Dkt. Slaa: Niliudhika kwa maneno ‘Mbowe si gaidi’, nyie ni nani mpaka kusema siyo gaidi? Ataka wananchi wanyamaze Mahakama ifanye kazi yake

Dkt. Slaa: Niliudhika kwa maneno ‘Mbowe si gaidi’, nyie ni nani mpaka kusema siyo gaidi? Ataka wananchi wanyamaze Mahakama ifanye kazi yake

Keshapoteza mvuto . Hata kesi zilizopo ICC watu wanazinzunguma.DR Slaa una haki ya kusema kusema Mbowe ni zaidi. Ni mahakama tu inayoweza kuthibitisha kama ni zaidi au sio gaidi
 
Kila mtu aliyetoka CDM mlisema ana siri nyingi sana za chama. Lijualikali alitangaza utayari wake wa kutoa ushahidi kuhusu maovu ya CDM na Mwenyekiti wake. Bado tunasubiri. Mnachosha sana.

Amandla...
Tulimpokea Katibu Mkuu Mashinji hakuwa na jipya itakuwa Lijualikali kwani ni maneno tuu wamekuja kutujazia wingi huku ccm
 
Na Jacqline Lema

Katibu Mkuu Mstaafu wa CHADEMA, Dkt. Wilbrod Slaa ambaye mpaka sasa pengo lake ndani ya chadema halijazibika ameamua kuwaondolea uvivu wafuasi wa chadema wanaoingilia uhuru wa Mahakama kwa kudai Mbowe si Gaidi.

Kwenye mahojiano maalum Nguli huyo wa siasa na Mbobezi wa siasa za upinzani ameshangaa Wanachadema wanavyolifanya suala la Mahakama kama suala la kisiasa na hasa wanaposhinikiza majaji kufanya maamuzi ya upande wao.

"Mimi huwa sizunguki niliudhika tangu siku ya kwanza nilipoona maneno kuwa Mbowe si Gaidi wao (chadema) ni kinanani mpaka waseme Mbowe si gaidi tena katika suala ambalo liko Mahakamani " Amesema Dkt. Slaa

Kauli hii nzito ya Dkt. Slaa inastahili kupongezwa na kila mtu anayepigania na kulinda uhuru wa Mahakamana Tanzania na Dunia nzima, ni aibu kwa mtu yeyote kuingilia uhuru wa Mahakama.

Wanasiasa aina ya Dkt. Slaa hasa kutokea upinzani huwa wanakuaga wachache sana kwa sababu ya uwezo wao wa kueleza ukweli, ndiyo maana mpaka sasa bado hajatokea ndani ya chadema kila siku wanafanya kazi ya kubadilisha Makatibu Wakuu.
7c65d27d-1b94-4767-b457-d3e8071ecba0.jpg
 
Dr. Slaa ni Moja ya watu wanaochukizwa na wananchi kumtetea Mbowe: amedai anakwazika akisikia watu wanasema Mbowe Siyo Gaidi huku akitaka mahakama iachwe ifanye kazi yake.
Slaa is irrelevant now ; alisha katwa mkia na JIWE na Mke amemkimbia!!! Iliyobaki arudi kwao akalime, asijiingize kwenye siasa za Chadema tena!!!
 
Mbali na kuwa wengi wanavielimu vya vyuo, ila vichwani ni hamnazo tuu,

Unamnunua na kumtusi mtu anaposimama kwenye ukweli? Ujinga tupu

Wimbo wa Mbowe si Gaidi, Nani imempa uahueni nafsini mwake?

Ni miezi sasa huo wimbo unaimbwa, mbona bado yuko lupango bwana Mbowe?
Poleni wachawi,
fukuto linapoongezeka mtajikuta mwazidi kujianika. Kama walivyofanya makaburu SA kwa Mandela, Chifu Hangaya na Kamanda Zero ndio walianza jaribu kuishawishi dunia kabla hata ya kesi yao 'kubumba' kuanza. Kama hamkukereka wakati ule unashangaza sijui mwalia sasa hivi.
Makaburu hawakuwahi kupata amani baada ya kulazimisha kifungo cha Nelson Mandela.
 
Aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA, Balozi Dkt. Wilbrod Slaa amekiri kuudhika na maneno kuwa 'Mbowe si gaidi' ambayo hutolewa na baadhi ya wananchi kuhusu kesi inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe. Amesema wananchi wanatakiwa kuiachia mahakama ambayo ndio chombo cha haki.


Hili ni hizi kama mengine,limejaa mvinyo kwenye mtumbo wake,sasa lazima lilambe matapishi
 
Kila mtu aliyetoka CDM mlisema ana siri nyingi sana za chama. Lijualikali alitangaza utayari wake wa kutoa ushahidi kuhusu maovu ya CDM na Mwenyekiti wake. Bado tunasubiri. Mnachosha sana.

Amandla...
Dr. Slaa
Dr. Mashinji hawa wote walikuwa watendaji wakuu wa CDM, awanajua mikakati yote ya siri iliyo kuwa ikiratibiwa na Mbowe dhidi ya Serikali.
 
Inabidi afumbe macho asiione Mbowe siyo gaidi". Au azibe masikio asisikie mzee mnafiki sana huyu.
 
Tangu atemwe ubalozi kimya kimya , naona njaa imezidi anatafuta tena uteuzi kwa fujo maana kwa umri wake kuwa tena waiter kule ulaya imekua ngumu, muacheni apambane na tumbo lake , maana hata mke walimchukulia wajuba baada ya kuona mzee show sio show anatia huruma sana kimsingi. Ila kuna jamaa yangu Mkatoliki anasema ndio inakuaga hivyo mapadili wote walioasi mwisho wake unakuaga sio mwema
 
Kauli aliyoitoa Balozi Mstaafu ndugu Dr Slaa , YA KUCHUKIZWA NA KAULI ZA MBOWE SIO GAIDI , kama alivyonukuliwa na vyombo vya habari , haiwezi kuachwa bila kujadiliwa .

Madai kwamba wadau hawapaswi kusema MBOWE SIO GAIDI eti kwa vile suala hilo liko Mahakamani , ni hoja Mufilisi isiyo na Mashiko yoyote , kwanza Slaa hajatuambia sisi tunaosema MBOWE SIO GAIDI kama tumevunja sheria yoyote ya nchi yetu , ameamua tu kusema kwa vile yeye ni miongoni mwa wanaokesha kuhakikisha Mbowe anateswa kwa lengo la kulipa visasi visivyo na tija yoyote , Dr Slaa kwa kushirikiana na Askofu Gwajima ndio waliomwingiza Edward Lowassa Chadema ( yeye mwenyewe amewahi kukiri hadharani) , sasa hii chuki ya yeye kukosa nafasi ya kugombea Urais ajilaumu yeye mwenyewe na Gwajima wake , pamoja na kwamba mengi yalitokea wakati ule , ikiwemo Dr Slaa kupitishwa mlango wa uani ili kuingia Hotel Serena kwa lengo la Kutukana Chadema na Lowassa baada ya kuahidiwa ubalozi , leo DR SLAA , SUMAYE , GWAJIMA na LOWASSA wote kwa pamoja wako CCM ! ( video za matusi yale na njia alizopitishwa kuingia serena kwa msaada wa Mwakyembe bado zingalipo )

Haya ndio malipo ya Dr Slaa kwa CHADEMA , chama kilichomuokota mitaani baada ya kunyimwa ubunge na CCM na hatimaye kumpandisha chati hadi kufikia UKATIBU MKUU na kupewa nyumba ya kuishi .

Bali wachunguzi wa Mambo wanadokeza kwamba haikuwa bahati mbaya kwa Dr Slaa kutoa kauli ya kikatili kama hii , AMELENGA KUFURAHISHA WATAWALA ILI AAMBULIE UENYEKITI WA BODI FULANI kama wanavyoambulia wastaafu wenzake .
 
Aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA, Balozi Dkt. Wilbrod Slaa amekiri kuudhika na maneno kuwa 'Mbowe si gaidi' ambayo hutolewa na baadhi ya wananchi kuhusu kesi inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe. Amesema wananchi wanatakiwa kuiachia mahakama ambayo ndio chombo cha haki.

“Katika masuala yaliyoko mahakamani ninaona kwanza kuna sura inatumika, kwenda kule Mahakamani kama sehemu ya siasa kitu ambacho mimi sikubaliani nacho.

“Hivyo sijaenda kwa kuwa ni kitu ambacho sikubaliani nacho, sikubaliani na principal ambayo inatumika, mnaenda kule kisha mnaanza kujipiga picha na mpo kwenye mitandao, hiyo ni siasa, mimi sichezi hizo siasa.

“Mimi nikiamua kumtembelea Mbowe nitaenda nyumbani kwake, sitaki kufanya kitendo cha Mbowe kuwa gerezani kuwa siasa, kama ni kumuombea nitauombea kwa nafsi yangu.

“Niliudhika tangu siku ya kwanza na yale maneno ‘Mbowe si gaidi’, nyie ni nani mpaka kusema Mbowe siyo gaidi?

“Wanatakiwa kuachia chombo cha haki kitoe maamuzi siyo wananchi.

“Lakini sina chuki na Mbowe wala sina uadui, nimeshakutana na Mbowe mara kadhaa airport, tukakumbatiana, tukabadilishana namba japo hakuna aliyempigia mwenzake,” anasema DK SLAA.

Source: MwanaHalisi

NANI ALIYEMWAMBIA TUPO KUFANYA MAMBO YANAYOMFURAHISHA YEYE? JINGA KABISA HILI LICCM
 
Back
Top Bottom