Dkt. Tulia: Kama wasingeenda Mahakamani ningetangaza nafasi kuwa wazi

Dkt. Tulia: Kama wasingeenda Mahakamani ningetangaza nafasi kuwa wazi

Mkuu Fundi Mchundo , vitu vingine sio vya kuuliza ni kutaka tuu kumuonea Spika. Uchaguzi unasimamiwa
Anaonewa kivipi? Hii ina tofauti gani na suala la vyeti vya kughushi serikalini? Serikali si ndio iliyochukua hatua baada ya kutambua kuwa imedanganywa? Kwa nini haikusema haihusiki na kuachia bodi ya mtihani ndio iwachukulie hatua wakati wakiendelea kufanya kazi? At the very least Spika alipaswa kushirikiana na Chadema kujua ukweli ili kama kuna nyaraka zilighushiwa, wahusika wachukuliwe hatua za kisheria ili wengine wasithubutu kufanya hivyo tena.

Atachukuaje hatua ya kuwanyang'anya ubunge kwa sababu Chadema wamewafukuza kwa kosa la kujipeleka bungeni bila ridhaa yao bila kutaka kujua ofisi yake iliwapokeaje? Mpira uko squarely kwa Spika na sio mtu mwingine. Spika alitakiwa achukue hatua kulinda heshima ya institution ya Bunge ambayo watu wachache wanataka kuiharibu. Suala la uhalali wa utaratibu waliofuata Chadema kuwafukuza wakina Halima kweli halimhusu. Lakini la utaratibu wa kuwapokea bungeni ni la Spika na si mwengine. Spika anapaswa kujiuzuru kama alipokea nyaraka alizojua ni za kughushi na kuzitumia kuwaapisha wakina Halima maana inaonyesha hana integrity anayopaswa kuwa nayo. TAKUKURU nao walitakiwa kujiingiza mapema kabisa.

Lakini sishangai. Boniface Jacob alinyang'anywa umeya kwa barua kutoka "Chadema" iliyomvua uanachama hata baada ya Chadema kusema kuwa haijawahi kuandika barua kama hiyo! Kulikuwa na majaribio ya kuwapa fomu wagombea kutoka "Chadema" ambao Chadema ilisema kuwa hakikuwachagua. Hili nalo ni muendelezo wa mambo kama haya. Halafu mnakazania kuwatetea watu ambao ni dhahiri hawakuingia kihalali bungeni. Kushindwa kwa Spika kuweka wazi nyaraka zilizowasilishwa kuwatambulisha kwake ni ushahidi tosha.

Amandla...

Nguruvi3 JokaKuu
 
Wale wa cuf sababu za kufukuzwa kwao hazikuwa na adhari kwenye utendaji wa Bunge

Chadema iligoma kupeleka wabunge viti maalum, Jambo la viti maalum ni Jambo la kisheria

So wakina mdee walivuliwa uanachama wao Kwa kutiii sheria ya viti maalum


Hapo sasa ndio chadema watafeli hata mahakamani
Ila kunataratibu kwenye vyama zinabidi zifuatwe ili kupokea wabunge wa viti maalumu je zikifuatwa. Siyo mtu yoyote anajipeleka tu bungeni .
 
Ila kunataratibu kwenye vyama zinabidi zifuatwe ili kupokea wabunge wa viti maalumu je zikifuatwa. Siyo mtu yoyote anajipeleka tu bungeni .

Kwani wao ni wajinga mpaka wajipeleke Tu? Mbona hawakujipeleka after tume Tu kutangaza
 
Mkuu P , kuna hoja moja tusaidie kuielewa ili tusimuonee Spika.

Spika Tulia kasema asubuhi ya jana, 'kuna shauri lipo mahakamani hatawazuia COVID19 bungeni''
Jioni Jaji Mgeta anatoa kauli ya mahakama ya 'status quo' kwa Wabunge

Swali, Spika alipata wapi taarifa za COVID19 kwenda mahakamani?
Kuna sheria gani inayomkataza asiwazuie kuingia Bungeni kabla ya 'hukumu' ya mahakama?
Swali la mwisho, je, Tundu Lissu ambaye shauri lake lipo mahakamani ni Mbunge halali?

JokaKuu Fundi Mchundo
Speaker kama gari lililotangulia kituoni katoa hukumu kabla hukumu haijatoka ndio ujuwe nchi hii hakuna mahakama wala haki. Angewafukuza asubuhi na kuwarudisha mchana baana ya hukumu kidogo angeonekana malaika ila kawahi kusoma script.
 
Hapo ndio shida ukisema Chadema walikataa viti maalumu kina Mdee wakaenda kina Mdee ndio nani chama cha siasa? sheria ziko wazi watu wanateuliwa na chama chao sio unajipeleka tu mwenyewe kwenye hili tuweke ushabiki huko hawa na sote tunajuwa nani aliwaweka bila kufuata utaratibu Bunge linatambua Chama sio watu mmoja mmoja. Haya ya CUF na Chadema hakuna tofauti yoyote. Speaker anasema ni jukumu lake kufuatilia kesi mahakamani sio kuletewa hukumu kama wasomi wetu wa sheria wanaongea hivi basi kuna shida kubwa katika nchi hii. Speaker katangaza hukumu kabla mahakama haijatoa hukumu jana kawahi sana Mama sasa anafanya damage control. Kufungua kesi mahakamani haina maana yoyote bila kuwa na hukumu angesubiri hukumu ndio angesema nilikuwa nataka kutangaza nafasi lakini nimepokea hukumu makahakamani kusimamisha ila bahati mbaya katoa hukumu yeye asubihi mahakama ikaleta tu karatasi baadae. Tulia aibu yako kama msomi wa sheria ndio wewe basi tusitegemee miujiza nchi hii sijui utawafundisha nini watoto zako. shame kwa wasomi wetu

Tatizo watu wa mitandaoni ujuaji ni mwingi
 
Acheni kuchoche chuki kwenye Taifa.

Hiyo Miaka yote uliwahi kuona Polisi wanaingia mpaka kwenye vyumba vya Kupiga kura na kubeba masanduku.
2020 Polisi wengi walijitokeza hadharani na kusema kuwa wao ni CCM na wengine mpaka kuchukua Fomu za kugombea Ubunge ili hali katiba inakataza.Ingekuaje kama wangine wangegombea kupitia Vyama vya upinzani?
Watu waliporwa fomu za uchaguzi mchana kweupe?
Watu wanaenguliwa nchi nzima.
Mawakala wanazuiliwa kuingia nchi nzima.
Watu walikatazwa kujumlisha kura zao . Watu walikatazwa kutumia simu.
Mitandao ilizimwa nchi nzima. Halafu unalinganisha na chaguzi nyingine.
Yaani unalinganisha uporaji wa ""Panya Road "" na wizi wa "" Tuma kwenye Namba hii""[emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Wizi wa Kura ulikuwepo lakini sio kama ule wa Panya Road wa 2020. Watu wakikata mapanga na kuuawa kila mahali. Mpaka Mgombea wa Chadema ananyima Kibali Cha kuruka na Helkopta halafu unahalalisha ushetani huo kweli.
Maisha ni mapito TU hakuna haja ya kufanya mabaya Kwa wengine ili hali kila mtu anataka kutendewa haki.

Ukitaka kujua Maisha ni mapito waangalie wale waliokua ni Vijana awamu zilizopita wakiwa na nguvu za kufanya uhuni wote wanaotaka ,Leo ni wazee wanatembea Kwa kudemadema. Wengine Wamebaki na kiburi TU lakini hawana furaha.

Haki huinua Taifa. Sio kauli ya kupuuzia maana ni kauli ya kinabii.

Hayo ni mambo ya kawaida Kwa siasa za Africa hakuna jipya hapo
 
Screenshot_20220517-070433.jpg
 
Anaonewa kivipi? Hii ina tofauti gani na suala la vyeti vya kughushi serikalini? Serikali si ndio iliyochukua hatua baada ya kutambua kuwa imedanganywa? Kwa nini haikusema haihusiki na kuachia bodi ya mtihani ndio iwachukulie hatua wakati wakiendelea kufanya kazi? At the very least Spika alipaswa kushirikiana na Chadema kujua ukweli ili kama kuna nyaraka zilighushiwa, wahusika wachukuliwe hatua za kisheria ili wengine wasithubutu kufanya hivyo tena.

Atachukuaje hatua ya kuwanyang'anya ubunge kwa sababu Chadema wamewafukuza kwa kosa la kujipeleka bungeni bila ridhaa yao bila kutaka kujua ofisi yake iliwapokeaje? Mpira uko squarely kwa Spika na sio mtu mwingine. Spika alitakiwa achukue hatua kulinda heshima ya institution ya Bunge ambayo watu wachache wanataka kuiharibu. Suala la uhalali wa utaratibu waliofuata Chadema kuwafukuza wakina Halima kweli halimhusu. Lakini la utaratibu wa kuwapokea bungeni ni la Spika na si mwengine.

Lakini sishangai. Boniface Jacob alinyang'anywa umeya kwa barua kutoka "Chadema" iliyomvua uanachama hata baada ya Chadema kusema kuwa haijawahi kuandika barua kama hiyo! Kulikuwa na majaribio ya kuwapa fomu wagombea kutoka "Chadema" ambao Chadema ilisema kuwa hakikuwachagua. Hili nalo ni muendelezo wa mambo kama haya. Halafu mnakazania kuwatetea watu ambao ni dhahiri hawakuingia kihalali bungeni. Kushindwa kwa Spika kuweka wazi nyaraka zilizowasilishwa kuwatambulisha kwake ni ushahidi tosha.

Amandla...
Mkuu Fundi, kama kungekuwa na ithbati ya Chadema kuandika barua Msajili wa vyama kwa chuki aliyo nayo dhidi ya Chadema asingekaa kimya.
Tume ya uchaguzi (NEC) kwa utendaji wake wa maagizo ya chama tawala wasingekaa kimya

Tuhuma za forgery ni mbaya sana kuliko tuhuma alizoitiwa Pascal Mayalla au CAG Assad, Bunge

Lakini, NEC, Bunge wote kimyaa kana kwamba wamekubali tuhuma za forgery
Kwamba institution hizo hazioni kashfa ya kughushi nyaraka? Real?

Sasa Bunge lina kashfa nyingine, Spika kawaruhusu COVID19 kwa hisia zake asubuhi ya jana
Hukumu ya mahakama imetoka jioni, Spika alitoaje kauli ya suala la mahakamani kabla?
 
Speaker kama gari lililotangulia kituoni katoa hukumu kabla hukumu haijatoka ndio ujuwe nchi hii hakuna mahakama wala haki. Angewafukuza asubuhi na kuwarudisha mchana baana ya hukumu kidogo angeonekana malaika ila kawahi kusoma script.
Jaji Mgeta aliomba muda wa kupitia shauri mchana na kutoa tamko jioni , wakati huo huo Spika wa Bunge Tulia Akson alishajua shauri limeamuliwaje asubhi ya siku hiyo

Kuna vilevi duniani lakini ulevi wa madaraka ni ulevi mbaya sana.
Anayefanya haya tunaambiwa ni mcha mungu sana kwa imani ana PhD na ni Mwalimu wa sheria wa chuo kikuu UDSM, na alishakuwa naibu mwanasheria mkuu wa nchi ya Tanzania, sasa anasimamia mhimili wa kutunga sheria zinazohusu watu milioni 55.
 
Yes coz chama kilivunja sheria ya kutotiii kupeleka wabunge wa viti maalum, Kwa sababu zao binafsi

Acha uongo, chama kisipopeleka wabunge kinapoteza hiyo haki. Hakuna Cha kuvunja sheria. Ndio maana serikali iliamua kuingia na kuwasupport kina Halima maana ilijua chadema haitwapeleka Bungeni.
 
Jaji Mgeta aliomba muda wa kupitia shauri mchana na kutoa tamko jioni , wakati huo huo Spika wa Bunge Tulia Akson alishajua shauri limeamuliwaje asubhi ya siku hiyo

Kuna vilevi duniani lakini ulevi wa madaraka ni ulevi mbaya sana.
Anayefanya haya tunaambiwa ni mcha mungu sana kwa imani ana PhD na ni Mwalimu wa sheria wa chuo kikuu UDSM, na alishakuwa naibu mwanasheria mkuu wa nchi ya Tanzania, sasa anasimamia mhimili wa kutunga sheria zinazohusu watu milioni 55.
Ni huzuni kwa kweli kwa Taifa na nasema hili kwa uchungu nikiona tunashindwa kuheshimu sheria zetu wenyewe na wanaovunja ndio viongozi wakubwa waliopewa dhamana. Mimi niseme wasi sina maslahi yoyote katika hili siko CCM wala Chadema na sijawahi kupiga kura maisha yangu yote ila inauma ukiona sheria zinavunjwa kwa makusudi kwa kiburi tu kama sheria hizi mbaya wana uwezo wa kuzibadilisha hata kama mabadiliko mabaya lakini tutaheshimu ni sheria lakini sio kuona watu wote wajinga hili ndio linaumiza kuliko yote.
 
Wanatii sheria ya viti maalum bila ridhaa ya chama?
Chama hakijawapeleka huko viti maalum kisha wao wanatii sheria ya viti maalum!
Very strange!

Nchi imepitia mengi!

Nasikitika Kwa sababu credibility yao machoni pa jamii imeharibika!
Watetea matumbo!
 
MIMI KAZI YANGU NI MOJA TU - SPIKA TULIA AKSON

Spika wa Bunge la Tanzania Mhe. Tulia Ackson Tulia Ackson amezungumza na wanaHabari kuhusu uamuzi wa kuwafukuza Bungeni Wabunge 19 wa CHADEMA Halima Mdee na wenzake. Amesema yeye anasubiri Maamuzi ya Mahakama.

View attachment 2227166
Hili somo la history kuwa binadamu alianza kama sokwe linawezekana kukawa kuna kiukweli fulani........
 
Tulia ukilala unasali kwa roho na kweli? Hujajifunza tu ya Job? Cheo ni dhamana na WAKATI SI MILELE!
Yuko wapi Job leo hii
Yuko wapi Sabaya
Yuko wapi Bashite....
Yako wapi mafirauni yote yaliyotamba kwa nyakati zao?
Wote hao, sasa hivi wanaweza kuwa ku
Wa napelekewa moto huku wakiwa wameufiata...Mavi ya kale....hayanuki!!
 
Kama uchaguzi ulikuwa batili. Mwenyekiti anaendaje kuonana na Rais batili, mnaandika barua kwa bunge batili, kwa muktadha huu itakuwa na nyie ni batili

Mwenyekiti kaenda kuonana na rais ili kuweka mazingira vizuri baada ya rais aliyeendesha uovu na uharibifu wa uchaguzi kuelekea motoni. Chama kimeandika barua kwa bunge la majizi ya kura kuwa wabunge wa Covid sio wanachama wake tena.
 
Mkuu Fundi, kama kungekuwa na ithbati ya Chadema kuandika barua Msajili wa vyama kwa chuki aliyo nayo dhidi ya Chadema asingekaa kimya.
Tume ya uchaguzi (NEC) kwa utendaji wake wa maagizo ya chama tawala wasingekaa kimya

Tuhuma za forgery ni mbaya sana kuliko tuhuma alizoitiwa Pascal Mayalla au CAG Assad, Bunge

Lakini, NEC, Bunge wote kimyaa kana kwamba wamekubali tuhuma za forgery
Kwamba institution hizo hazioni kashfa ya kughushi nyaraka? Real?

Sasa Bunge lina kashfa nyingine, Spika kawaruhusu COVID19 kwa hisia zake asubuhi ya jana
Hukumu ya mahakama imetoka jioni, Spika alitoaje kauli ya suala la mahakamani kabla?
Mkuu hii inasikitisha mno. Nawashangaa watu wanaoona tatizo kubwa ni utaratibu uliotumiwa na Chadema kuwafukuza wakina Halima wakati mtu hata kuinsinuate kuwa institution kama Bunge ni corrupt ni jambo la hatari mno. Nilitegemea Bunge lipigane kufa na kupona kujisafisha kwenye hizi tuhuma.

Dokta amejiharibia kwenye hilo. Ndio ubaya wa kuchagua upande wakati mtu unapaswa kuwa neutral and beyond reproach. Namkumbuka Spika wa House of Commons John Bercow alivyokuwa ana hakikisha kuwa serikali haiburuzi upinzani ingawa mwenyewe alikuwa Conservative.

Amandla....
 
Hii nchi imejaa wapumbavu wengi z sana!
Ulitaka raisi akae hotel ya uswahilini huko new York?

Halafu nyie washamba mnateseka sana for nothing. Hapa Tanzania tu kuna hotel zina bei kubwa kuliko hiyo. Kuna ubaya gani?
Chawa kazini
 
Back
Top Bottom