Ujamaa ni mhimu
JF-Expert Member
- Sep 30, 2022
- 1,203
- 1,011
Katiba ya wananchi italetwa na wananchi wasio na mihemko ya vyama vya siasa ili iwesheria mama Kwa vyama vyenu.Unaelewa unazungumza nini lakini? Unaelewa maana ya "chama cha siasa" kweli wewe?
Vyama vya siasa ndiyo hao watu. Utasemaje wafanye shughuli zao nje ya vyama vyao?
Mimi bado naamini huelewi unazungumza nini...!!
Hujui unasema nini wewe. Unahitaji kuelimishwa..!!
Wewe unadhani chama cha siasa ni kitu gani? Ni mlima au mnyama fulani?
Kama ulikuwa hujui, ngoja nikufundishe:
Kwamba, chama cha siasa ni mkusanyiko wa watu ambaao ndiyo hao wananchi unaowasema. Hawa nao katiba inawahusu na ni ya kwao pia Kwa sababu imebeba maslahi yao kama wananchi..
Muhimu ni makundi yote ya kijamii (all social fractions) kuungana na kuidai hiyo katiba...
Ingia na wewe kwenye harakati hizo za kudai katiba mpya ili uhakikishe maslahi yako yanaingia kwenye katiba mpya...
Cha ajabu wewe unataka vyama vya siasa visishiriki. Je, maslahi yao yatawakilishwa na nani kwenye katiba mpya itakayoandikwa?
Kwanini huelewi simple logic kama hii? Umesomea shule gani wewe?
Hapa kidogo akili zimekurudia na umeandika something sensible...
Lakini kabla ya kuundwa hiyo taasisi, lazima wananchi wa makundi yote ya kijamii (ukiwemo wewe bodaboda) mshirikiane na taasisi zingine huru kama vyama vya siasa (CCM, CHADEMA, ACT WAZALENDO, CHAUMA nk); NGOs, vyama vya kitaaluma kama TALGWU, MEWATA, CWT, RAAWU nk; vyama vya wakulima na wafugaji nk nk ili kutia pressure kwa watawala wenye mamlaka ya kisheria kukubali matakwa ya wananchi na kuanzisha mchakato wa kuandika katiba mpya..
Hakuna unajisi hapo. Ni haki yao pia maana nao ni sehemu ya wananchi wa nchi hii na katiba inawahusu na imebeba maslahi ya kisiasa vile vile...
Nisome huko☝️☝️☝️☝️huko juu utaelewa
Huelewi. Nisome kuleeeee juu☝️☝️☝️
Vyama siasa ni vinaundwa na wananchi pia. Nao katiba mpya inawahusu. Unataka waende wapi..?
Hujui unaandika nini!!
Katiba mpya inatakiwa ibebe Kila aina ya "mihemko" toka makundi yote ya kijamii kama vile:
1. Wafanyakazi wa sekta ya umma (walimu, madaktari, wahasibu, wanasheria nk)
2. Wakulima & wafugaji..
3. Wanasiasa na vyama vya siasa.
4. Bodaboda, mamantilie, mafundi sherehani nk nk...
WHY? Kwa sababu hawa wote ni wananchi na katiba ni yao!!
Kama utakuwa hujaelewa mpaka hapo, basi wewe utakuwa na roho ngumu kwelikweli..!!
Kwa heri..