Dkt. Slaa kuwataja walio nyuma ya uuzwaji wa Bandari kama 2007 alivyowataja Mkapa na Kikwete kwenye ‘List of Shame’ Mwembeyanga

Quinine

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2010
Posts
22,227
Reaction score
49,628
Tarehe 24/10/2007 Balozi Dr. W.P. Slaa, akiwa viwanja vya Mwembeyanga Temeke alitaja majina 11 akiwemo Rais mstaafu Mkapa na Rais aliyekuwa madarakani Mh Kikwete kuwa ni miongoni mwa Mafisadi wa nchi.

Akiongea na waandishi wa habari kwenye hotel ya Regency 13 June, Slaa alisema,

“Waliohudhuria maonesho ya Dubai Expo 2022 ni viongozi wa Serikali, wamesafiri, wamelala hoteli, wamekula chakula kwa kodi ya watanzania.”

“Naomba pia kuwakumbusha kuwa Serikali ya Tanzania iliwakilishwa na Rais mwenyewe na kulisainiwa mikataba 17.”

Tutarajie makubwa tena kwenye mkutano wake unaotarajiwa kufanyika Jumapili ya tarehe 23/7 mwaka huu. Je atawataja wahusika wote walio nyuma ya uuzwaji wa Bandari zetu? Na je, majina ya baadhi ya walio kwenye Listi of Shame kama kina Rostam Azizi yatajirudia? Tutege masikio.

Mwembeyanga List of Shame.

1. Dr. Daudi T.S. Balali X
2. Gray Mgonja
3. Basil P. Mramba X
4. Patrick W.R. Rutabanzibwa
5. Nimrod E. Mkono X
6. Benjamin W. Mkapa X
7. Andrew J. Chenge
8. Edward N. Lowassa
9. Rostam Aziz
10.Nazir Karamagi
11. Jakaya Mrisho Kikwete.
 
Kabla ya kuwataja hao anaodai wamehongwa kwenye Bandari...yeye sasa atuambie alihongwa nini mpakabakawa na uwezo wa kwenda kula bata na aliyekuwa Mkewe Bi Josephine Mshumbuzi kule Canada na baadae alifanya miujiza gani ya kiutumishi mpaka kuzawadiwa Ubalozi tena Ulaya. Asipotaja sisi tutamkumbusha
 
Ngoma inogile,upande wapili wao wako bize kutaka wazalishwe na waarabu ndio faida ya kugawa bandari kwa waarabu,hopeless kabisa.
 
Kama una uhakika alihongwa wewe taja na yeye atawataja walionyuma ya mkataba kwa upande wake.
 
Pumba tupu
 
Dr Slaa anapaswa ajiweke na yeye mwenyewe katika hio "LIST OF SHAME" yake, jina lake liwe namba 1 au 2 pale juu kwa alichotufanyia watanzania na upinzani 2015.

Bila uzandiki na tamaa zake za kununuliwa 2015, sasa hivi CCM ingekua mahututi ICU au kaburini kabisa.

Hichi kizee kinatafuta kiki kisiasa na huruma ya wananchi ili kianzishe chama chake cha siasa 2025.
 

BASIL PESA MBILI MRAMBA.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…