06 Julai 2023
🅻🅸🆅🅴 DKT NSHALA ADAI KUTISHIWA MAISHA '' MAISHA YANGU YAKO HATARINI
Mkutano na waandishi wa habari Dr. Nshala athibitisha kupata taarifa kutoka vyanzo vinavyothibitika kuna njama za kuondoa uhai wake Ikiwemo uhai wa wakili Boniface Mwabukusi Prof. Issa Shivji hivyo siwezi kukaa kimya kwani imewahi kutokea kwa Mwangosi, Azori, Ben Saanane kupigwa risasi Tundu Lissu.
Dr. Nshala anasema inasikitisha kuona kuna watu wamejipatia leseni ya kuondoa uhai wa watu kwa kuwa tu kuna wametoa maoni yanayokinzana na wale waliopo madarakani .
Dr. Nshala amesisitiza kuwa mkataba wa bandari unamuhusu rais kutokana na kibali cha rais na mara nyingi mikataba huwa haina muongozo wa rais.
Kulinda maliasilia ya nchi yetu ni haki ya kila raia iliyotamkwa ndani ya katiba ya Tanzania. Hivyo tunavyopiga kelele tunatimiza haki yetu ya msingi ibara ya 26.1 ya katiba inasema .
Ibara ya 9 (c) ya katiba inaitaka serikali kuwajipika pia kutunza mali za taifa.
Huu mkataba unamilikisha mali zote kwa mtu binafsi yaani kampuni ya DP World ya Dubai.
Juzi kumevuja marekebisho yaani Miscellaneous amendments laws ili kuondoa bandari za maziwa na katika mito ya maji ili DP World waweze kufaidi Mali ya asili ya bandari.
DP World anaendelea kupewa ukiritimba wa kumiliki mali zetu kwa aina ya ajabu kupitia muswaada huu mpya utakaopelekwa bungeni kinyume na sheria ya rasilimali iliyotungwa mwaka 2017 ya kulinda mali kwa vizazi vyetu na vizazi vijavyo.
Dr. Nshala nimepata utaalamu mkubwa katika vyuo vikuu tajwa vya Yale na Harvard vyote vya nchini Marekani kwa miaka 10 1/2 kuelewa mikataba na sheria za wawekezaji vizuri. Hivyo elimu niliyopata siwezi kuacha kuitumia kutetea mali ya nchi yetu Tanzania ambayo imenisomesha.
Ningeweza kubaki Marekani kuajiriwa wakati ule kwa mshahara wa dola za kimarekani 22,000.00 kwa mwezi na bonasi kubwa kila mwaka.
Dr. Nshala amesema sitaweza kutishika kukimbia nchi yangu nitabaki hapa hapa Tanzania na wale waovu wanaotaka kuondoa uhai wangu wakifanikiwa basi wao na vizazi vyao laana hii itawaandama milele na kuwasumbua sana.
Mwandishi John Marwa wa Jambo TV anauliza swali kwa Dr. Nshala kuwa kauli za wakili Dr. Nshala zilikuwa kali kwa maoni ya baadhi ya Tanzania.
Vibaraka wa ndani ya nchi wanajidanganya kupindisha maana ya kauli na maneno utetezi wa mali ya umma. Anasisitiza Dr. Nshala kujibu swali la mwandishi, Lugha ni ya uchungu na siyo kali bali kuwaamsha rais, makamu wa rais, mawaziri, bunge kuwa wanapaswa kukubali makosa yao kwa kuwaambia ukweli ....