Pre GE2025 Dkt. Kigwangalla: Mbowe hataki kuachia Uenyekiti, alimfukuza Zitto na sasa anamfanyia figisu Lissu. Tumwite Ayatollah Mbowe au Kabaka Mbowe

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Sawa na ccm watataachia nchi lini tangu ,1961 mpaka Leo hakuna la maana wamefanya zaodi ya rushwa na ufisadi
 
Mkuu matongee,
nikusahihishe kidogo kwenye jina la bwana mdogo Ni pambalu sio pumbulu
 
MBOWE aondoke
Aende wapi? Bado yupo sanaaa, hadi CDM wenyewe waamue!! Naona kuna kile ki dada kilikuwa chadema huko geita, UPENDO, kila muda kinahangaika kuisema chadema,!! Kweli ukiwa magamba hata kama prof. akili yako inazidiwa na mtu wa std seven
 
Chadema kama chama mbadala kilipaswa kuonesha mfano mzuri wa kuheshimu na kufuata misingi ya demokrasia. Kujificha kwenye madhaifu ya ccm ni kuutangazia umma kwamba chadema ni sawa na ccm.
Hakuna mwana ccm anayeitakia mema CDM!! Kipindi cha jiwe mlisema lazima kife, ikashindikana, na sasa kitawatesa sana, kwani wananchi wameshaanza kuelewa
 
Sawa na ccm watataachia nchi lini tangu ,1961 mpaka Leo hakuna la maana wamefanya zaodi ya rushwa na ufisadi
Babu zako waliokuwa wakitembea zaidi ya kilometa 10 kuitafuta shule ilipo wakisoma hii comment yako watakulaani.
 
Chadema kama chama mbadala kilipaswa kuonesha mfano mzuri wa kuheshimu na kufuata misingi ya demokrasia. Kujificha kwenye madhaifu ya ccm ni kuutangazia umma kwamba chadema ni sawa na ccm.
Sawa mkuu,
japo binafsi Sina mlengo wowote kisiasa ngoja tuoneee
 
kwani demokrasia kwa tafsiri yako ni nini?
Demokrasia ni katiba ya nchi au chama ambayo inampa kiongozi wa chama au nchi akae madarakani kwa muda fulani uliyowekwa na chama au nchi husika.

Katiba ya Chadema iliyotungwa wakati wa uanzishaji wa chama ilikuwa ni ya mihula miwili tu ya miaka mitano mitano. Mwenyekiti wa chama aliechaguliwa kidemokrasia na chama aliruhusiwa kukaa madarakani kwa muda wa miaka mitano ya muhula wa kwanza, na endapo atahitaji kuendelea basi itabidi agombee tena na akishinda amalizie muhula wa pili.

Muongozo wa katiba hiyo ulifuatwa na viongozi wote waliotawala kabla ya Mbowe. Alianza mzee Mtei akatawala, mihula yake ilipoisha akatoka kwa mujibu wa katiba na kumpisha mgombea mungine aliegombea na kushinda uenyekiti (Bob Makani)

Marehemu Bob Makani nae akafuata katiba ya chama kwa kutawala mihula miwili kisha akaacha wagombea wengine wapambane, mshindi akawa Mbowe, Bob Makani akamkabidhi kijiti kwa mujibu wa katiba ya chama.

Mziki ukaja kwa Mbowe ambae hakutaka kutoka katika kiti, akaamua kubadilisha katiba ili aendelee kuwa anagombea miaka yote mpaka uzeeni. Na kwa mazingira yetu ya kiafrika ni vigumu sana mtu wa kawaida kushindana na kiongozi aliepo kwenye kiti, maana yeye ndo boss wa wapiga kura wote, na pia boss wa wahesabu kura wote.

So ni rahisi mno kuwadhibiti, kuwahonga au kuwatisha ili wampitishe. Nafikiri umeshasikia Lisu akilalamika juu ya rushwa inavyotembea katika chaguzi. Sasa kwa mantiki hiyo hata kama wanachama hawamtaki mwenyekiti yeye ataendelea kupita tu kwa sababu ana hela za kuwahonga.
kwani hawaruhusu watu wengine kugombea? mbowe huwa anapita bila kupingwa? nisaidie mkuu maana mimi nimezaliwa 2010
Kushindana na mtu aliebadilisha katiba ili miaka yote aendelee kutawala ni kazi bure. Yeye ndio kiongozi wa wapiga kura na wahesabu kura, hivyo uwezekano wa uchaguzi huo kuwa wa haki ni mdogo sana. Ni sawa na mpinzani ashindane na raisi katika uchaguzi. Uwezekano wa mpinzani huyo kushinda uchaguzi huo ni mdogo sana hata kama yeye atakuwa amepata kura nyingi kushinda raisi.

So mkuu usidanganyike na watu kuchukua fomu kushindana na Mbowe, ile ni geresha na hata hao wachukuaji fomu hujua kabisa kwamba hawatoweza kushinda kwa namna yoyote ile.
 
Kama Kuna kitu kitafanya cdm kuonekana ni chama Cha hovyo ni kukubali Mbowe kuendelea kuwa mwenyekiti tena. Katika jambo ambalo siwezi kuunga mkono cdm, ni hiki kitendo Cha kuruhusu kiongozi mmoja kukaa madarakani muda mrefu hivyo. Kwenye hili siko tayari kuunga mkono, na Sina hofu na kamanda yoyote wa cdm hata watukane watakavyo, maana hayo matusi yenyewe nayamudu vyema.

Nilipinga Lowassa kupewa nafasi ya kugombea urais ndani ya cdm bila hofu. Na Sasa naendelea kupinga Mbowe kuwa mwenyekiti muda mrefu kiasi hiki, huku akiwa Hana tija tena.
 
Uko sahihi sana, Mbowe must go. Kwa sasa Mbowe anaipotezea cdm haiba yake, kuliko anachoipa cdm.
 
BWANA mkubwa,
itapendeza utupe merits & demerits za mbowe kuendelea kua mwenyekiti wa CDM
 
Uko sahihi sana, Mbowe must go. Kwa sasa Mbowe anaipotezea cdm haiba yake, kuliko anachoipa cdm.
Na mfumo unataka Mbowe aendelee kuwa mwenyekiti, ili waendelee kumtumia yeye kama kiongozi wa chama kuwafinya kimya kimya wale wote wanaojaribu kuichalenji serikali.

Siku watu wakija kuusikia wasifu wa Mbowe, nina imani wengi watapigwa na butwaa na wengine wataacha kabisa kuwaamini wanasiasa wote wa Tanzania hata wale ambao wanastahili kuaminiwa. Maana inaonesha wazi kuwa wasifu wake hauna tofauti na wa Mrema, sema tu yeye alibahatika kupata watu wenye akili ambao walimsaidia kukitengeneza chama hivyo sasa hivi anakula matunda ya chama na ya kazi yake nyingine.

Bahati mbaya au nzuri wasifu wao hutolewa baada ya muhusika kufariki, hivyo waliopoteza fedha zao na jasho lao kumpigania bila kujua, hawatokuwa na la kuifanya maiti.
 
Uongozi wa Mbowe ni aibu kwa democrasia. Kiongozi unaposhindwa kuandaa wengine kuchukua nafasi yako na kuona kama wewe pekee ndiye anayefaa, hapo umefeli kama kiongozi.

Wajinga wengine watakuja na hoja “kwani katiba yao inasema je? Alafu wanakuja kuomba mabadiriko katiba ya nchi. Aibu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…