ya Corona, ndio msimamo wa Serikali?

Dkt. Kigwangalla kushauri "Herd Immunity" dhidi ya Corona, ndio msimamo wa Serikali?

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
53,868
Reaction score
121,001
Hamis Kigwangala ambaye ni daktari wa afya ameandika meengi katika mtandao wake wa instagram. Kwa tafsiri rahisi ni kwamba anashauri herd immunity.

Kutokana na mwenendo wa serikali katika mapambano dhidi ya corona Je,huu ndio msimamo wa serikali?

Mbona maambukizi mapya hayatangazwi,mbona vifo havitangazwi. Upuliziaji wa dawa ya kuua virus huko Dar es Salaam mbona umesitishwa?

Naomba kuwasilisha hoja

----

Kupitia akaunti yake ya Instagram ameandika...

Ugonjwa wa COVID-19 tunao na ushasambaa nchini kote. Ndugu zetu wenye umri mkubwa ama wenye magonjwa mengine wanaathirika zaidi ama wanapoteza maisha kabisa. Hatuna chanjo wala tiba, we are helpless kama binadamu.

Kipindi kigumu sana kwa walimwengu na ulimwengu. Maisha yetu yamebadilika sana na kamwe hayatokuwa sawa tena, baada ya janga hili. Life has changed and shall remain changed for good; pengine mpaka pale tutakapopata chanjo ama dawa ya kutibu COVID-19.

Kwa sasa tunahitaji utafiti wa namna ya kurudi kwenye maisha yetu taratibu. Utafiti utuambie lini tuwe tayari kurudi kawaida. Na siyo mbali sana. Maana tumechoka kuishi kwa mashaka. Pengine tujue tu kuwa haya ndiyo yameishakuwa maisha yetu. Our ‘new normal’.

Utafiti utuelezee new normal itakuwaje. Wananchi wasisitizwe kuishi kwa kuendelea kuchukua hatua za kujikinga dhidi ya Covid-19. Wajue namna ya kuzika sasa inakuwaje, serikali isaidie kushiriki mazishi ya watu wetu watakaopata bahati mbaya ya kifo dhidi ya ugonjwa huu, wawazike kwa mila na desturi za dini zao kwa kuzingatia misingi yote ya kujikinga dhidi ya maambukizi.

Hotel zifunguliwe, watu tuanze kutembea kwa amani, tujamiiane kwa kuzingatia ‘social distancing’ n.k. Hakuna haja ya karantini tena, hakuna haja ya ‘social isolation’ tena.

Kuvaa barakoa ndiyo our new normal. Tuanze kushona za kifashion fashion hivi. Tuzowee. Kunawa mikono kila wakati nayo Ndiyo ishakuwa another new normal. Tuzowee tu. Kukaa mbalimbali, kuto-shake hands ndiyo ishakuwa new normal. Tuzowee tu. Bajeti yetu tuielekeze kwenye tiba na kuwalinda askari wetu wa mstari wa mbele.

Tuwekeze kwenye kuiboresha mifumo yetu ya kuwatibu wale asilimia chini ya 5 watakaopata ugonjwa serious zaidi. Utafiti utakaoambatana na kupima utusaidie kujua ni watu wangapi wanaoweza kuwa wameambukizwa na wakapona na kiwango cha maambukizi kikoje kiasi tujue kama tunaweza kupata kinga ya jamii yote baada ya muda gani? (Herd Immunity).

Jamii ieleweshwe kuwatenga na kuwalinda wazee na wenye magonjwa mengine. Tunahitaji utafiti haraka turudi makazini kama mwanzoni tuishi na adui bila hofu ila kwa tahadhari kama Dance ya Simba na Swala.

Hatuwezi kuendelea kwenda mbele
 
Hakika watu wa Lumumba... kuanzia viongozi na wafuasi wao wote akili zao za hovyo!!

Yenyewe inataka kufanya coronavirus iwe ni sehemu ya maisha ya Watanzania kabla hawajafanya jitihada za kudhibiti maambukizi!!

Yaani yanakurupuka tu na kutaja nchi zinazotaka kuachia lockdown kama justification eti na zenyewe zinataka kuwa kama Tz... very stupid!!

Wanajidanganya hayo bila ya kufahamu wenzao waliweka lockdown ili kudhibiti ugonjwa usisambae sana, na hatimae wana mpango wa kulegeza restrictions kwa sababu wanaona kuna maeneo maambukizi yanashuka, na ndio maana wanafikiria kulegeza restrictions!

Spain kwa mfano ambayo inaongoza vifo Ulaya, hatimae hali inatengemaa na sasa wanafikiria kulegeza restrictions!!

Kuna Walevi wa Lumumba wanajilinganisha na South Korea huku wakisahau discipline kubwa ya wananchi kuishi kulingana na hali iliyopo... discipline ambayo kwa Tanzania HAIPO!!

Na Magufuli asichojua ni kwamba, hata kama dunia mzima maisha yataendelea bado Tanzania itachukuliwa kama radioactive country... itaendelea kuogopwa na wageni!

Utalii unaopigiwa upatu lazima utaendelea kuathirika sana kwa sababu sio tu Watalii wao binafsi watahofia kuingia Tanzania bali hata nchi zao kama Marekani zitaendelea kutoa tahadhali kwa wananchi wake kutokwenda Tanzania kwa sababu itaonekana bado sio salama!!

Kila mwenye akili timamu duniani anafahamu Tanzania ni moja ya nchi ambazo hazijafanya jitihada za maana kudhibiti ugonjwa usienee!!

Badala yake, viongozi wanaongelea watu wakubaliane na hali huku wakiacha kuchukua hatua za maana kudhibiti kusambaza kwa virus!

Na kwa jinsi walivyo wajinga wanadhani kutotoa updates za maambukizi itafanya watu waamini hakuna maambukizi kumbe hapa wanauthibitishia ulimwengu kwamba hatupo serious kwenye hii vita, na kwamba tunaficha takwimu!!

Balozi za nchi kubwa zilizopo Tz zote zina watu ambao moja ya kazi zao ni kutafsiri daily newspapers... Kwahiyo wanafahamu nini kinaendelea inside out hata kama Kiswahili hawakijui!!

Zile maiti zinazookotwa tayari watu wana taarifa zake!

So, staili hii ya kujificha kama mbuni anayeacha kiwiliwili chote nje na kudhani amejificha ni suicide!!!

Watalii watakuwa na confidence ya kwenda mahali kama South Africa ingawaje reported cases ni zaidi ya mara 10 ya Dar kuliko kuingia Tz kunakoonekana hakuna maambukizi!!

Mathalani, leo hii mamlaka za SA zikisema Capetown HAKUNA kabisa maambukizi, Watalii wataamini hata kama Johannesburg mamia kwa mamia watakuwa wanakufa!!

Sasa kuna mtalii gani ataamini taarifa za JPM kwamba norther circuit hakuna maambuki kwahiyo Watalii waendelee kwenda tu?!
 
View attachment 1433011

Hamis Kigwangala ambaye ni daktari wa afya ameandika meengi katika mtandao wake wa instagram. Kwa tafsiri rahisi ni kwamba anashauri herd immunity.

Kutokana na mwenendo wa serikali katika mapambano dhidi ya corona Je,huu ndio msimamo wa serikali?

Mbona maambukizi mapya hayatangazwi,mbona vifo havitangazwi. Upuliziaji wa dawa ya kuua virus huko Dar es Salaam mbona umesitishwa?

Naomba kuwasilisha hoja
This man is rubbish! Herd immunity ni kuwa unaacha Darwins theory of natural selection to take its course! Acha wafe watakaobaki basi watakuwa wamekuwa selected kuhimili virus na hivyo maisha kuendelea na a few selected ones INCLUDING HIM na boss wake! HUWEZI KUWA NA HERD IMMUNITY BILA VACCINATION OF THE MASSES
Nchi ya kishenzi sana hii. na ndio msimamo wa Jiwe, ndiyo maana ameamua kujificha ambao yuko 100% assured hataguswa na walio wake! Ndio maana mnaona PM, VP hawaonekanai katu! Wanasubiri natural selection to take its course maana kwa ulivyo contagious/infectious hiyo itakuwa attained within a short time!
 
OKW BOBAN SUNZU ,

..Mheshimiwa anasema tunahitaji " utafiti. "

..mimi nilitegemea kwa nafasi yake Mheshimiwa angetuambia utafiti huo utafanywa na nani au chombo gani.

..lingine ni kukosekana kwa UONGOZI wakati wa janga hili.

..viongozi wamejificha na kuwaacha wananchi wajiongoze wenyewe.
 
Herd immunity inakuja pale ambapo watu wengi wameugua wakapona, mwili wao umejifunza jinsi ya kupambana na hicho kirusi ili kikirudi tena mtu haugui, kinga ya mwili inashinda mapema tu.

Tatizo sasa ni moja, herd immunity inafaa kwa magonjwa ambayo ukiugua ukapona mwili unajenga kinga ya huo ugonjwa kwa muda mrefu, miezi kadhaa hadi miaka, tatizo la korona ni kua hatujui immunity inakaa muda gani baada ya mtu kupona, kama iingekua muda mrefu basi sawa ila kama inakaa siku chache alafu inapotea herd immunity haiwezi fanya kazi, utakua ukipona baada ya wiki huna kinga unaupata tena.

Kama daktari nilitegemea afikirie kitu kama hicho sio kukurupuka na kutoa solution moja huku anajua sio complete solution. Na hii hua ni last option, mkiwapelekea wazee wenu haka kaugonjwa kwa sababu tu nyie hakawezi kuwaua mkae mjue wao watakufa mapema tu, watanzania wengi umri 50+ wana afya mgogoro, hawafanyi mazoezi, wanakula daily chakula kilekile tu ugali, nyama kibao, unakuta mtu ana tambi limejaa utadhani ana minyoo tani nzima kabeba.
 
View attachment 1433011

Hamis Kigwangala ambaye ni daktari wa afya ameandika meengi katika mtandao wake wa instagram. Kwa tafsiri rahisi ni kwamba anashauri herd immunity.

Kutokana na mwenendo wa serikali katika mapambano dhidi ya corona Je,huu ndio msimamo wa serikali?

Mbona maambukizi mapya hayatangazwi,mbona vifo havitangazwi. Upuliziaji wa dawa ya kuua virus huko Dar es Salaam mbona umesitishwa?

Naomba kuwasilisha hoja
Wewe upo Dunia gani? Mbona kila siku tunaona update kwenye mitandao ya Kitaifa na kimataifa. Wewe ukiandika update Covid-19 itakuonesha.
Serikali ipo Makini kuhakikisha watu wake wapo salama salimini..
 
This man is rubbish! Herd immunity ni kuwa unaacha Darwins theory of natural selection to take its course! Acha wafe watakaobaki basi watakuwa wamekuwa selected kuhimili virus na hivyo maisha kuendelea na a few selected ones INCLUDING HIM na boss wake!
Nchi ya kishenzi sana hii. na ndio msimamo wa Jiwe, ndiyo maana ameamua kujificha ambao yuko 100% assured hataguswa na walio wake! Ndio maana mnaona PM, VP hawaonekanai katu! Wanasubiri natural selection to take its course maana kwa ulivyo contagious/infectious hiyo itakuwa attained within a short time!

..kwenye nchi za wenzetu Mh.Dr.Kigwangala angelazimishwa kujiuzulu kutokana na hiki alichoandika.
 
Mtu mwenye fikra za ‘social cleansing’ halafu kuna mtu kabisa alianzisha thread eti awe waziri wa afya kipindi hiki.

Worst ni M.D by proffesional ulitegemea yeye kwa ethics za alichosomea ndio awe mstari wa mbele kufikiria kuokoa maisha ya watu and not otherwise.
 
Back
Top Bottom