Uchaguzi 2020 Dkt. Magufuli: Natamani kufika kila eneo kufanya kampeni lakini siwezi

Uchaguzi 2020 Dkt. Magufuli: Natamani kufika kila eneo kufanya kampeni lakini siwezi

Atamtuma Gambo! 😀

Khaa watanzania wapole usoni aisee! Wanakuchekea huku wanakumaliza.

Yaani mheshimiwa aliaminishwa zile comedy, zenye slogan, za tunaishukuru serikali ya awamu ya 5, chini ya Dr.
Bashite alimpoteza sana jamaa...Na zile bongo movie zake!

Everyday is Saturday................................😎
Bashite ndie alie mhalibia mzee kwa ushauri mbovu usio na tija walizani kinunua wapinzani ndio suluhisho eti tukimchukua flani kwa sababu kule anakubalika bas na wananchi wote ni wetu in bashite voice
 
12 Mar 2
WanaCCM walilia Magufuli aende Mtwara na Lindi

Spika wa baraza la wawakilishi Zanzibar, Zubery Ally Maulid amesema kuna haja ya Rais wa Dk John Pombe Mgufuli kutembelea mikoa ya Lindi na Mtwara ili kusikia kilio cha wakulima juu ya kutolipwa fedha zao za korosho.

Korosho ni siasa huku kusini vigogo wa CCM walaumu watendaji serikalini kuficha ukweli pia hata wadai kundi la waandishi wa habari wanaoandamana na viongozi hao wa CCM ktk ziara mwisho wa siku taarifa za korosho hawazioni katika magazeti, radio wala TV jioni hivyo wanashangaa kwanini taarifa za korosho zimekuwa mwiko kuripotiwa na vyombo vya habari, labda kuna ajenda wasiyoifahamu...

'UPO UMUHIMU RAIS MAGUFULI KUTEMBELEA LINDI, MTWARA' - SPIKA MAULID​

 
Mzee: Hali ni mbaya kwakweli kwa nilichowafanyia watu wa kusini siwezi kwenda huko nimeona nimtume waziri mkuu akasaidie kuokoa jahazi

Campaign manager : sasa mzee ujue watu hawatakuelewa kabisa usipotokea hata kidogo

Mzee: Wewe hujui kitu wale wazee wakule wamenipania sana kuna siku walinitumia moshi nusura waniuwe, ngoja nizuge zuge hapa dar mpaka siku ziishe.
 
Akihutubia jimbo la Kawe, Rais Magufuli amesema yeye ni Binadamu hataweza kwenda lindi na Mtwara hivyo atamtuma Kassim Majaliwa Kassim

Mimi kama mwana ccm naunga mkono kumtumia Mama Salma Kikwete na Jakaya Kikwete mikoa ya lindi na Mtwara na tayari hilo limefanyika

Kwa uamuzi huu Rais ameona mbali sana na hongera kwake sana sana,

Wale wa maeneo ya Ngende,Nanjilinji na Nkanared na wale wanaotamka mwana Nke badala ya Mwanamke na mnaotamka Ntoto badala ya mtoto wa mikoa ya lindi na Mtwara tunawategemea sana kupiga kura ya ndio kwa JPM

Kazi za serikali ni nyingi zinahitaji muda pia.

----
Nilipenda sana kupita maeneo mbalimbali. Nilipenda nifike Mbagala; nitamtuma Mheshimiwa Jakaya Kikwete. Nilipanga niende mpaka Ukonga mwisho, napo nitamtuma Mh. Jakaya Kikwete na viongozi wengine.

Nilipanga kupita kila eneo, lakini mimi ni binadamu. Ningependa hata nifike Katavi na Rukwa lakini ilibidi nimtume Makamu wangu wa Rais, Mama Samia.

Ningependa nifike Mtwara na Lindi lkini nitamtuma kule Waziri Mkuu wangu, Ndugu Kassim Majaliwa.

Ningependa nifike Morogoro; ningependa nifike Pwani; ningependa nifike Pemba na maeneo mengine. Mimi ni binadamu, siwezi kuwa kila mahali na wakati huohuo nifanye kazi za serikali. Kwasababu serikali lazima iendelee kwenda, wafanyakazi wapate mishahara yao. Madawa lazima yapatikane hospitali. Na mengine mengi. Wakulima lazima wapate pembejeo. Hatya yote unayasimamia wakati ukifanya kampeni.
Rais ni binadamu anachoka pia anamajukumu ya serikali hawezi kwenda huko kote...hongera Sana Magufuli hujawa mlafi umeamua kuwatuma watu wengine wakusaidie baadhi ya majukumu.. wewe ni Rais unaethamin vipaumbele na kipaumbele chako ni wananchi wako.. CCM oyeee..
 
Bashite ndie alie mhalibia mzee kwa ushauri mbovu usio na tija walizani kinunua wapinzani ndio suluhisho eti tukimchukua flani kwa sababu kule anakubalika bas na wananchi wote ni wetu in bashite voice
Mbona watanzania wengi walihama na Samatta kule Aston villa.....? [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Anaogopa atakosa la kusema kuhusu bei ya korosho kwa sasa kwavile huu ndo wakati mwafaka wa msimu wa mauzo na wananchi wa mikoa hiyo wangependa kuona ahadi inayotekelezeka kuanzia sasa na si ahadi. Kiufupi Magufuli hana sera mpya juu ya maslahi kwa zao hilo na watu wakusini.
 
Bernard Membe si lolote si chochote. Hana meno ya Kumung'ata Dk. Magufuli. Namshauri Magufuli aende kusini. Akaweke Maua kwenye kaburi la Mzee Makapa
 
Back
Top Bottom