Dkt. Rugemeleza Nshala: Nimetishiwa maisha baada ya kutoa maoni kuhusu mkataba wa Bandari na DP World

Dkt. Rugemeleza Nshala: Nimetishiwa maisha baada ya kutoa maoni kuhusu mkataba wa Bandari na DP World

Habari wasomaji na wananchi wote.

Je, tumekuwa Taifa la ovyo hivi.

Je, hili ni suluhisho la mjadala katika mambo ya Kitaifa?

Akiuawa, tunatuna ujumbe gani.


Pia soma

---
Ndugu Watanzania!
Dkt. Rugemeleza Nshala ametujulisha kuwa maisha yake yako hatarini. Wakili Dkt. Nshala anasema kuwa ametaarifiwa juu ya mipango ya kutaka kumuua (assassination) inayopangwa dhidi yake! Vitisho dhidi ya maisha ya Wakili Dkt. Nshala vinakuja muda mfupi tu baada ya yeye kutoa maoni yake kwa hisia kali akipinga Mkataba wa Bandari kati Serikali ya Tanzania na Ufalme wa Dubai.

Dkt. Rugemeleza Nshala, ambaye alikuwa Rais wa Tanganyika Law Society (TLS) ni wakili na mwanasheria mbobevu anayejua vema mipaka yake kikatiba na kwa nafasi yake anao wajibu wa kutoa ushauri na maoni kwa Watanzania katika masuala ya sheria na katiba ya nchi.

Sisi Askofu tumepata muda wa kuomba na Dkt. Nshala na kumtia moyo kuwa asiogope kwani alitoa maoni yake kama raia anayeipenda nchi yake na hakuvunja sheria ye yote ya nchi. Kwa maoni yetu, watu wanaomtisha Dkt. Nshala au wanaotaka kuondoa uhai wake ni watu waoga ambao wanataka kumchafua Rais Dkt. Samia ili dunia ifikiri ameanza kuwaua wakosoaji wake.

Kwa hiyo, sisi Askofu Mwamakula tunatoa wito kwa watu, kikundi, vikundi hata taasisi ambao wanapanga kutoa uhai wa Dkt. Nshala pamoja na wanaharakati wengine wanaotoa maoni yao au hata kuikosoa Serikali kuhusiana na suala la Mkataba wa Bandari waache mara moja. Kama wao wanafikiri kuwa Dkt. Nshala na wenzake wamefanya kosa lo lote kisheria, wawapeleke mahakamani badala ya kuanza kuwatisha.

Kutisha watu na kutaka kuwaondoa au kuwaua watu nje ya mfumo wa kisheria ni uhaini, uuaji, unyama na ujambazi bila kujali mtu anayefanya matendo hayo. Sisi Askofu tunatoa tahadhari hii kama kukinga mapema ili watu hao wajue kuwa wanachokipanga kufanya hakikubariki. Kama Dkt. Nshala na wenzake watadhulika kwa lolote, watu waliowahi kutoa kauli zao kwa lengo la kuwatisha, hao watawajibika. Kukinga ni bora kuliko kutibu! Tumetimiza wajibu wetu!

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Dar es Salaam, 6 Julai 2023; 09:39 am.


View attachment 2680028
Kwa jinsi ninavyoifahamu nchi hii ya Tz, uwezekano wa jambo hili kuwa kweli ni zaidi ya takribani asilimia 99.9999
 
Rais Mstaafu wa Chama Cha Wanasheria Tanganyika (TLS) Wakili Dkt.Rugemeleza Nshala amesema amepokea taarifa za vitisho ikiwemo kuuawa.

Akizungumza leo Julia 6, 2023 mbele ya waandishi wa habari amesema kuwa amepata taarifa hizo kutoka kwenye vyanzo vya kuaminika ambavyo akuwa tayari kuviweka adharani.

Amedai kuwa vitisho hivyo vimekuja kufuatia maoni yake aliyoyatoa kuhusu sakata la Bandari ambalo limekuwa gumzo kubwa.

"Nimekuja hapa kama mtanzania na nashikilia Imani yangu, nasema nilichokisema kama Mungu anaona ni uongo kwa kushika biblia hii nianguke chini niondoke duniani. Sisemi Mungu nisaidie Bali nasema kama niliyosema ya uongo naomba uhai wangu Mungu auchukue. Mimi mkristo mkatokiki kwa miaka yangu 57 nineyaona mengi"amesema Dkt. Rugemeleza

Akiwa ameshikiria Biblia pamoja na Katiba mkononi amesema atasimamia anachokiamini kwa imani yake na mapenzi yake kwa Nchi, huku akiwataka wanahusika kutoa vitisho kutubu.

"Naipenda Tanzania, nitaifia nchi yangu damu yangu ikimwagika iendelee kumwagilia rasilimali za nchi yetu na hao watakaofikiria hayo yatawakuta mabaya sana kwao. Nawasihi watuvu wafahanu kwamba siku ya mwisho watajibu sio kwao Bali kwa familia zao na vizazi vyao 440 vya familia zao. Kuanzia Sasa zitateswa na zitateseka kwa dhambi hiyo wanayoifanya. Nayasema haya nikiwa na moyo mweuoe lakini ndugu zangu kama ndio mwisho wangu nasema kwaherini tutaonana paradise" amesema Dkt. Rugemeleza

Ikumbukwe kwenye kauli zake alizozitoa hivi karibuni kuhusu sakata hilo ni pamoja na kukosoa vikali mkataba huo na wahusika waliosaini sambamba na Bunge lililojadili na kupitisha.
 

06 Julai 2023​

🅻🅸🆅🅴 DKT NSHALA ADAI KUTISHIWA MAISHA '' MAISHA YANGU YAKO HATARINI




Mkutano na waandishi wa habari Dr. Nshala athibitisha kupata taarifa kutoka vyanzo vinavyothibitika kuna njama za kuondoa uhai wake Ikiwemo uhai wa wakili Boniface Mwabukusi Prof. Issa Shivji hivyo siwezi kukaa kimya kwani imewahi kutokea kwa Mwangosi, Azori, Ben Saanane kupigwa risasi Tundu Lissu.

Dr. Nshala anasema inasikitisha kuona kuna watu wamejipatia leseni ya kuondoa uhai wa watu kwa kuwa tu kuna wametoa maoni yanayokinzana na wale waliopo madarakani .

Dr. Nshala amesisitiza kuwa mkataba wa bandari unamuhusu rais kutokana na kibali cha rais na mara nyingi mikataba huwa haina muongozo wa rais.

Kulinda maliasilia ya nchi yetu ni haki ya kila raia iliyotamkwa ndani ya katiba ya Tanzania. Hivyo tunavyopiga kelele tunatimiza haki yetu ya msingi ibara ya 26.1 ya katiba inasema .

Ibara ya 9 (c) ya katiba inaitaka serikali kuwajipika pia kutunza mali za taifa.

Huu mkataba unamilikisha mali zote kwa mtu binafsi yaani kampuni ya DP World ya Dubai.

Juzi kumevuja marekebisho yaani Miscellaneous amendments laws ili kuondoa bandari za maziwa na katika mito ya maji ili DP World waweze kufaidi Mali ya asili ya bandari.

DP World anaendelea kupewa ukiritimba wa kumiliki mali zetu kwa aina ya ajabu kupitia muswaada huu mpya utakaopelekwa bungeni kinyume na sheria ya rasilimali iliyotungwa mwaka 2017 ya kulinda mali kwa vizazi vyetu na vizazi vijavyo.

Dr. Nshala nimepata utaalamu mkubwa katika vyuo vikuu tajwa vya Yale na Harvard vyote vya nchini Marekani kwa miaka 10 1/2 kuelewa mikataba na sheria za wawekezaji vizuri. Hivyo elimu niliyopata siwezi kuacha kuitumia kutetea mali ya nchi yetu Tanzania ambayo imenisomesha.

Ningeweza kubaki Marekani kuajiriwa wakati ule kwa mshahara wa dola za kimarekani 22,000.00 kwa mwezi na bonasi kubwa kila mwaka.


Dr. Nshala amesema sitaweza kutishika kukimbia nchi yangu nitabaki hapa hapa Tanzania na wale waovu wanaotaka kuondoa uhai wangu wakifanikiwa basi wao na vizazi vyao laana hii itawaandama milele na kuwasumbua sana.

Mwandishi John Marwa wa Jambo TV anauliza swali kwa Dr. Nshala kuwa kauli za wakili Dr. Nshala zilikuwa kali kwa maoni ya baadhi ya Tanzania.

Vibaraka wa ndani ya nchi wanajidanganya kupindisha maana ya kauli na maneno utetezi wa mali ya umma. Anasisitiza Dr. Nshala kujibu swali la mwandishi, Lugha ni ya uchungu na siyo kali bali kuwaamsha rais, makamu wa rais, mawaziri, bunge kuwa wanapaswa kukubali makosa yao kwa kuwaambia ukweli ....

KATISHIWA KUWAWA KWELI HUYU
 
Aache upumbavu kutafutia kiki za sifa za kihaya wangapi wametoa maoni Yao kuhusu bandari na hawajatishiwa yeye ni nani nchi hii ana nguvu gani ya kuzuia jambo wenye maslai nalo wakitaka kulipitisha
 
Rais Mstaafu wa Chama Cha Wanasheria Tanganyika (TLS) Wakili Dkt.Rugemeleza Nshala amesema amepokea taarifa za vitisho ikiwemo kuuawa.

Akizungumza leo Julia 6, 2023 mbele ya waandishi wa habari amesema kuwa amepata taarifa hizo kutoka kwenye vyanzo vya kuaminika ambavyo akuwa tayari kuviweka adharani.

Amedai kuwa vitisho hivyo vimekuja kufuatia maoni yake aliyoyatoa kuhusu sakata la Bandari ambalo limekuwa gumzo kubwa.

"Nimekuja hapa kama mtanzania na nashikilia Imani yangu, nasema nilichokisema kama Mungu anaona ni uongo kwa kushika biblia hii nianguke chini niondoke duniani. Sisemi Mungu nisaidie Bali nasema kama niliyosema ya uongo naomba uhai wangu Mungu auchukue. Mimi mkristo mkatokiki kwa miaka yangu 57 nineyaona mengi"amesema Dkt. Rugemeleza

Akiwa ameshikiria Biblia pamoja na Katiba mkononi amesema atasimamia anachokiamini kwa imani yake na mapenzi yake kwa Nchi, huku akiwataka wanahusika kutoa vitisho kutubu.

"Naipenda Tanzania, nitaifia nchi yangu damu yangu ikimwagika iendelee kumwagilia rasilimali za nchi yetu na hao watakaofikiria hayo yatawakuta mabaya sana kwao. Nawasihi watuvu wafahanu kwamba siku ya mwisho watajibu sio kwao Bali kwa familia zao na vizazi vyao 440 vya familia zao. Kuanzia Sasa zitateswa na zitateseka kwa dhambi hiyo wanayoifanya. Nayasema haya nikiwa na moyo mweuoe lakini ndugu zangu kama ndio mwisho wangu nasema kwaherini tutaonana paradise" amesema Dkt. Rugemeleza

Ikumbukwe kwenye kauli zake alizozitoa hivi karibuni kuhusu sakata hilo ni pamoja na kukosoa vikali mkataba huo na wahusika waliosaini sambamba na Bunge lililojadili na kupitisha.
Kwa hisia kali
 
Screenshot_20230706-134559.jpg
 
Back
Top Bottom