KWELI Dkt. Slaa alitoa kauli ya kuipindua Serikali wakati wa mahojiano

KWELI Dkt. Slaa alitoa kauli ya kuipindua Serikali wakati wa mahojiano

Taarifa hii imethibitika kuwa ya kweli baada ya kufanya tathmini ya kina
Salaam

Ndugu zangu, katik pitapita zangu mitandaoni hasahasa kwenye mjadala unaomuhusu Dkt Slaa nimekuwa nikikutana na clip fupi ya Sekunde zipatazo 15 ikimuonesha anatamka kuhusu kupindua Serikali. Kwa namna Clip hiyo ilivyokatwa nashindwa kuelewa muktadha wa kauli hiyo.

Naombeni mtusaidie kutafuta ukweli wa tukio hilo au Interview hiyo kwa kirefu zaidi.

Clip niliyokutana nayo na inayosambaa ni hii hapa chini:

1692205023774.png

Picha: Dkt Slaa


Video 1: Kipande (clip) inachosambaa kwenye mitandao ya kijamii


Video 2: Sehemu ya kipande cha Dkt. Slaa kwa urefu zaidi
Chanzo: Star TV
 
Tunachokijua
Tangu kukamatwa kwa Dkt. Slaa mnamo Agosti 13, 2023 kumeibuka mijadala mbalimbali kumhusu. Wakili wake Adv. Dickson Matata katika ukurasa wake wa X (zamani Twitter) alitoa taarifa zinazodai kuwa Dkt. Slaa amehojiwa kuhusu kosa la uchochezi kinyume na Sheria na baada ya muda tuhuma zikabadilika na kuwa uhaini.

Tangu kutolewa taarifa hiyo ya Wakili mijadala imeibuka katika mitando mbalimbali ya kijamii kuhoji sababu ya Dkt. Slaa kuhusishwa na kosa la uhaini. Baadhi ya watu katika mitandao wamekuwa wakisambaza video yenye Sekunde 15 ikimuonesha Dkt. Slaa akitamka kuhusu kupindua Serikali.

Je, ni kweli Dkt. Slaa alitoa kauli ya kuipindua Serikali?
JamiiForums imefanya uchunguzi na kubaini kuwa kauli hiyo ya Dkt. Slaa aliitamka katika mahojiano yake aliyofanyiwa kwenye kipindi cha Medani za Siasa kinaendeshwa na Star TV. Mahojiano hayo yaliwekwa katika ukurasa wa YouTube wa Star TV Habari mnamo Julai 1, 2023 yakiwa na urefu wa 01:30:53 (Saa moja dakika thelathini na sekunde hamsini na tatu).

JamiiForums baada ya kutazama mahojiano yote ambayo kwa kiasi kikubwa Dkt. Slaa aliongelea Mkataba wa Bandari na harakati zake za kisiasa. Imebaini kuwa kauli ya kuhusu kuipindua Serikali aliitoa kuanzia 1:06: 40. Sehemu ya mahojiano hayo Dkt. Slaa anasema:
Tunaishinikiza Serikali mpaka iondoke kwa sababu Serikali ibara ya nane ya katiba inasemaje?
Ni Serikali ya ajabu ambayo imeingia kwenye mkataba bila kushirikisha watu wake, tatizo lipo kwenye katiba yetu na ndiyo maana tunataka katiba mpya sasa, sio jana Wala si kesho Ili upuuzi usitokee tena.
Upuuzi imetokea, tazama Marekani Rais anapelekwa mahakamani. Donald Trump sasa hivi yupo mahakamani kwa kesi ya ngapi? Juzi amepelekwa na kushitakiwa kwa makosa 37 kwenye kesi Moja.
Sisi tumekinga Marais wa kwetu hii ni nchi ya aina gani? Tunaishi Dunia ipi? Afadhali Dunia ya kina Mangungo waliodanganywa kwa kupewa shanga na kioo Cha kujitazamia Hadi inauzwa ni kwa sababu ameletewa kitu Cha kujitazama, ndiyo kitu muhimu sana kwake.
Hatuko huko tena, tutapiga kelele, tutaishinikiza Serikali na Matokeo yake kama hawataona leo wataona karibuni sana.
Mwandishi: Hoja ya msingi hapa kwa sababu mmeshafikia kwenye hii hatua, Watanzania hawana Cha kufanya.
Dkt. Slaa: Sio hawana Cha kufanya Serikali inaweza, kwani Serikali zinapopinduliwaga sasa kwanini zinapinduliwa? Huwezi kuniambia hamna Cha kufanya.
Mwandishi: Tufanye nini sasa hapo?
Dkt. Slaa: The extreme ni kuipindia Serikali. Serikali ibara ya nane inasema mamlaka yake yote yanatoka kwa Wananchi, Serikali inayofanya vitu bila kujali mamlaka ya Wananchi na inafanya vitu kwa kejeli inatuona Sisi watoto wadogo.
Inasema kwamba itarekebisha wakati tunajua hakuna njia. Jana nilimsikiliza Shivji. Shivji katika nchi hii ni kama Dictionary ya Sheria. Amesema njia pekee ni Bunge likae chini na wajitambue kwamba walikosea, wajishushe, wabatilishe kwasababu ndiyo njia pekee iliyobaki kufuta huo mkataba mbaya na huyo ndiyo Mwalimu ambaye Dunia inamtambua kama mtaalaum wa sheria. Halafu Serikali inakuja inapiga piga machenga.

Hivyo, kutokana na chanzo hiki kilichopitiwa na JamiiForums, hoja inayodai kuwa Dkt. Slaa alitamka kuhusu kuipindua Serikali ni ya kweli.
Naona Padre Slaa anasagiwa kunguni hapa.

Hii ni laana ya kuwatelekeza Watoto wa Mwangosi.
 
Nimesikiliza Clip inayotembea mtandaoni ikionesha kuwa Slaa,Mdude na Mwabukusi Wakiwa mtandao wa Club house walikuwa wanajadili maswala ya uchochezi na mikakati ya kupindua nchi kwa kuunguza vituo vya polisi.

Naomba kuwaukiza wataalamu wa sauti,hizo sauti ni za kwao au zimetengenezwa na watu wa kitengo.

Kama ni sauti zao,unafikiri wewe ungekuwa na mamlaka ungewaacha?

Au ungechukua hatua stahiki kukomesha hali hiyo.

Tusipotoshe watu tujadiliane ukweli.
 
Nimesikiliza Clip inayotembea mtandaoni ikionesha kuwa Slaa,Mdude na Mwabukusi Wakiwa mtandao wa Club house walikuwa wanajadili maswala ya uchochezi na mikakati ya kupindua nchi kwa kuunguza vituo vya polisi.

Naomba kuwaukiza wataalamu wa sauti,hizo sauti ni za kwao au zimetengenezwa na watu wa kitengo.

Kama ni sauti zao,unafikiri wewe ungekuwa na mamlaka ungewaacha?

Au ungechukua hatua stahiki kukomesha hali hiyo.

Tusipotoshe watu tujadiliane ukweli.View attachment 2718837
Wewe Una uhakika hizo ni sauti zào ?
 
Nimesikiliza Clip inayotembea mtandaoni ikionesha kuwa Slaa,Mdude na Mwabukusi Wakiwa mtandao wa Club house walikuwa wanajadili maswala ya uchochezi na mikakati ya kupindua nchi kwa kuunguza vituo vya polisi.

Naomba kuwaukiza wataalamu wa sauti,hizo sauti ni za kwao au zimetengenezwa na watu wa kitengo.

Kama ni sauti zao,unafikiri wewe ungekuwa na mamlaka ungewaacha?

Au ungechukua hatua stahiki kukomesha hali hiyo.

Tusipotoshe watu tujadiliane ukweli.View attachment 2718837

View: https://www.youtube.com/watch?v=wA4Ibd5C8HU
 
Kwa Hii nchi Ilivyo chochote kinawezekana Hat hizi Sauti siamin kam ni Za Kwao, maan Kuna watu wana kipaji cha kuigiza sauti.
 
Sijui atatokaje kwenye hili, labda asimamie kwenye neno kuipindia

Ndiyo maana kuna haja ya kuchagua maneno inapotokea unatoa maoni yako public hasa unapokuwa umeghadhabika kama ilivyotokea kwa Dr. Slaa
Unajua maana ya "extreme"?

Amandla...
 
Muulizeni S.Nyerere !!



anajua ukweli wa hizo Sauti !!.


alichokifanya Kwa Mwaka 2015, alipokua anaigiza sauti za JN kumnanga EL, ili ionekane kwamba EL alishakataliwa na JN Toka zaman .


Walewale wa TISI ya JK, Kwa Staili ileile, wanatumia mbinu ileile, kuhalalisha Ujinga wao.


WATANZANIA TUSIMAME NA AKINA MWABUKUSI, DR SLAA, ,,, SHETAN HAJAWAHI KUSHINDA.
 
Muulizeni S.Nyerere !!



anajua ukweli wa hizo Sauti !!.


alichokifanya Kwa Mwaka 2015, alipokua anaigiza sauti za JN kumnanga EL, ili ionekane kwamba EL alishakataliwa na JN Toka zaman .


Walewale wa TISI ya JK, Kwa Staili ileile, wanatumia mbinu ileile, kuhalalisha Ujinga wao.


WATANZANIA TUSIMAME NA AKINA MWABUKUSI, DR SLAA, ,,, SHETAN HAJAWAHI KUSHINDA.
haaaa yaani wewe ndiyi shetani wa nchi hii yaani ujinga wanaouongea hao wahaini bado unawatetea?
 
Serikali za kipuuzi zinapinduliwa wala hakuna uongo juu ya hilo na serikali iliyopo Tanzania ni ya kipuuzi.
 
Jaman JF jiepusheni na kusema jambo ni Kweli au Sio Kweli.

Ukweli ni kitu kigumu sana kuthibitisha.

Yohana 18:38.
Pilato akamwambia, Kweli ni nini? Naye akiisha kusema neno hilo akawatokea Wayahudi tena, akawaambia, Mimi sioni hatia yo yote kwake.
 
Najua Mkuu

life-threatening
Dkt. Slaa: The extreme ni kuipindia Serikali. Serikali ibara ya nane inasema mamlaka yake yote yanatoka kwa Wananchi, Serikali inayofanya vitu bila kujali mamlaka ya Wananchi na inafanya vitu kwa kejeli inatuona Sisi watoto wadogo.

Nilivyomuelewa Dkt Slaa hapa ni kuwa wananchi wana options tofauti hili na the "extreme" ni kuipindua serikali. Na kitu "extreme" hakipendezi na ni option ya mwisho ya wananchi pale wanapoona kuwa mamlaka yao hayathaminiwi.

Amandla...
 
Back
Top Bottom