Pre GE2025 Dkt. Samizi aungana na wanamichezo kusaidia wenye uhitaji na kumuunga mkono Rais Samia

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

BWANKU M BWANKU

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2019
Posts
377
Reaction score
435
Jana Jumapili imekua siku nzuri kwa Mbunge wa Jimbo la Muhambwe mkoani Kigoma, Dkt. Florence George Samizi kufurahi na wananchi wake wa Jimbo la Muhambwe ambapo alipata mwaliko wa uzinduzi wa tawi la Yanga SC pale Mukabuye.

Uzinduzi wa tawi hilo la Yanga SC umekuwa na shangwe na umati mkubwa sana wa watu ambapo Mbunge pamoja na mashabiki na wanachama wa Yanga walisaidia wahitaji, kupata chakula cha pamoja na kushuhudia mechi ya mpira wa miguu kati ya kata ya Mukabuye na kata ya Nyaruyoba.

Mbunge amefurahishwa na malengo mazuri ya tawi hilo ikiwamo Bima ya afya, kusaidiana kama wanachama, kujitolea kilimo cha pamoja na mengine mengi.

Pia soma: Uzi Maalum wa Vibweka na Hekaheka za wanasiasa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Mashabiki na wanachama wamemuahidi Mbunge Samizi kuendelea kuiunga mkono serikali yao ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan huku akiwashukuru waandaji wote kwa kumkaribisha kuzindua tawi hilo la Yanga la Mukabuye.

Your browser is not able to display this video.

Your browser is not able to display this video.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…