dalalitz
JF-Expert Member
- Sep 6, 2013
- 3,423
- 1,987
Mkuu inaelekea una ukaribu kama si wa kinasaba basi niwakimaslahi na huyo bwana mkubwa,Hiyo clip ilikatwa kwa malengo ila Kuna clip ambayo aliendelea kufafanua vizuri hadi spika akaridhika.
Si kwa utetezi huo aisee😀
Ile Clip ipo wazi kama uchi-wa-mbuzi kuwa bwana mkubwa ameshindwa kufafanua
kwa Lugha rahisi kitu ambacho hata mimi nilieishia dalasa la tatu B nimegundua kuna shida.
Kumbuka yeye ni Dakitari mbobevu kwenye nyanja yake.
Kingine;
Huko kuridhika kwa Kiti,
Haingii akili kuwa kulifanyika muda ule labda wawe wamefafanuliana nje ya Ukumbi na hata ikiwa hivyo
unajua kuwa ubabaishaji ule umeshaingia kwenye kumbukumbu za mjadala rasmi wa Bunge?
Ni malizie kukuambia si kila jambo tulifanye Siasa jamani.
Na kwakuwa una MAHABA na mtu au kitu uteteee tu.
Mheshimiwa sana amechemsha.