Uchaguzi 2020 Dkt. Mwinyi: Wajumbe wa Zanzibar waliotupigia kura ni 68 hata kama ni kweli wenzangu walipata 35 basi na mimi nilipata 33

Uchaguzi 2020 Dkt. Mwinyi: Wajumbe wa Zanzibar waliotupigia kura ni 68 hata kama ni kweli wenzangu walipata 35 basi na mimi nilipata 33

Tujiandae saa tatu kamili kutazama mahojiano mahsusi Kati Dr. Hussein Mwinyi(Rais mtarajiwa wa Zanzibar) na Tido Muhando UTv(Channel 108 azam tv)
 
Fuatilia mahojiano mahsusi Kati Dr. Hussein Mwinyi(Rais mtarajiwa wa Zanzibar) na muandishi mahiri sana Tido Muhando UTv(Channel 108 azam tv)

Twende pamoja majibu ya maswali yote tutayapata hapa.

Karibuni sana
 
Dr. Mwinyi anajua kujieleza sana kwa kifupi na kwa kueleweka kabisa.

Anaonekana mtu makini sana kwenye kuzungumza
 
Kwamba mwanaccm kutoka Bukoba anachagua mtu anaeenda kuongoza nchi ya Zanzibar!! shida ni kua unatetea ujinga lakini kibaya zaidi Mh Rais/m.kiti akasema itenguliwe ili wananchi wa Z bar ndo wafanye uchaguzi pekeyao napo utatetea na kusema sawa.
Kwani hawa wazanzibar wanatokea mbinguni? Si wapo kwenye chama na Serikali. Sifa na ubora wao si unajulikana, sasa wanachama wote wakichagua mgombea wao kwa kuzingatia sifa zao kuna shida gani?

Hiki chama kiliungana kikawa chama kimoja, lazima mambo yake yafanyike kwa pamoja. Otherwise labda Afro Shiraz irudi iwe inachagua wagombea wake. Lakini kwasasa utaratibu ndo huo.
 
Mwinyi amesema hata kama ni kweli wenzake hawakupigiwa kura na wajumbe wa bara kitu ambacho hakiamini, bado yeye naye atakuwa amepata kura 33 kutoka Zanzibar.
 
Kwani hawa wazanzibar wanatokea mbinguni? Si wapo kwenye chama na Serikali. Sifa na ubora wao si unajulikana, sasa wanachama wote wakichagua mgombea wao kwa kuzingatia sifa zao kuna shida gani?

Hiki chama kiliungana kikawa chama kimoja, lazima mambo yake yafanyike kwa pamoja. Otherwise labda Afro Shiraz irudi iwe inachagua wagombea wake. Lakini kwasasa utaratibu ndo huo.
Mwinyi ni bonge la rais Zanzibar hawatajutia
 
Mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM Dr Mwinyi amesema wajumbe wa Zanzibar waliowapigia kura walikuwa 68 na siyo 35 kama inavyovumishwa.

Mwinyi amesema hata kama ni kweli wenzake hawakupigiwa kura na wajumbe wa bara kitu ambacho hakiamini, bado yeye naye atakuwa amepata kura 33 kutoka Zanzibar.

Dkt. Mwinyi amewataka watanzania wawe wakweli badala ya kuzusha mambo yasiyo na tija yoyote.

Source Swahili times

Maendeleo hayana vyama!
Asianze tabia ya Trump ya kujisifia na kulalamika hata pasipokuwa na ulazima. Maneno hayo hayakutakiwa kutolewa na yeye.
 
Si vibaya majina ya wajumbe wa Zanzibar yakiwekwa hapa ili tujirodhishe na huo utetezi. Vinginevyo wanaosema ni wajumbe 35, au yeye anayesema 68, wote ni waongo.
Kweli kabisa.
Hoja yako ni ya msingi sana.
Thanks mkuu.
 
Tunayo list yote, ni wajumbe 35 tu waliotoka Zanzibar, kama alipata kura 33 kutoka zanzibar basi hizo vote zilienda zikiwa zipo kwenye ballot box, na akileta ubishi tutaweka list yote.
 
Wanzanzibar muungeni Maalim mchukue nchi yenu tumewachoka huku Bara
 
Nmesoma meseji karbia zote lkn bado sijapata jibu la kwel, wajumbe walikua 68 au 35?. Km walkua 35 kunaulakini mkubwa sn lakini km walkua 68 inaonekana wazanzibar wanamkubali mwinyi.
 
Mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM Dr Mwinyi amesema wajumbe wa Zanzibar waliowapigia kura walikuwa 68 na siyo 35 kama inavyovumishwa.

Mwinyi amesema hata kama ni kweli wenzake hawakupigiwa kura na wajumbe wa bara kitu ambacho hakiamini, bado yeye naye atakuwa amepata kura 33 kutoka Zanzibar.

Dkt. Mwinyi amewataka watanzania wawe wakweli badala ya kuzusha mambo yasiyo na tija yoyote.

Source Swahili times

Maendeleo hayana vyama!
Vijana wa lumumba mmeanza propaganda tena? Wajumbe wa Zanzibar walikua 35 na Bara 129, yeye alijipatia kura zote 129 kutoka bara. Iko hivyo, hata mtoto wangu mdogo hapa amekucheka sana. Unakwama wapi kwenye mahesabu ya kujumlisha na kutoa tu?
 
Ameshafeli kama ameanza mapema kuingia kwenye huu mtego, CCM wanafanya makosa sana kuacha kura za visiwani zipigwe bara na wabara pia..

Kura za Urais Zenji zilipashwa zipigwe na wazenji tena wakiwa kisiwandui pale au bwawani hoteli, kura za wazenji kupigwa dom tena wapiga kura wengi wakiwa wabara ni dhahiri kunathibitisha wazenji hawawezi kujiamulia mambo yao wenyewe na kila kitu lazima kifanywe bara..

Wazanzibar simameni pamoja kuwaonyesha wabara nyie ni wazenji na Rais wenu lazima atoke zenji kwa kura za wazenji..

Rais wa Tanzania ni wa wote kwa maana ya Bara na Zenji hivyo kura lazima zipigwe na wote labda tulete serikali tatu, Zenji rais wao, bara rais wao na Tanganyika rais wake au zenji na bara ziwe na Mawaziri wakuu na Rais awe mmoja, au makamu wa Rais awe Rais wazenji na huku bara kuwe na waziri mkuu tu....
Kayasemea wapi haya.. kishajichnaganya.
 
Dkt Mwinyi anapaswa kuwa makini mno kwa sasa kwa kauli zake, anapaswa kuwa na timu kabambe sana ya kampeni tena yenye kujumuisha watu waliokuwa kambi tofauti naye. Ili pale zitolewapo kauli za mitego kama hizo, wawe ndiyo wa kwanza kuzitolea majibu ya kuzikanusha.

Nyufa zipo kubwa sana kwa upande wa CCM Zanzibar, akumbuke matokeo yaliyompatia yeye ushindi yameaacha si makovu tu mioyoni mwa waliokuwa wajumbe na kambi zao bali vidonda halisi. Matokeo yale yaliliza baadhi ya wajumbe, kwa hiyo kitu muhimu sasa ni kutumia kila njia awezayo ili kuleta maafiakiano na kujenga umoja ndani ya chama chake. Ili kufanya pale anapokwenda kukabiliana na Maalim Seif, awe amejizatiti kweli kweli.
Uliyosema ni kweli kabisa nilimuona Nahodha tangu siku ya uchaguzi amenuna mpaka leo hajacheka kati ya wagombea wote huyu ameumia kweli. Lakini napenda kumfahamisha kwamba duniani hakuna haki akitaka haki basi ataikuta mbinguni akubali yaishe na maisha yaendelee.
 
Uliyosema ni kweli kabisa nilimuona Nahodha tangu siku ya uchaguzi amenuna mpaka leo hajacheka kati ya wagombea wote huyu ameumia kweli. Lakini napenda kumfahamisha kwamba duniani hakuna haki akitaka haki basi ataikuta mbinguni akubali yaishe na maisha yaendelee.
Hata kujieleza alishindwa maskini!!
 
Wakati wa mahojiano ya jana au juzi anaonekana kutaka kuonesha kuwa yeye alisimama yeye mwenyewe na wala sio kwa kubebwa na baba yake lakini pia na suala la kura alizopata. Naona namna alivyojibu kwa kweli ni aibu tu kwani inaonesha uwezo wake wa kupambanua mambo ni mdogo nikilinganisha pengine na baba yake alivyokuwa.

WaTanzania wote tunajua kuwa Mzee Mwinyi alikuwa mtu wa watu na anapendeka mpaka sasa. WaTanzania pia wanatamani kuwa na kiongozi kama alivyokuwa Mwinyi kwa baadhi ya mambo aliyoyasimamia - mfano kuwapa nafasi na uhuru zaidi - yaani "ruhusa". Kuna tunaoamini Hussein Mwinyi paia anaweza akawa kama alivyokuwa Mzee Mwinyi na tungependa awe hivyo.

Kwa maana hiyo tunavyomwona yeye vile alivyo ni kama tunakumbushwa mema ya Mzee Mwinyi yamerithiwa na Hussein Mwinyi huyu. Sasa anavyokataa kujilinganisha naye hata kidogo tu sidhani kama anapatia sana. Kwani ni dhambi mtu kusema baba yake kwa namna moja au ingine - direct or indirectly - anaweza akawa amechangia yeye kupigiwa kura?. Kwani ni lazima Hussein Mwinyi ajue kuwa baba yake alimpigia debe? Sidhani kama Mzee Mwinyi ilitokea hakumwombea kura kwa mtu hata mmoja mwanae Hussein.

Kuna lile suala la kura 35 pia. Nafikiri Hussein alivyoanza kufafanua kwa kuweka assumptions ya kura zile zilivyopigwa alikuwa anakosea sana! Yeye alivyoulizwa na Tindo angesema tu kuwa sio kweli waliopiga kura zile ni WaZanzibari 35 tu. Alitakiwa tu ajibu kuwa waliopiga kura walikuwa 64 na sio 35 kama watu tunavyotaka kuaminishwa!

Hussein Mwinyi we ni Raisi Mtarajiwa jitahidi sasa kuwa Mwanasiasa makini sio kila swali kulijibu kivileeeeeeeee! Ukiendelea kufanya hivyo hakika kuna mambo utaibua na utasababisha upinzani ukugalagaze huko Visiwani!
 
Back
Top Bottom