Uchaguzi 2020 Dkt. Mwinyi: Wajumbe wa Zanzibar waliotupigia kura ni 68 hata kama ni kweli wenzangu walipata 35 basi na mimi nilipata 33

Uchaguzi 2020 Dkt. Mwinyi: Wajumbe wa Zanzibar waliotupigia kura ni 68 hata kama ni kweli wenzangu walipata 35 basi na mimi nilipata 33

Ataweweseka sn mpaka amwambie baba yake awaombe msamaha watz kwa kauli yake ile ya kipumbavu.....hizi ndo tabia Mwal alikua anazikemea na kuziita tabia za kimalayamalaya......
Wazanzibari hawamtaki kabisa mwinyi na kwa pamoja kura zote watampa MAALIM SEIF
Unaweza kuweka takwimu ni kwa vipi wa zanzibar hawamtaki Mwinyi?

Mlishazusha eti hajapigiwa kura na wajumbe wa zanzibar?

Kura 68, yeye kapata 33 wenzie wamegawana 35.
Ina maana hata wangepiga wanzanzibar pekee angeshinda tofauti na mnavyizusha!

Mwambieni Seif kipigo kipo pale pale na hivi ni mzee.
 
Kua mbunge miaka zaidi ya 10 , sijui waziri sijui nn.. hakumfanyi mtu awe na uwezo wa kupambanua mambo.

Kuna watu ukiwasikiliza tu unajua hamna kitu unazima na TV

Kuna mtu ukimsikikiza tu unajikuta umekesha kwa kumsikiliza.
Hapana ila tatizo linalo kusumbua ni hizo chuki binafsi zako.
 
Hujui madhara ya majibu yake! Kwani unafikiri waliozua kuwa wapiga kura wa Zanzibari walikuwa 35 unafikiri walikuwa hawajui?
Madhara yake ni yapi? Si kajibu kuondoa sintofahamu wanayozusha wazushi? Sasa shida iko wapi?

Yeye kasema wagimbea walikuwa 3, wapiga kura walikuwa 68 wenzie wamepata kura 35 yeye 33. Sasa hatari yake iko wapi hapo? Au mnajaribu kutengeneza picha kwamba kuna hatari?

Au ulitaka angepata kura zote wakati ule ulikuwa ni uchaguzi wenye washindani 3?
 
Unaweza kuweka takwimu ni kwa vipi wa zanzibar hawamtaki Mwinyi?

Mlishazusha eti hajapigiwa kura na wajumbe wa zanzibar?

Kura 68, yeye kapata 33 wenzie wamegawana 35.
Ina maana hata wangepiga wanzanzibar pekee angeshinda tofauti na mnavyizusha!

Mwambieni Seif kipigo kipo pale pale na hivi ni mzee.
Kizazi hiki kinataka ushahidi!!!!!....Uchaguzi ukiwa huru na haki mwinyi hawezi kua rais wa zanzibar, hizo za mwinyi zimeibiwa tu ndio maana wazanzibari wote walitoka kwenye kikao wanalia.....
Zamani ccm ilikua na wenyewe lkn siku hizi ccm ina mwenyewe anayeamua kila kitu. Haya mambo ya ndani huwezi kuyajua ww endelea kulamba makalio tu utapata cheo
 
Nyie wengine labda wakati wa Mwinyi hamkuwepo au mlikuwa watoto, Mzee mwinyi pia alikuwa anaongea na kufanya matakataka mengi sana!

Misingi ya nchi hii alianza kuibomoa Mwinyi, ndio maana Mwl akawa anasimama mara kwa mara kumweka sawa.

Hivyo msitegemee akili za kurithi toka kwa mwanae!
 
Wakati wa mahojiano ya jana au juzi anaonekana kutaka kuonesha kuwa yeye alisimama yeye mwenyewe na wala sio kwa kubebwa na baba yake lakini pia na suala la kura alizopata. Naona namna alivyojibu kwa kweli ni aibu tu kwani inaonesha uwezo wake wa kupambanua mambo ni mdogo nikilinganisha pengine na baba yake alivyokuwa.

WaTanzania wote tunajua kuwa Mzee Mwinyi alikuwa mtu wa watu na anapendeka mpaka sasa. WaTanzania pia wanatamani kuwa na kiongozi kama alivyokuwa Mwinyi kwa baadhi ya mambo aliyoyasimamia - mfano kuwapa nafasi na uhuru zaidi - yaani "ruhusa". Kuna tunaoamini Hussein Mwinyi paia anaweza akawa kama alivyokuwa Mzee Mwinyi na tungependa awe hivyo.

Kwa maana hiyo tunavyomwona yeye vile alivyo ni kama tunakumbushwa mema ya Mzee Mwinyi yamerithiwa na Hussein Mwinyi huyu. Sasa anavyokataa kujilinganisha naye hata kidogo tu sidhani kama anapatia sana. Kwani ni dhambi mtu kusema baba yake kwa namna moja au ingine - direct or indirectly - anaweza akawa amechangia yeye kupigiwa kura?. Kwani ni lazima Hussein Mwinyi ajue kuwa baba yake alimpigia debe? Sidhani kama Mzee Mwinyi ilitokea hakumwombea kura kwa mtu hata mmoja mwanae Hussein.

Kuna lile suala la kura 35 pia. Nafikiri Hussein alivyoanza kufafanua kwa kuweka assumptions ya kura zile zilivyopigwa alikuwa anakosea sana! Yeye alivyoulizwa na Tindo angesema tu kuwa sio kweli waliopiga kura zile ni WaZanzibari 35 tu. Alitakiwa tu ajibu kuwa waliopiga kura walikuwa 64 na sio 35 kama watu tunavyotaka kuaminishwa!

Hussein Mwinyi we ni Raisi Mtarajiwa jitahidi sasa kuwa Mwanasiasa makini sio kila swali kulijibu kivileeeeeeeee! Ukiendelea kufanya hivyo hakika kuna mambo utaibua na utasababisha upinzani ukugalagaze huko Visiwani!


=========

Hussein Mwinyi amesema kuwa yupo tayari kutoa ufafanuzi kwa yale yote yaliyokuwa yanasemwa na alikataa kuongea kabla ya uchaguzi kwa kuwa huenda kauli yake ingetafsiriwa tofauti.

Mahojiano yao yalikuwa:

Swali, Katika hatua mbalimbali za mchakato ambao umemfikisha hapo alipofikia ni hatua gani ilikuwa inamtia wasiwasi ambayo alikuwa anadhani akiivuka mambo yake yatakuwa mazuri.

Jibu, Katika utaratibu wa chama kutoka kwa wale wote waliochukua fomu huchujwa na kupata watano, na kutoka watano kwenda tatu bora, hatua zote ni ngumu na hazitabiriki kuwa kuna moja ni rahisi zaidi ya nyingine bali zinataka kuwa makini na yeye alikuwa anasubiri baada ya hatua hizo nani atashinda na anashukuru alifanikiwa kushinda.

Swali Unadhani katika mchakato huo kuna watu ambao ulikuwa unahofia kuwa iwapo wataingia huenda mpambano utakuwa mzito zaidi huenda wana ushawishi zaidi Zanzibar au vipi au nao waliingia katika hao watu 32 ?.

Jibu Katika uchaguzi huwezi umdharau mtu yoyote na aliona katika wote waliochukua fomu wana nafasi ya kushindahususani wale waliokuwa katika serikali au chama walikuwa na nafasi kama ambavyo alikuwa nayo yeye.

Swali Kwenye hotuba yako ulisema kuwa mtihani wa kutafuta nafasi ya kuwania urais ulisema ulikuwa mgumu, wewe ni daktari na mitihani ya madaktari kwa kawaida huwa ni migumu zaidi lakini umesema huu wa kuwania urais wa Zanzizibar ulikuwa mgumu zaidi ?.

Jibu Mtihani ulikuwa mgumu kuliko yote kwakuwa haukuwa mwepesi na hautabiriki kwa hiyo mpaka kuumaliza kwa ushindi anamshukuru Mungu.

Swali Sasa Dr.Hussein Tayari yameshabaki majina matano na tayari mmeshafika Dodoma ulijisikiaje kufika katika hatua hii? Lakini je,uliona mtihani ulizidi kuwa mgumu zaidi kwakuwa miongoni mwa wale watano yoyote anaweza kuchaguliwa?

Jibu Kutoka kwenye watu wote mpaka kufika watano maamuzi hayo yalifanywa na kamati kuu Zanzibar na unaweza kusema kuwa wale ambao hawakuwa na nguvu sana walikuwa wameshatoka na kubaki wale ambao walikuwa na nguvu zaidi kuliko wengine hivy mtihani ulizidi kuwa mgumu zaidi.

Swali Je, ulipofika Dodoma ulikuwa tayari una tetesi ya kuwa nani unakutana nao kwenye kinyang'anyiro hicho au mpaka unafika Dodoma hukua unajua chochote.

Jibu Kwakweli taarifa zilitoka kwenye mitandao ila hawakuwa na uthibishi ila yeye aliamini hivyo hivyo walipofika Dodoma walikuwa wanasubiri kuthibisha kama ni hivyo.

Swali Sasa baada ya hapo mkabaki watatu na wenzako wawili walikuwa na hali ya kufahamika zaidi, wao wana shughuli zao Zanzibar hivyo kufahamika zaidi japo na wewe unafahamika ila ni maneno yalikuwa yanesemwa.

Jibu Yeye hakuliona katika mtazamo huo alikuwa anaona ni maneno ya watu ambao hawakuwa upande wake kwa sabau yeye amekuwa mbunge wa Kwahani kwa miaka 15 na miaka hiyo ni mingi na alikuwa anajiona ni mmoja ya watu wanaofahamika zaidi Zanzibar hivyo kusema alikuwa hafamiki haikuwa sahihi.

Swali Kwa mshangao wa wengi na sijui kwa upande wako wewe ulilichukuliaje suala la Mh. Rais na mwenyekiti wa chama kusema kikao cha halmashauri kuu kitakuwa cha wazi hata kwenye "television" kioneshwe, ulifurahia uamzi huo au ulipata mshangao na kuona suala hilo hakutakuwa na cha siri tena?

Jibu Kwa kweli nichukue fursa hii kumshuru rais kwa kuwa kila mmoja aliondoka pale akiwa ameridhika na kuona kulikuwa na haki hakuna kuibiwa wala kuonewa.

Swali Baada ya kuitwa kwenda kushikwa kurazenu na kuona wewe unakuwa na rundo kubwa la kura ulijisikiaje kuona kuwa unaelekea kushinda?

Jibu,kwa kweli nilijisikia vizuri sana kwa kuwa kila mgombea ana mategemeo ya kushinda na nilimshukuru Mungu kwa kuwa niliona naelekea kushinda.

Swali kuna maneno yanasemwa kuwa nafasi yako umeipata kwa msaada wa wajumbe kutoka Tanzania bara na sio kutoka wajumbe wa Zanzibar.

Jibu Ni maneno potofu ila ukweli utabaki palepale na ni ukweli wa kitakwimu kuwa, wajumbe wanaopiga kura ni 68 na ukichukuwa kura za wenzangu ambo jumla 35 na hivyo 33 zilipiga kwangu na mimi nimepata karibu nusu ya kura na hivyo mimi nimepata karibu nusu ya kura za Zanzibar.

Swali Maneno kama haya ya watu wanapiga kwenye mitandao yanakupa tabu gani hasa wakati huu unapoelekea kwenye kampeni.

Jibu Hazinipi changamoto yoyote kwa kuwa maneno ya sikupata kura za watu wa Zanzibar sio kweli.

Swali Je, wazanzibari wategemee utabadilika na kuwa mkali kama Rais Magufuli maana unaonekana ni mtu mpole na mtaratibu kiasi.

Jibu Sio rahisi kunielewa vizuri kwa kuwa sikuwa na wizara ambayo nilikuwa naonekana ila nimejifunza kutoka kwa watangulizi wangu kama JK Kikwete na Rais Magufuli ukali wake wa kupinga ubadhilifu na rushwa nimejifunza na nitapenda kuwa kama yeye katika kuhakikisha ubadhilifu, rushwa havipati nafasi.

Swali Inasemekana wewe ni kweli umezaliwa na wazazi ambao ni wazanzibari ila hukuzaliwa Zanzibar na hukukulia wala kusoma Zanzibar hivyo huna ukaribu zaidi Na Zanzibar kuliko sehemu nyingine za Tanzania bara.

Jibu Mimi nimezaliwa Zanzibar japo sikusoma Zanziba ila hii hainiondolei sifa ya kugombea nafasi ya kuwa Rais wa Zanzibar.

Swali Wengine wanakwenda mbali zaidi kwakusema kuwa nguzo yako kubwa ni kuwa wewe ni mtoto wa rais mstaafu na hiyo ndio nguzo yako kubwa katika kuwania nafasi hii.

Jibu Yeye ni daktari na ana uzoefu katika serikali kwa muda mrefu na haina mahusiano yoyote na nafasi ya uongozi uliopita wa mzazi wake.

Swali unajisikiaje kupambana na mtu ambae ameshakuwa na uzoefu Maalim Self Hamad hii ni mara ya sita na tayari ameshakuwa na uzoefu.

Jibu Uchaguzi ni kampeni na sera wananchi watachagua sera nzuri na pia wananchi wengi ni vijana na watapenda damu changa na sera nzuri na hii kwao ni faida.

Swali Ni kipi unaweza kuiga kutoka kwa mzazi wako ambae ni rais mstaafu, ambae alikalia kiti ambacho wewe nawe unataka kwenda kukalia.

Jibu Mimi sijawahi kufanya kazi na Mzee Mwinyi ila kwenye historia kuna mambo mazuri ambayo ameyafanya kama kuruhusu biashara za aina zote zifanyike na mimi naweza fanya hivyo ila kwa utaratibu wa sasa.

Swali Katika kipindi cha hivi karibuni uchumi wa Zanzibar umekuwa ukiendeshwa na utalii ila sio biasharaya kutemgea sana kama kipindi hiki kuna corona na zao la karafuu limezorota, wewe unajipanga vipi kuleta maendeleo Zanzibar.

JibuUchumi wa visiwa unafanana na Zanzibar lazima iige mbinu za Visiwa vinavyofanya vizuri badala ya kutegemea watalii lakini pia kuendeleza bandari na uvuvi ili kuongeza pato kwa ujumla na yapo ambayo tutaboresha ili kuongeza kipato zaidi.

SwaliKwenye utalii kumekuwa na kelel kwamba Si kwakiasi kikubwa Zanzibar imekuwa ikifaidi na hivyo wageni kufaidi zaidi una mpango gani ili kiasi kikubwa cha mapato kiifaidishe zaidi Zanzibar ?

Jibu Biashara au shughuli yoyote inayofanyika Zanzibar ni lazima iwafaidishe wananchi hivyo ni vyema kuangalia upaya sera na kuona jinsi ya kufanya wananchi wa Zanzibar waweze kupata mafufaa, lakini pia Kodi sera za kodi kwa kiwango gani tunapata manufaa na kuboresha ili kuleta mafuaa.

Swali Hakuna shaka kama utapata nafasi basi muungano utakuwa katika mikono salama lakini pia umejipangaje kuhusu malalamiko au kero za muungano kama wanavyoziita ili yasiwepo

Jibu Ni kweli lakini si kero bali ni changamoto ila tutaangalia jinsi ya kuyatua yale machache ambayo bado yapo ili kila mmoja apate manufaa ya muungano huu.

Swali Ni nini kauli mbiu au ahadi yako kwa wazanzibari na kuwaonesh akuwa wewe ndie unaefaa kuchukua kijiti cha nafasi ya rais ajaye.

Jibu Dhamira yangu ni njema nia yangu ni kuweza kuongeza kipato cha Mzanzibari na kufanya kazi kwa maslahi ya Mzanzibari na kusimamia serikali nitakayoiunda ili kuongeza kipato na kuboresha huduma za kijamii Zanzibar.

Swali Mwishi kabisa unawaambia nini au una ushauri gani kwa Wazanzibari

Jibu Nawaambia kuwa tunakwenda kwenye uchaguzi na vyama vingine na mimi nawaambia wana CCM na Wazanzibar kuwa tudumishe amani tuliyonayo atakaeshindwa akubali matokeo na sisi tunaimani kama tutashinda na atakaeshinda akfanye kazi kwa nguvu sana ili kuleta maendeleo Zanzibar.

Jamani mwachieni Rais kijana.
Wembe ameutaka mwenyewe, msichagulie namna ya kunyoa!
 
Wazanzibari wanasema haya, Zanzibar kwanza mengine yatafata baadae, hata utoe ahadi mia 100 kama hakuna Zanzibar kwanza wananchi watakwambia no.

Mifano ipo halisi bila ya kuwa na Zanzibar yenye mamlaka kamili.

Kwanza Zanzibar haiwezi kunufaika na rasilimali zake za ndani kama utalii, visa za wageni wote , fedha zinaenda Tanganyika

Pili mikopo, Zanzibar haiwezi kukopa nje wala haiwezi kupata misaada moja kwa moja ya kifedha bila ya kupitia serikali kuu Tanganyika kwa kupata kibali au kusainiwa na vile vile fedha za kigeni lazima zipite BOT

Tatu mapato ya muungano ikiwemo misaada, Zanzibar haifadiki hata kidogo kupitia hilo, ndio maana wazanzibari wanataka mamlaka kamili ya Zanzibar.

Michezo, michezo sio jambo la muungano Lkn time ijiitayo ya taifa imeundwa kinyume na katiba ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania, ikachukua mamlaka na kuingia katika socca la kimataifa FIFA , imeikosesha Zanzibar fursa nayo kimichezo, hili kero kubwa la muungano.


Kama huna strategy ya Zanzibar kwanza, kushinda uchaguzi labda kwa bunduki, kwa kura huwezi kushinda , wazanzibari wanajielewa sana na tunajua mahitaji yetu
 
Kizazi hiki kinataka ushahidi!!!!!....Uchaguzi ukiwa huru na haki mwinyi hawezi kua rais wa zanzibar, hizo za mwinyi zimeibiwa tu ndio maana wazanzibari wote walitoka kwenye kikao wanalia.....
Zamani ccm ilikua na wenyewe lkn siku hizi ccm ina mwenyewe anayeamua kila kitu. Haya mambo ya ndani huwezi kuyajua ww endelea kulamba makalio tu utapata cheo
Mpumbavu kweli wewe! Kila kitu kinaenda kwa takwimu siyo kwa hisia za kichadema,!

Kikao kilikuwa live kwa uwazi na kura zilipigwa live alafu unataka kuaminisha watu kwa mind set zako za kuibiwa kwamba hata zile kura za kumchagua mgombea wa zanzibar ziliibiwa?

Hao wazanzibar ndio katika ile kamati nusi yao walimpigia kura Mwinyi katika wagombea wote 3!

Narudia, mwambieni mzee Seif ajiandae kisaikolojia.
 
Mpumbavu kweli wewe! Kila kitu kinaenda kwa takwimu siyo kwa hisia za kichadema,!

Kikao kilikuwa live kwa uwazi na kura zilipigwa live alafu unataka kuaminisha watu kwa mind set zako za kuibiwa kwamba hata zile kura za kumchagua mgombea wa zanzibar ziliibiwa?

Hao wazanzibar ndio katika ile kamati nusi yao walimpigia kura Mwinyi katika wagombea wote 3!

Narudia, mwambieni mzee Seif ajiandae kisaikolojia.
Patachimbika Zanzibari mwaka huu!
 
Nyie wengine labda wakati wa Mwinyi hamkuwepo au mlikuwa watoto, Mzee mwinyi pia alikuwa anaongea na kufanya matakataka mengi sana!

Misingi ya nchi hii alianza kuibomoa Mwinyi, ndio maana Mwl akawa anasimama mara kwa mara kumweka sawa.

Hivyo msitegemee akili za kurithi toka kwa mwanae!
Mzee Mwinyi ni mtupu mpaka kesho.

Na alidhihirisha hilo alipoanza kusema Magufuli aongezewe miaka mitano baada ya 2025, katiba ibadilishwe mara moja kwa ajili ya Magufuli, halafu akipita urudishwe ukomo wa urais wa miaka 10.

Hiyu ndiye mtu aliyepigiwa kelele sana na Nyerere kuhusu umuhimu wa kuheshimu katiba.

Sasa sijui hakuelewa somo au amedharau tu.
 
Kauli hiyo di lazima iwe ya mtu ambaye hawezi kuchangia mada.

Inaweza kuwa.

1. Mtu anachangia mada kwa kuunga mkono, kwa kuanzia walivyosema waliomtangulia na kuchangia yake.

2. Ku build consensus.

3. Hata kupandikiza yake kijanja kwa kutumia muhuri wa "waliomtangulia".

4. Kuji align na authority.

5. Kufupisha maneno adirudie yaliyokwishasemwa ajazie zaidi tu.

Acceptance speech ya Mwinyi haikuwa mbaya. In fact kwa zama hizi za Magufuli ni kazi ngumu sana kutoa speech mbaya zaidi ya za Magufuli.

Mimi tatizo langu kwa Mwinyi ni utendaji zaidi.

Sijaona lolote alilolifanya. Amekuwa kama wallflower aliyekaa akisubiri promotion tu.

Na scandals kibao, ikiwamo ya milipuko ya mabomu, tena mara mbili (2009 Mbagala na 2014 Gongo la Mboto), si mara moja, zilitakiwa zimfanye ajiuzulu.
Kamkoa cha Zenji kama mtosha, kataendeshwa kwa rimoti kutokea Chamwino
 
wengine sio lazima wajielezee ndio uelewe wana uelewa mkubwa.kujieleza ni karama kama ikrama nyingine huenda ukawa una utendaj kazi mkubwa na wa ajabu ila kujieleza kidogo inakua sio sana.nabii musa alikua na kigugumizi ila aliwakoa wana wa israel
 
Hakika inatia hamasa maelfu ya wananchi wajitokeza kumlaki Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi(CCM) Dr Hussein Mwinyi.
 
Back
Top Bottom