Dkt. Ritta Kabati Kutoa Bima za Afya kwa Watoto wenye Mahitaji Maalum Mkoa wa Iringa

Dkt. Ritta Kabati Kutoa Bima za Afya kwa Watoto wenye Mahitaji Maalum Mkoa wa Iringa

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

MBUNGE MHE. DKT. RITTA KABATI KUTOA BIMA ZA AFYA KWA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM MKOA WA IRINGA
MBUNGE VITI MAALUM MKOA WA IRINGA (CCM), Mwenyekiti wa Wabunge wa CCM Iringa, Mjumbe Bodi ya Wasanii COSOTA na Balozi wa Walemavu Bungeni Mhe. Dkt. Ritta Kabati ameahidi kutoa msaada wa jumla ya kadi za bima ya afya kwa watoto wenye mahitaji maalum 150 wa mkoa wa Iringa ili kupunguza gharama za matibabu wa watoto hao.

Kabati ameyasema hayo wakati wa hafla ya kukabidhi kadi za bima ya afya 172 zilizotolewa na taasisi ya Rounding Hands kwa kushirikiana na Online Tv ya Makutano ambapo hafla hiyo ilifanyika katika viwanja vya taasisi ya Nyumba Ali iliyopo Manispaa ya Iringa.

Aidha, Mhe. Kabati amesema bima za afya kwa watoto wenye mahitaji maalum zina umuhimu mkubwa kulingana na watoto wengi kuhitaji matibabu ya mara kwa mara hali inayopelekea changamoto kubwa kwa wazazi wasio na uwezo wa gharama za matibabu.

Mhe. Kabati amewataka wadau zaidi kujitolea kwa watoto wenye mahitaji maalum kwa kuwapa vitu wezeshi vitakavyosaidia kupunguza changamoto walizo nazo.

Katika hatua nyingine Mhe. Kabati, amelaani vikali tabia za watu katika jamii kuonesha vitendo vya unyanyapaa pamoja kuwafanyia vitendo vya ukatili watu wenye ulemavu wakiwemo watoto wenye mahitaji maalum.

WhatsApp Image 2023-03-26 at 18.27.31.jpeg

WhatsApp Image 2023-03-26 at 18.27.31(1).jpeg
WhatsApp Image 2023-03-26 at 18.27.31(2).jpeg
WhatsApp Image 2023-03-26 at 18.27.32.jpeg
WhatsApp Image 2023-03-26 at 18.27.32(1).jpeg
 
Watu kama Rita Kabati ndiyo wametuchelewesha sana kuifikia Tanzania iliyo bora. Hizi siasa za kurubuni watanzania mpk lini?

Rita Kabati yuko bungeni (chombocha maamuzi) kwann asitengeneze mfumo jumuishi wa kitaifa wa kusaidia watoto wote nchini?

Huu ujinga wa kuanza kujipendekeza kwa wananchi ili kupata kura kwenye uchaguzi mkuu ni wa kupingwa na kila mpigania maslahi ya taifa.
 
Watu kama Rita Kabati ndiyo wametuchelewesha sana kuifikia Tanzania iliyo bora. Hizi siasa za kurubuni watanzania mpk lini?

Rita Kabati yuko bungeni (chombocha maamuzi) kwann asitengeneze mfumo jumuishi wa kitaifa wa kusaidia watoto wote nchini?

Huu ujinga wa kuanza kujipendekeza kwa wananchi ili kupata kura kwenye uchaguzi mkuu ni wa kupingwa na kila mpigania maslahi ya taifa.
Bunge limeshatunga sheria ya Bima ya Afya kwa wote. Hapo amefanya yeye kama yeye kwa mapenzi yake.
 
Back
Top Bottom