ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 66,537
- 75,687
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Nyie mpo kwenye dunia yenu na mengi alizungumza mhariri ni miradi ya Magufuli. Nitafutue picha ya Zahanati au kituo Cha afya mtaani kwako Leo inayojengwa alafu piga picha itume.-Kikokotoo dhalimu ndio aliasisi ,hata hivyo mama ni msikivu Serikali imesema meimosi majibu yatatoka
-Mfumuko upi wa bei wakati takwimu zote haijawahi zidi 4%? Pili kama Kuna mfumuko wa bei ingeathiri uwekezaji na Mapato ya Serikali lakini yameongezeka mara dufu.
-Bima ya Afya imefanya nini? Sana sana Mama ameleta sheria ya bima ya Afya Kwa wote na kuweka historia , utekelezwaji wake ni WA hatua Kwa hatua ila kabla ya 2028 Kila mtu atatibiwa Kwa bima.
-Ingia TIC utaona maelfu ya biashara yaliyoanzishwa na ndio chachu ya kuongezeka Kwa Mapato ya Serikali.
-Unazungumzia Ajira Kwa Samia? Hilo sio swali ni jibu,zingine hizi hapa 👇View attachment 2968972
Wahisani wamefanya nini?Swala hili si la mama, ni la Waisani na mashirika ya kimataifa. Umeme umefika vijiji vingapi vipya? Bei ya umeme, TOZO? Gharama za maisha, gharama ya internet, uhuru wa habari? Democrasia vipi?
Ukilala usiku hua unaota kweli au ni fuvu lisilo na wire kichwani?Samia akifanya kosa moja litashikiwa bango kulinganisha na mema mia anayoendelea kuyafanya. Sababu haswa ni jinsi yake ya kike, wengi wetu tunaishi na mtazamo duni kwamba mwanamke ni dhaifu na hawezi kufanya kitu.
How much AID does Tanzania get kutoka nje? Kwa taarifa Yako more than 30 percent? How does mama Samia anasaidia Wamama wajawazito? Program hizi zimekuwepo kabla yake na magufuli ndio alifungua huo Mlango Kwa kutoa exemption wewe unaongea Nini?Wahisani wamefanya nini?
Ukiwa umejawa na chuki huwezi kuona mengi yanayofanyika kwa sababu hiyo chuki inakutia upofu.Ukilala usiku hua unaota kweli au ni fuvu lisilo na wire kichwani?
Mambo yote yametajwa ni miradi ya Magufuli, miradi Gani yeye katekeleza, kama ni growth in different sector ukiangalia Kwa umakini ni matokeo ya maandalizi makubwa her predecessor amefanya.
DP world naomba nitumie mkataba, Kwa Nini bungee halikpata nakalaUkiwa umejawa na chuki huwezi kuona mengi yanayofanyika kwa sababu hiyo chuki inakutia upofu.
DP World hapo bandarini wamebadilisha kabisa utendaji wa kazi na faida za kiuchumi zinaanza kuonekana, hiyo ni kazi ya Samia.
Tembea huko mikoani uone mfumuko wa viwanda vilivyoanza kufanya kazi baada ya JPM kufariki dunia.
Hayo yameelezwa na KM wa CCM Dkt.John Nchimbi wakati wa ziara yake ya Mikoa 6 akiwa Njombe.
DK Nchimbi ameonekana kushangazwa na kufurahishwa na Wingi wa miradi na maendeleo yaliyofanyika na yanayoendelea kufanyika akisema ni kama miujiza maana kilichotakiwa kufanyika Kwa muda mrefu kimewezekana ndani ya mda mchache kabisa.
Kwa wasio fahamu,haters na wabishi hii hapa ni summary tuu ya kilichofanywa na Samia.👇👇
1-Mapato ya TRA kuongezeka kutoka wastani wa 1.5T Hadi 2.5T(ongezeko Trilioni 1 )
2-Makusanyo ya Halmashauri kuongeza kutoka Bil.800 Hadi Trilioni 1.2(Ongezeko Bil.400)
3-Ongezeko la Mapato ya Utalii Hadi 3.5T(Watalii 1.9m) kutoka 3T(Watalii 1.5mln).
4-Ujenzi wa Bandari Ziwa Nyasa(MbambaBay),Ziwa Tanganyika(Kigoma),Ziwa Victoria (Mwanza,Bukoba,Chato) na Bhari ya Hindi(Dar,Tanga,Kilwa na Mtwara).
5-Ujenzi wa viwanja wa ndege 15 Unaendelea Tanzania nzima eg Sumbawanga,Tabora,Shinyanga,Kigoma,Ruaha NP,Nyerere NP,Moshi,Iringa nk huku akikamilosja viwanja vya Songwe, Songea,Iringa na Katavi.
6-Ujenzi wa Hospital za Wilaya mpya 129 ,Mikoa 7 na Rufaa za Kanda 3(Mtwara,Kigoma na Ukerewe).
7-Ujenzi wa Vituo vya Afya vipya 402 kwenye kata za kimkakati hapo tozo za miamala (234).
8-Ununuzi wa vifaa tiba ambavyo havikuwahi kuwepo Kwenye hospital za Tanzania mfano Ultra Sound 192 ,Digital X-rays 147,CT Scan 32,MRI machines 7.
9-Ujenzi wa majengo ya Wagonjwa Mahututi(ICU) 28 na Dharula 127,
10-Upanuzi na Ujenzi wa Vyuo Vikuu (Taasisi za Elimu ya Juu 23),Mikoa yote Tanzania na Zanzibar ikiwemo Mikoa 14 ambayo awali haikuwa na Vyuo Vikuu au kampasi eg Kigoma,Simiyu,Njombe,Ruvuma, Rukwa,Katavi,Shinyanga,Lindi,Mtwara nk.
11-Kaongeza Bajeti Kila Wizara ila Kwa upekee ni Wizara ya Kilimo(Umwagiliaji )kutoka Bil.270 Hadi Bilioni 950.Skimu Mpya za uwamwagiliaji hectare 95,000 zimejengwa na kufufuliwa,kafungua ofisi za Kilimo Kila Wilaya na kaajiri Wataalamu na kawapa vitendea kazi.
12-Kaondoa shida ya vitambulisho NIDA,zaidi ya vitambulisho 12,000,000 vimegawiwa.
13-Ujenzi wa minara mipya 1,200 ambapo Kupitia mradi wa Tanzania ya Kidijitali minara 728 inaendelea na Ujenzi Kwa Bilioni 126.(Kijijini kama mjini)
14-Amefikisha maji ya Bomba Kwa zaidi ya Vijiji 11,000.(Kampeni ya kumtua Mama ndio kichwani) Vyenhe miradi takribani 1,000 na kunufaisha zaidi ya watu Milioni 5.
15-Amefikisha umeme Kila Kijiji,kazi inaendelea kwenye vitongoji na migodi ya umeme.
16-Amewasha Umeme gridi ya Taifa Mikoa Kigoma,Katavi na kazi zinaendelea Rukwa ,Lindi, Mtwara.
17-Kazi zinaendelea ujenzi wa Vyanzo vipya vya Umeme eg Mto Malagalasi,Kakono,Umeme Jua Kishapu,Joto Ardhi Mbeya nk
18-Amejenga zaidi ya Shule Mpya za Sekondari 3,200 ,shule za msingi zaidi ya 300 na madarasa 24,000 ,mabweni 137 nk
19-Kupitia TanRoads amekamilisha zaidi ya km 1,000 za lami na zingine zaidi ya 3,700 zinaendelea na Ujenzi.
20-Kupitia Tarura amejenga zaidi ya km 800 za lami na zingine zaidi ya 500 zinaendelea na Ujenzi (Hapa amefungua maelfu ya Vijijini Kwa Barabara Mpya za changarawe na madaraja). Bajeti ya Tarura aliongeza kutoka bil.270 Hadi Bil.800.
21-Sekta ya mifugo amegawa Boti za Kisiasa zaidi ya 200 na viximba zaidi ya 1300 Kwa Vijana.
22-Sekta ya Elimu kaongeza mikopo Kwa wanafunzi ambapo Sasa Diploma Hadi Chuo Kikuu wanapata,chekechea Hadi form six Elimu Bure(kafuta ada ya form Six),Kafuta Mapenato na mambo ya hivyo ya Bodi ya Mikopo.
23-Katoa Ajira zaidi ya 55,000 kada zote huku Elimu na Afya wakipewa kipaombele.
24-Anajenga na kukamilisha zaidi ya miradi ya maji 3,700 mikubwa Kwa midogo mfano mradi wa Miji 28,bwawa la kidunda na kukwamua miradi iliyokwamba kama same-mwanga,Tarime-Kiabakari nk.
25-Kwenge sekta ya biashara baada ya maboresho maelfu ya miradi imemenika Kila sekta baada ya Wafanyabiashara kurejesha Imani Kwa Serikali Kupitia sera ya Diplomasia ya Uchumi na kuifungua Nchi.Hakuna ziara ambayo mama alifanya Nje ya Nchi hajakutana na Wafanyabiashara wa Kimataifa.
26-Sekta ya michezo na Burudani.Huko Kila mtu anajua kwamba Mama alikatabati viwanja,akaleta ufunguzi wa AFL na sasa ameileta Afcon 27 na uwanja Mpya inajengwa Arusha.Likewise kuwapa mikopo Wasanii.
27-Ujenzi wa Vyuo vya Ufundi Stadi (VETA) 100 .Lengo Kila Wilaya na Mkoa iwe na Chuo Cha ufundi.
28-Kaongeza Boom Kutoka 8,500 Hadi 10,000
29-Amefufua sekta ya Nyumba ilivyokuwa imekufa
30-Amefungua Uchumi,Watalii na Biashara Vinamiminika mfano ni kuzinduliwa Kwa viwanda vya Vioo,magari na mbolea.
31.Ujenzi wa Daraja la Jangwani
Ujenzi wa TPA Dar Port Tank Farm ,Bilioni 679.
Kiufupi ni vigumu kuelezea vyote,pamoja na Changamoto ila Mama kaupiga mwingi ,Anatosha na Chenji inabakia.
View: https://www.instagram.com/p/C59CY7uMJC5/?igsh=MTNiYnozM2hubjMwZQ==
My Take
Yote hayo kafanya na anaendelea kufanya lakini hajawahi acha mradi hata 1 aliourithi kutoka Kwa Mwendazake kama Bwawa la JNHPP,Daraja la JPM,EACOP,SGR,Ndege Mpya,Ujenzi wa Mji wa Serikali na hajatoa visingizio.👇👇
View: https://youtu.be/wLGSs8-pCcU?si=6t-U9ZR8BOp4PEIh