Dkt Slaa na wenzake wanashindwa kuelewa IGA ya DPW haiwezi kuwepo bila mabadiliko ya sheria yetu ya Natural Wealth and Resources Permanent Sovereignty

Dkt Slaa na wenzake wanashindwa kuelewa IGA ya DPW haiwezi kuwepo bila mabadiliko ya sheria yetu ya Natural Wealth and Resources Permanent Sovereignty

Hivi ni kwa nini unalipenda sana hilo jina la Tanganyika tulilopewa na mkoloni Mwingereza? Yule mkoloni Mujerumani alituita Deutsche Ouster Africa. Hata muungano wetu na Zanzibar ukivunjika, kamwe hatutakubali majina hayo waliotuita wakoloni hao yarejee. Tutatafuta jina letu wenyewe zuri. Tunaweza kuendelea na jina la Tanzania. Au tukajiita Nyanyembe au Msimbazi na kadhalika.
Panua akili kidogo. Hapa siyo swala la kupenda hili jina Tanganyika.
Hata hivyo umekosea, Tanganyika siyo jina alilotoa mkoloni. Inaonekana historia ya nchi hii huijui. Lakini la muhimu ninakuelekeza kwenye huo mstari huo wa kwanza.
Naona wewe ni kati ya hawa watu wa aina ya 'mwendo kasi', pamoja na kuwa na hiyo MD.

Pamoja na hayo yote, mada yako ni ya msingi sana.
 
Panua akili kidogo. Hapa siyo swala la kupenda hili jina Tanganyika.
Hata hivyo umekosea, Tanganyika siyo jina alilotoa mkoloni. Inaonekana historia ya nchi hii huijui. Lakini la muhimu ninakuelekeza kwenye huo mstari huo wa kwanza.
Naona wewe ni kati ya hawa watu wa aina ya 'mwendo kasi', pamoja na kuwa na hiyo MD.

Pamoja na hayo yote, mada yako ni ya msingi sana.
Mimi ni 'Muhenga'. Wa mwendo kasi ni hao akina Dr Slaa, Mwabukusi na Mudude wanaohamasisha maandamano yasiyo na kikomo kwa kupinga jambo (IGA) ambalo halipo.
 
Uwepo wa sheria (maandishi) ni jambo moja na utekelezaji (uwepo wa watu waadilifu na utashi wa kisiasa) ni jingine.
Sheria za kuzuia wizi na maovu mengine zipo.
Hata hivyo, wizi na ufisadi hushamiri au kupungua kutokana na uadilifu wa watu, hasa wanaokuwa kwenye madaraka.
 
Mimi ni 'Muhenga'. Wa mwendo kasi ni hao akina Dr Slaa, Mwabukusi na Mudude wanaohamasisha maandamano yasiyo na kikomo kwa kupinga jambo (IGA) ambalo halipo.
Nilikuelewa toka mwanzo, nilitaka tu kukupanua akili uone kuwa hiyo DP World ni kipande tu cha matatizo mengi yanayo sababishwa na hilo moja tu la uTanganyika kupotea.

Mwabukusi aliweka wazi toka mwanzo kuhusu hili.

Kwa hiyo unakosea kudhani kwamba kwa IGA kudhibitiwa, ndiko kuwe mwisho wa kero nyingi nyinginezo zinazohusu muundo wa muungano tulionao sasa; unao waruhusu akina Samia toka Zanzibar kuja kuamua maswala yote yaihusuyo Tanganyika, huku wakati huo huo, Zanzibar iking'ang'ania mambo yake yenyewe, na kudai ya ziada toka upande wa pili.

Wewe katika mada yako umeshikilia hicho kipande kidogo tu cha IGA na DP World.
 
Nilikuelewa toka mwanzo, nilitaka tu kukupanua akili uone kuwa hiyo DP World ni kipande tu cha matatizo mengi yanayo sababishwa na hilo moja tu la uTanganyika kupotea.

Mwabukusi aliweka wazi toka mwanzo kuhusu hili.

Kwa hiyo unakosea kudhani kwamba kwa IGA kudhibitiwa, ndiko kuwe mwisho wa kero nyingi nyinginezo zinazohusu muundo wa muungano tulionao sasa; unao waruhusu akina Samia toka Zanzibar kuja kuamua maswala yote yaihusuyo Tanganyika, huku wakati huo huo, Zanzibar iking'ang'ania mambo yake yenyewe, na kudai ya ziada toka upande wa pili.

Wewe katika mada yako umeshikilia hicho kipande kidogo tu cha IGA na DP World.
Sawa. Hilo la Katiba tuliache kwa leo. Ni jambo pana. Katiba ndiyo roho ya Taifa. Bila katiba hakuna Taifa. Katiba kama ya Marekani ni ile ile ya tangia wapate uhuru kutoka kwenye ukoloni wa Mwiingereza, kinachokuwa kinafanyika ni updates and upgrades kuendana na matakwa ya wakati. Uingereza haina katiba. Wanasema wao ni a civilized society hawahitaji mwongozo wa Katiba kutunga sheria zinazofaa kwani Katiba ni mwongozo tu (guideline) ya kuzuia kutunga sheria zisizowafaa wananchi wake.

Hivyo tuliache kwanza. Serikali iendelee na mpango wake wa kutoa elimu ya kuhusu katiba ya nchi. Na sisi hapa JamiiForums tutafanya mchakato wa vipande pande bila papara, ushabiki au jaziba. Lengo ni kupata upgrade inayoendana na wakati wa sasa.
 
Mikataba ya hadhi ya IGA (Intergovernmental Agreement) au BIT (Bilateral International Treaties) au MIT (Multilateral international Treaties) ni lazima ziendane na sheria za nchi husika vinginevyo ni null and void de novo.

Hivyo kwa kuwa mkataba kati ya Dubai Emirate na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ulikuwa unapingana na sheria yetu ya Natural Wealth And Resources Permanent Sovereignty Act No. 15 of 2017, ili kuwa valid ulihitaji Tanzania kufanya mabadiliko ya sheria yake hiyo kuondoa bandari zetu (maritine spaces) kwenye orodha ya Natural Wealth and Natural Resources za nchi yetu.

Ndiyo maana serikali ilikuwa imepeleka musuada bungeni wa kufanyia marekebisho sheria hiyo inayozuia mkataba wa DP-WORLD kutekelezeka. Bahati nzuri baada ya kelele nyingi za Watanzania serikali iliondoa musuada huo na hivyo kuufanya mkataba huo wa IGA kuwa batili.

Akina Dr Slaa na wenzake wanajifanya hawaelewi jambo hili kwamba hiyo IGA haipo, ilishatupwa technically kisheria kwenye dustbin. Kilichopo ni hizi HGA, Concession Contracts and Lease Agreements. Kwa maelezo ya serikali mikataba hii imezingatia sana sheria zetu za Natural Wealth and Resources, sheria ya manunuzi, Public Private Parternaship na kadhalika. Serikali itakuwa na undiluted shares za asilima 35% kwenye kampuni hiyo na kadhalika. Kipi sasa akina Dr Slaa wanaendelea kukipigia kelele na kutaka maandamano yasiyo na kikomo nchi nzima?

Dr.Slaa kakimbiwa na huyu Pasta wake au?

View: https://twitter.com/TZWaziriMkuu/status/1723040277084991575?t=L8T3EoaOPjj_3rMSBvY2qw&s=19
 
Uingereza haina katiba. Wanasema wao ni a civilized society hawahitaji mwongozo wa Katiba kutunga sheria zinazofaa kwani Katiba ni mwongozo tu (guideline) ya kuzuia kutunga sheria zisizowafaa wananchi wake.
Hakuna jambo linaloweza kufanyika bila ya 'guideline', (mwongozo); vinginevyo itakuwa 'chaos', hata hapo Uingereza penyewe.
Hao watu leo wakisema hawamtaki 'King'; hana lolote analoweza kuwafanya huo 'king'. Leo hii sisi tukisema hatumtaki Rais, polisi wanajaa barabarani kutulazimisha huyo rais awepo. Tofauti kubwa sana.
Hivyo tuliache kwanza. Serikali iendelee na mpango wake wa kutoa elimu ya kuhusu katiba ya nchi. Na sisi hapa JamiiForums tutafanya mchakato wa vipande pande bila papara, ushabiki au jaziba. Lengo ni kupata upgrade inayoendana na wakati wa sasa.
EEEeeenHEEeeeee!
Nawe unaamini serikali ina mpango wa kutoa elimu ya miaka mitatu kuhusu katiba! Inanibidi nicheke tu kuhusu ujinga wa namna hii.

Kama ninakuelewa vizuri, maana yako ni kwamba hakuna mahitaji ya Katiba Mpya. Iliyopo inafaa ila ifanyiwe viraka hapa na pale!

Maoni yangu ni kwamba hiyo iliyopo ni mbovu kabisa, haihitaji kuwekwa viraka.

Najuwa kwa nini CCM wanalikwepa sana hili swala la Katiba Mpya. Sababu yenyewe ni muundo wa muungano. Hili linawapa shida sana CCM.
 
Mikataba ya hadhi ya IGA (Intergovernmental Agreement) au BIT (Bilateral International Treaties) au MIT (Multilateral international Treaties) ni lazima ziendane na sheria za nchi husika vinginevyo ni null and void de novo.

Hivyo kwa kuwa mkataba kati ya Dubai Emirate na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ulikuwa unapingana na sheria yetu ya Natural Wealth And Resources Permanent Sovereignty Act No. 15 of 2017, ili kuwa valid ulihitaji Tanzania kufanya mabadiliko ya sheria yake hiyo kuondoa bandari zetu (maritine spaces) kwenye orodha ya Natural Wealth and Natural Resources za nchi yetu.

Ndiyo maana serikali ilikuwa imepeleka musuada bungeni wa kufanyia marekebisho sheria hiyo inayozuia mkataba wa DP-WORLD kutekelezeka. Bahati nzuri baada ya kelele nyingi za Watanzania serikali iliondoa musuada huo na hivyo kuufanya mkataba huo wa IGA kuwa batili.

Akina Dr Slaa na wenzake wanajifanya hawaelewi jambo hili kwamba hiyo IGA haipo, ilishatupwa technically kisheria kwenye dustbin. Kilichopo ni hizi HGA, Concession Contracts and Lease Agreements. Kwa maelezo ya serikali mikataba hii imezingatia sana sheria zetu za Natural Wealth and Resources, sheria ya manunuzi, Public Private Parternaship na kadhalika. Serikali itakuwa na undiluted shares za asilima 35% kwenye kampuni hiyo na kadhalika. Kipi sasa akina Dr Slaa wanaendelea kukipigia kelele na kutaka maandamano yasiyo na kikomo nchi nzima?

Kina Dr Slaa ni wapuuzi, wanatikisa kiberiti kama kimejaa. Jibu chepesi ni kuwa kama kila nchi ina natural wealth sovereignty yake hapo tayari zimejicancel out. Mfano halisi ni bomba la mafuta Uganda hadi Tanga tutumie natural wealth sovereignty ya nani? Mafuta yanachimbwa Uganda yanaliwa China kupitia Tanzania hela ni ya Wafaransa.
 
Kina Dr Slaa ni wapuuzi, wanatikisa kiberiti kama kimejaa. Jibu chepesi ni kuwa kama kila nchi ina natural wealth sovereignty yake hapo tayari zimejicancel out. Mfano halisi ni bomba la mafuta Uganda hadi Tanga tutumie natural wealth sovereignty ya nani? Mafuta yanachimbwa Uganda yanaliwa China kupitia Tanzania hela ni ya Wafaransa.
Kuhusu bomba la mafuta la kutoka Uganda hadi bandari ya Tanga jibu lake ni hili hapa:

- Mafuta ni natural wealth/ resource ya wananchi wa Uganda. Ni mali yao ya asili waliyopewa na Mwenyezi Mungu. Ili waweze kunufaika nayo inabidi waichimbe (extract). Wakishaipata wataitumia nchini mwao na nyingine wataiuza kwa nchi hitaji hususani za Tanzania na Ulaya, wapate pesa ya nje.
  • Kwa kuwa Uganda hawana utalaam wala nyezo za kuyachimba hayo mafuta yao kwa sasa, wameajiri kampuni ya Ufaransa kwa mkataba fulani kufanya huo uchimbaji (diggers). Wafaransa hawajamilikishwa hayo mafuta. Wao ni vibarua tu vya kuyachimba.
  • Pia kwa kuwa Mwenyezi Mungu hakuipa Uganda maritime space (bandari), ili iweze kusafirisha hayo mafuta ilituomba watumie sehemu ndogo ya bandari yetu ya Tanga na sehemu ndogo ya ardhi yetu kupitishia hilo bomba lake. Tukakubali na kuwekeana mkataba ambao tutanufaika kwa kulipwa USD 12 kwa kila pipa la mafuta yanayopita kwenye natural wealth yetu ya hiko kipande kidogo cha bandari ya Tanga na hiko kipande kidogo cha ardhi walichopitisha bomba lao.
Hivyo kwenye huo mradi huo, natural wealth sovereignty ya mafuta ni ya Uganda na ile ya bandari ya Tanga na ardhi linamopita bomba ni ya Tanzania.
 
Back
Top Bottom