Dkt. Kigwangalla: Mashine ya nyungu iliyo Muhimbili ivunjwe, viongozi wavae barakoa

Dkt. Kigwangalla: Mashine ya nyungu iliyo Muhimbili ivunjwe, viongozi wavae barakoa

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
2F3ADBB1-C654-45B5-9ED4-E4B68D1DB26A.jpeg

Mbunge wa Nzega Mjini, Dkt. Hamis Kigwangalla ameshauri mashine ya kujifukizia iliyowekwa Hospitali ya Muhimbili ivunjwe na watu wafauate hatua za kujikinga na #COVID19 ikiwemo kupata chanjo.

Kigwangwalla amesema wataalamu wa Afya wana jukumu la kumshauri Rais Samia na yeye kama mbunge watalizungumza bungeni ili kuanza kufuata njia za kisayansi.

Amesema si sawa kwa taasisi kubwa kama Muhimbili kuwa na mashine za kupiga nyungu, ni muhimu watu kufuata hatua a afya kama kuvaa barakoa nk

Zaidi, Soma: Baada ya Hospitali ya Taifa Muhimbili kusema hawatavunja mashine za kujifukiza, Kigwangalla ahoji zaidi...
 
Kama ni kweli kasema hivyo duuh, hawa Viongozi wetu hata siwaelewi, na wa Fedha nae kaanza kuongea.

Mimi najiuliza hivi kama waliona yasiyo sawa wakati Mwendazake bado akiwepo kwa nini hawakuthubutu kuhoji?

Hii inaonesha kuwa kwao madaraka ni bora kuliko Wananchi...kwa hiyo wao tukiumizwa sisi huwa wanatuchungulia tu kwa jicho pembe kulinda ugali wao.

Nape alijaribu kupaza sauti kuhusu Kodi wakati bado Mzee akiwepo lakini nadhani naye ni kwa vile alishaona hana cha kupoteza tena.
 
Back
Top Bottom