Uchaguzi 2020 Dkt. Magufuli atinga Kagera, Mama Tibaijuka asema watampa kura za heshima na kusisitiza wao ni 'Natural Allies'. Magufuli amuahidi cheo

Uchaguzi 2020 Dkt. Magufuli atinga Kagera, Mama Tibaijuka asema watampa kura za heshima na kusisitiza wao ni 'Natural Allies'. Magufuli amuahidi cheo

Anna Tibaijuka: Nashukuru sana mheshimiwa Rais kuniruhusu na mimi nikapumzike. Ninapopumzika, hapa tunaacha ni mahali salama. Kuna mtu mwenye mashaka na baba huyu? Kuna mtu mwenye wasiwasi? (Wananchi: Hamna).

Nyinyi wanangu wa Muleba, walio wengi hapa ni wanangu na wewe mheshimiwa Rais ukiwa mdogo wangu. Hapa Muleba, jirani yetu ni Chato, wembe ni uleule. Wazungu wanasema kama huyu Rais Magufuli ana mshikaji wake, wanasema natural allie ni Muleba Kusini, Muleba kwa ujumla.

Kwa hio kura hapa zitaendelea kuwa za heshima mheshimiwa Rais kama ilivyokuwa 2015. Hapa usiwe na shaka na mimi hapa mstaafu na dada yako, nashukuru sana.
Sasa nimeanza kuelewa maana ya professorial rubbish. Kufurahisha genge.
 
Serikali hii ina mavyeo mengi na ndio maana nimemwambia hata Prof. Tibaijuka, ameniambia hapa, mdogo wangu nimestaafu. Mimi nakwambia hapa, Prof. hujastaafu. Hauwezi tukamuacha Profesa akakaa tu hapa wakati kuna maeneo mengi ya kwenda kufanya.[emoji848][emoji87][emoji30][emoji30][emoji30][emoji30]
 
Jamaa yangu alikuwa kwenye huo mkutano. Anasema ulinzi wa hapo ulikuwa mkali mno. Mkutanoni watu walikuwa wanasema "Mshaija yaija kutubia" maana yake Mwanaume kaja kutudanganya 😂.
 
Tunamsubiri Bukoba Mjini tumpige spana na sijui atajikomba komba nini kwa yale aliyotufanyia 2016 baada ya tetemeko
 
Hao Ndio wapiga kura wenu? View attachment 1570403
IMG_20200915_123640.jpg
 
Magufuli kipenzi cha watanzania, wewe na chuki zako katafute malimao mapema maana hits amini yatakayotokea Oct 28. JPM tano tena, Tanzania ya kijani.
Kwanini hautaki Mh Jiwe kuwaeleza wana kagera aliko peleka hela za rambirambi?
 
Mkoa wa Kagera huyu mzee anakwenda kupoteza muda wake tu, hawajasahau kauli zake za hovyo wakati wa tetemeko.

Ni vizuri akitumia mkutano huu kuwaeleza rambirambi zao za tetemeko zimekwenda wapi?
lami Muleba- Kanyambogo...na sasa Kanyambogo- Nshamba!......
Rambirambi zilijenga shule Ihungo, zahanati, vituo vya afya pamoja nai vifaa tiba au wewe ulitaka zifanye nini Kamanda?
 
Serikali hii ina mavyeo mengi na ndio maana nimemwambia hata Prof. Tibaijuka, ameniambia hapa, mdogo wangu nimestaafu. Mimi nakwambia hapa, Prof. hujastaafu. Hauwezi tukamuacha Profesa akakaa tu hapa wakati kuna maeneo mengi ya kwenda kufanya.[emoji848][emoji87][emoji30][emoji30][emoji30][emoji30]

Hivi kwenye kampeni ahadi kama hizi zinaruhusiwa?!
 
Back
Top Bottom