Katibu Mkuu Mstaafu wa CHADEMA, Dkt. Wilbrod Slaa ambaye mpaka sasa pengo lake ndani ya chadema halijazibika ameamua kuwaondolea uvivu wafuasi wa chadema wanaoingilia uhuru wa Mahakama kwa kudai Mbowe si Gaidi.
Kwenye mahojiano maalum Nguli huyo wa siasa na Mbobezi wa siasa za upinzani ameshangaa Wanachadema wanavyolifanya suala la Mahakama kama suala la kisiasa na hasa wanaposhinikiza majaji kufanya maamuzi ya upande wao.
"Mimi huwa sizunguki niliuzika tangu siku ya kwanza nilipoona maneno kuwa Mbowe si Gaidi wao (chadema) ni kinani mpaka waseme Mbowe si gaidi tena katika suala ambalo liko Mahakamani " Amesema Dkt. Slaa.
Kauli hii nzito ya Dkt. Slaa inastahili kupongezwa na kila mtu anayepigania na kulinda uhuru wa Mahakamana Tanzania na Dunia nzima, ni aibu kwa mtu yeyote kuingilia uhuru wa Mahakama.
Wanasiasa aina ya Dkt. Slaa hasa kutokea upinzani huwa wanakuaga wachache sana kwa sababu ya uwezo wao wa kueleza ukweli, ndiyo maana mpaka sasa bado hajatokea ndani ya chadema kila siku wanafanya kazi ya kubadilisha Makatibu Wakuu.
View attachment 2134036
Sent from my SM-A325F using
JamiiForums mobile app