inaelekea Mshumbusi kakomba kila kitu mzee ana njaa sanaNjaa ni hatari sana.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
inaelekea Mshumbusi kakomba kila kitu mzee ana njaa sanaNjaa ni hatari sana.
Labda alisahau [emoji28][emoji28]Siku ameitisha press pale Serena siku anatangaza kuacha siasa za majukwaani alitakiwa kulisema swala la utekaji na utesaji ndani ya chadema ili kina Mwigulu walishikie bango kuzunguka nchi nzima kuichafua Chadema. AJABU KUBWA ANASEMA LEO
Hakuna ccm fisadi anayeweza mkumbatia Dr.slaa,ila wale smart na wasio wafia vyama ndo wanaelewa Dr.Slaa siku zote anasimamia misimamo.CHADEMA HAWATOKUJA KUJISAFISHA KWA KUPOKEA MAFISADI.
Hilo linatosha kabisa Bila kuanza kuingia ndani,Drama zao na CCM sisi tunaona waigizaji tu na ndugu zao kina mzito kabwe
Slaa tokea asaliti yeye na Lipumba, hakuna anayewaskiliza tenaSikutarajia Slaa aongee tofauti na hivyo, eti wawekezaji walikuja awamu ya tano. Slaa anadhani kwakuwa aliwahi kuamini hapo nyuma basi na sasa ataaminika.
huyu mzee kiazi sanaKwenye swala la kupigwa risasi Tundu Lissu, anajitahidi kuonyesha UPUMBAVU WAKE WA UZEENI, yaani kwa style ile ya uongozi wa Magufuli, CHADEMA wapange njama za kumshambulia Lissu, wawaondoe walinzi wa area D, wang'oe CCTV camera, wafanye tukio la kumiminia risasi Lissu, waondoke ndani ya mipaka ya jiji la Dodoma wakiwa salama?
Baada ya kupigwa risasi, wafanye mpango wa kushawishi spika asimlipe fedha za matibabu, (spika naye akubaliane na Chadema kutomlipa stahiki zake, na akae kimya)
Baada ya kumnyima matibabu, Chadema wafanye njama za kumvua ubunge na kusimangwa kuwa "hajulikani alipo" halafu serikali ya MAGUFULI inyamaze tu, isikifute CHADEMA????
Anafikiria kwa kutumia tumbo Mzee huyoSijawahi kufikiria kama Dr. Slaa anaweza kuwa mnafiki kiasi hiki! Kwa umri wake, hastahili kuwa hivyo. Lazima kuna kitu hakipo sawa kichwani au moyoni mwake.
Kama CHADEMA walijaribu kumwua kiongozi wao, yeye Dr. Slaa alikuwa kiongozi kwenye Serikali ya awamu ya 5, tena Serikali iliyouchukia sana upinzani, serikali iliyokuwa tayari hata kuyatengeneza makosa dhidi ya wapinzani ili kuwakomoa/kuwakomesha, alishindwa nini kuitoa hiyo taarifa? Jinai huwa haifi.
Polisi wanatakiwa kumkamata Dr. Slaa na kumhoji kuhusika kwake na utekaji na kukusudia kumwua mtu aliyemtaja. Yeye alikuwa mtendaji mkuu wa chama. Kama kuna uovu uliofanywa, yeye aliyekuwa mtendaji mkuu, ndiyo mahali sahihi pakuanzia. Hata kama hakushiriki, bado ana hatia. Maana kujua kuwa kuna uovu umetendeka halafu ukakaa kimya, ni hatia.
Lakini pia tujiulize, aliyetekwa na kujaribu kuuawa ni mzima, alinusurika, kwa nini hakwenda kushtaki, wakati watekaji walikuwa wanafahamika?
HAKUNA JAMBO LISILO NA MWISHO,UNAFIKI WA MTU UTAJULIKANA TU.Njaa
Mwanasiasa Willbrod Peter Slaa amefanya mahojiano na kuzungumza mambo mengi kuhusu siasa, mahojiano haya ni mwendelezo ya interview aliyofanya wiki iliyopita.
TAARIFA YA CAG INAPOTOSHWA
“Kuna upotoshwaji kwenye taarifa ya CAG, nadhani Zito Kabwe angelisaidia sana taifa hili kama angekuwa mkweli, mimi na Zitto tulishiriki kutengeneza sheria ya ukaguzi wa fedha 2009, hata maneno yaliyopo kwenye sheria hiyo yametoka kwetu.
“Moja ya maelezo ya ile sheria inasema baada ya CAG kukabidhi ripoti yake kwa Rais kisha kuifikisha Bungeni siku saba baadaye, ripoti hiyo haitakiwi kuwa public discussion, kwa kuwa ni kama mhtasari tu wa ripoti.
“Inatakiwa Kamati ya Bunge ndiyo iifanyie kazi, mfano kuna sehemu unaweza kukuta risiti haikuonekana wakati wa ukaguzi lakini hiyo ikapitishwa na kuonekana ni wizi, tumepotosha maana ya ile taarifa ya CAG.
CAG AMESABABISHA TAHARUKI KWA RIPOTI YAKE
“Kwanza hata CAG mwenyewe amechangia kuleta hii taaruki kwa kuwa huwa ni ya awali tu na analijua hilo, inatakiwa irudi kwa akaunti ofisa wa Serikali ijadiliwe, pia CAG wakati anatoa taarifa zake hadharani hatakiwi kuingia ndani kutoa ufafanuzi zaidi kama anavyofanya.
“Unaweza kukuta ripoti hiyo ikifika kwenye Kamati ya Bunge vitu vingi vikawekwa sawa, mfano labda kulikuwa na upotevu fulani wa mambo madogomadogo ambayo kwa nje yanaonekana kama ni wizi lakini details zikiwekwa sawa kunakuwa hakuna tatizo.
UBUNGE WA KINA MDEE SPIKA HANA KOSA, NITAZUNGUMZA CHADEMA WAKISHAKAA KIKAO
“Nimeona kwenye vyombo vya habari kuwa watajadiliwa na chama chao katika rufaa yao, naona lawama zimepelekwa kwa mtu ambaye hausiki (Spika).
“Chama kilitakiwa kufungua kesi Mahakamani kuhoji Tume ya Uchaguzi kwa kupitisha majina hayo lakini sijaona kesi. Mimi nitazungumza baada ya rufaa yao kupitiwa na CHADEMA, nimesikia wanakaribia kuwajadili kwenye kikao chao.
HOJA YA KATIBA SIYO MAHITAJI MUHIMU YA WANANCHI
“Mabosi wa vyama vya siasa ni wananchi, wanatakiwa kujiuliza wanayoyafanya yanawagusa vipi wananchi, kwa sasa kuna mambo mengi ya muhimu lakini hivyo vyama vimekuwa bize kuzungumza habari za ajenda ya Katiba.
“Hawana ajenda ambazo mwananchi anaweza kujiuliza kama inaweza kuweka chakula mezani, hakuna katiba ambayo inaweza kuzungumzia kila kitu.
“Katiba yetu ina vipengele vingi vya muhimu lakini havitekelezwi, japo sijasema kuwa katiba siyo muhimu.
“Mimi ni kati ya watu waliozunguka Tanzania kukusanya maoni lakini tusipotoshe kuwa katiba ndiyo jibu la kila kitu, siyo kweli.
“Leo hii Marekani ina katiba tunayoisifu lakini Donald Trump si alishutumiwa anataka kufanya mageuzi.
KATIBA PENDEKEZWA NI MBOVU KULIKO KATIBA YA SASA
“Sisi tuna maoni ya Jaji Warioba, licha ya kuwa kulikuwa kuna mambo yamekosekana lakini yapo mazuri ambayo tunaweza kuyatumia.
“Baada ya maoni hayo kupelekwa Bungeni ikachujwa ikatoka inayoitwa Katiba Pendekezwa, ni mbovu kuliko hata katiba tuliyonayo sasa hivi.
SIZUNGUMZII SUALA LA LISSU KUPIGWA RISASI SABABU UTEKAJI ULIKUWEPOA CHADEMA
“Kuna watu wananiuliza kuhusu Tundu Lissu kupigwa risasi, kuwa sipendi kulizungumzia hilo kwa kuwa sita taarifa zake za uhakika.
“Nitoe mfano iliwahi kutokea huko nyuma nikiwa Katibu Mkuu CHADEMA, nililetewa taarifa za mtu wangu anaitwa Joseph, huyu alikuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Temeke, alitekwa saa sita usiku. Kesho yake saa sita mchana nikahitisha mkutano na waandishi wa habari nikaisema sana Serikali na Usalama wa Taifa.
“Saa nane mchana siku hiyohiyo Joseph akapatikana, alikutwa ametupwa maeneo ya Ununio ameumia sana usoni.
“Mwezi mmoja baadaye kijana wangu wa Red Brigade anakuja kwangu kuniambia yeye ndiye aliongoza kukosi cha kwenda kumteka nyara huyo mwenyekiti huyo.
“Nikauliza kwa nini hakuja kwangu akasema ‘wapo viongozi wanaojua’, nikaamua kunyamaza, ndiyo maana ninapoulizwa suala la Lissu ninasema hapana, CHADEMA kwanza wajiangalie wao ndani.
“Huyo kijana (Joseph) walivyomtupa ufukweni walijua amekufa, kumbe alikuwa hajafa labda upepo ulimpiga akaamka. Miaka kadhaa baadaye tukaanza kusikia watu wanaokotwa wamekufa ufukweni, unadhani inatoa pcha gani!
“Ukiwa kiongozi lazima uwe kunasema ukweli hata kama unaona watu wako wanakosea.
SINA TATIZO LA LOWASSA
“Mimi na Lowassa tulipishana kwenye principal siyo maisha, mimi niliwahi kufanya fund rising na Jakaya Kikwete siku moja baada ya kupanda jukwaani na kumsema tena kwa mambo mazito.
“Nimeishi Ulaya, nimeona mambo ya kwenye mabunge, kuna muda inafika hatua wabunge wanapigana ngumi lakini wakitoka wanaenda kunywa bia. Unatakiwa kutofautisha maisha binafsi na siasa. Hivyo sikuwa na tatizo binafsi na Lowassa.
AWAMU YA TANO HAIKUFELI DIPLOMASIA YA KIMATAIFA
“Watanzania tuwe wakweli, tumefeli wapi, mimi nimekutana na wafanyabiashara wengi, wapo walioniambia wamchoshwa na Tanzania yenye ufisadi.
“Wapo walioamua kuondoa biashara zao huko nyuma lakini katika awamu ya tano waliamua kurejesha biashara hapa nchini, kwa nini? Ni kwa sababu kulikuwa kuna mambo mengi yanaenda vizuri, nazungumza kwa kuwa najua zaidi kilichokuwa kinaendelea.”
Chanzo: Dar24
[emoji28][emoji28][emoji28] dingi kalazwa Sana kwenye Noah. Alaf nackia mkewe kabaki mbele, analiwa na mzungu hukoLissu Ile siku amesema walivyomteua Lowassa kua mgombea wao kupitia CHADEMA walivyoenda nyumbani kwa Dr. Slaa walikuta mkewe amemfungia nje ya mlango amemtupia na mashuka,Slaa akawa analala kwny Noah yake [emoji16][emoji16][emoji16],mpk leo Dr. Mihogo hataki kabisa kumsikia Lissu
Siyo 'huenda' hakika ndiyo kazi anayofanya. Kitendo cha kutuletea mfano usiolingana na mazingira halisi si cha kiungwana! ni kitendo cha kukosa utuHuenda Slaa ameamua kiusafisha awamu ya 5 dhidi ya hizo tuhuma maana alikuwa mtumishi wake.
Halafu, yule kijana aliyetekwa na kuteswa, ametuambia kuwa, hakufa. Kwa mazingira hayo, bila shaka taarifa zake zilifika polisi. Kwa hiyo, hakuwaambia hao polisi ni kina nani waliomfanya vile?Kwamba chadema ndio waliotoa CCTV camera kwenye eneo la tukio pamoja na kuwafukuza polisi wa doria wanaolinda eneo hilo ili kupisha shambulizi?
Tupo wengi sana tunaomwamini bado.Nani atamuamini Tena msaliti?
Hoja hapa ni kuwa ikiwa Dr Slaa anadhani tukio linaweza kufanywa na yoyote asingetutolea mfano wa red brigade. Pili, kama ametoa mfano huo hakutakiwa kuacha facts nyingine kama za Walinzi kuondolewa eneo lile, Camera kuondolewa hadi leoSlaa hajapinga Lissu kupigwa risasi ila kapigwa na nani?
Ndugu nakuambia katika siasa kuna mambo mengi! Si CCM wala si Chadema, kuna watu humo ndani ni mamafia kwelikweli na wanashirikiana kwenye mambo yao ya mauaji vzri tu! Usicheze ata kdg na hawa watu ukiteleza unaenda na maji
Mzee Slaa,anajiongezea laana....Damu ya Lissu pale Area D,itawatesa wengi sana Maisha yao yote!Hoja hapa ni kuwa ikiwa Dr Slaa anadhani tukio linaweza kufanywa na yoyote asingetutolea mfano wa red brigade. Pili, kama ametoa mfano huo hakutakiwa kuacha facts nyingine kama za Walinzi kuondolewa eneo lile, Camera kuondolewa hadi leo
Dr Slaa alitakiwa apige kelele tujue kwanini Walinzi waliondolewa ili kama ni njama za Chadema zijulikane. Alitakiwa apiga kelele kuhusu Camera ili tujue waliofanya unyama ni red brigade au wasiojulikana. Alichokifanya ni kuchukua upande akisukuma ''agenda'' kwamba TL alitendewa na wenzake.
Huu ni upuuzi na tuuite hivyo kwasababu Dr Slaa ni mhanga wa matukio kama hayo leo tunajiuliza 'bei yake ni kiasi gani' kwamba anaweza kufanya kazi chafu kama hiyo tena akiwa Padre
Si mara moja watu wamemvumilia lakini sasa anavuka mipaka aelezwe ukweli.
Kwa maneno ya Dr Slaa usidhani watu kama TL na Wahanga wengine wanajisikia vizuri
Kauli zake binafsi kwa matamanio yake ya kusikika asizifanyie mzaha kwa damu za wanadamu
Kama hawajulikani uchunguzi unatakiwa. Tuelezwe nani aliondoa Walinzi, Camera ziliondolewa na nani. Tukipata majibu hayo tutajua akina nani wamehusikaKama watekaji hawajulikani! Kwanini tusiwe na mashaka kwamba wenyewe kwa wenyewe wanaweza kutekana na kupigana risasi!
Kawaulize Polisi wewe mfuasi wa Jiwe, hao ndio wana mamlaka na nyenzo za uchunguzi.
Ndo shida ya wafuasi wa chadema.
Kushughulisha akili hamtaki .
mna mwenyekiti,mna makamu mwenyekiti ,mna katibu MKUU n.k
Wakashindwa kutolewa ufafanuzi haya madai ya slaa?
Nenda leo uniambie pale kuna walinzi?Hoja hapa ni kuwa ikiwa Dr Slaa anadhani tukio linaweza kufanywa na yoyote asingetutolea mfano wa red brigade. Pili, kama ametoa mfano huo hakutakiwa kuacha facts nyingine kama za Walinzi kuondolewa eneo lile, Camera kuondolewa hadi leo
Dr Slaa alitakiwa apige kelele tujue kwanini Walinzi waliondolewa ili kama ni njama za Chadema zijulikane. Alitakiwa apiga kelele kuhusu Camera ili tujue waliofanya unyama ni red brigade au wasiojulikana. Alichokifanya ni kuchukua upande akisukuma ''agenda'' kwamba TL alitendewa na wenzake.
Huu ni upuuzi na tuuite hivyo kwasababu Dr Slaa ni mhanga wa matukio kama hayo leo tunajiuliza 'bei yake ni kiasi gani' kwamba anaweza kufanya kazi chafu kama hiyo tena akiwa Padre
Si mara moja watu wamemvumilia lakini sasa anavuka mipaka aelezwe ukweli.
Kwa maneno ya Dr Slaa usidhani watu kama TL na Wahanga wengine wanajisikia vizuri
Kauli zake binafsi kwa matamanio yake ya kusikika asizifanyie mzaha kwa damu za wanadamu