Dodoma: Bunge lapitisha azimio la kuunga mkono mkataba wa Tanzania na DP World

Dodoma: Bunge lapitisha azimio la kuunga mkono mkataba wa Tanzania na DP World

Alikuwa sahihi tu....

Ninakumbuka maneno yake..."Mimi si mwanasiasa....".

Bungeni kuna wanasiasa...
Bungeni kuna siasa.....

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Alifuata nn siasani? Ili uwe balozi nyumba kumi, mtendaji, diwani, mbunge, wazir, Rais ni lazima uwe mwanasiasa!! Je CCM alikua anatafuta nn? C angejitoa ili tujue hakua mwanasiasa? Weka vitu ambavyo ni reasonable!!
 
Bunge linapitisha azimio hili ili kumridhisha nani? Adhabu ya wabunge waliopitisha wote hawa asirudi bungeni mbunge hata mmoja wananchi wawakatae katika uchaguzi mkuu ujao. Huu ndio usaliti mkubwa wa nchi. Nani kawaloga wabunge wetu. Hii mikataba ya aina hii haitaishia kwenye bandari tu itatakiwa isainiwe kwenye miradi mingine pia ambayo kwa hoja kama hii haina ufanisi. Wenye ufanisi ndio hao wanaoingia mikataba na nchi yetu. Fikirieni hao wenye ufanisi watakapokuja na wataalamu wao waliobobea kwenye fani hizo, kuna mwananchi ataambulia post za juu kama si kuishia kufanya vibarua tu, kwa elimu na ujuzi upi kama tu hawa wameshindwa kuleta ufanisi? Duh! Mh, hao wafagiaji na wafanya usafi huenda wakawa na elimu za juu ili kuleta ufanisi
 
Kama uwekezaji utatuwezesha kufikia viwango vya bandari zingine hiyo Iko poa tu! Nchi ya wajinga huliwa na wajanja!

Hawa wote wanaoongoza nchi ni wazee tutaenda nao mavumbini na watoto wetu hawatafanya ujinga ujinga kama wao maana hawamjui Mwalimu Wa butiama Wala mkoloni wanamjua Magu tu and what he did for bongoland!
 
Hivi Bunge letu lina jipya na cha maana kweli ukiondoa compliance ya Katiba? Nina maanisha does it meet objectives of its establishment or it merely the matter of Katiba compliance?
Just a rubber stamp only.

Hivi wewe na akili zako ulitarajia bunge hili la Tz lingekuja na kitu chochote kipya na cha maana kuhusu suala hili????
Seriously???????!!!!?????????
 
DP World itakuza na kuchochea:-
# Kukua kwa sekta za uzalishaji
# Itakuza na kuongeza ajira kwa wazawa;
# Itakuza viwanda vya ndani;
# itaongeza pato la taifa;

CCM kupitia DP World mmeipiga pabaya CDM, ACT, NCCR, CUF, UP, NLD nk. Kwa vyovyote vile CCM lzm wananchi wawaamini tena 2025 - 2030.
Hongera sana SSH Mwenyekiti wa CCM taifa.

Msakila Kabende Msakila
Kakonko.
 
Ngojeni nilie kwanza nitacomment baadaye maana kwa Sasa jinsi nilivyo na hasira na Hawa wabunge wa fisi_emu naweza kutukana kabisa!View attachment 2652751
Pole sana ndugu, Ila hii picha haina uhalisia kwa upande wangu, kama alikuwa anakata mti apate kuni, sasa angepata vipi hizo kuni wakati huo mti ulikuwa unaangukia mtoni? Au alitaka kutuambia nini huyu artist. Ila nimeipenda imefungua akili yangu kutafakari kwa kina kuwa Watanzania hatuna pa kukimbilia, hapa ni kwetu na tupambane kwa akili zetu binafsi. Mwisho wa siku maamuzi ya mwisho ni yako, fanya kazi ulishe familia mengine Mungu atayamaliza.
 
Azimio la Bunge kuhusu Pendekezo la Kuridhiwa Mkataba baina ya Serikali ya Jamhuri ya Mungano wa Tanzania na Serikali ya Dubai kwa lengo la kuanzisha Ushirikiano wa Kiuchumi na Kijamii katika Uendelezaji wa Maeneo ya Bandari Nchini leo Juni 10, 2023.



======

Leo Juni 10, 2023, Bunge la Tanzania linatarajia kujadili mkataba kati ya Serikali na Kampuni ya DPWorld unaodaiwa kutotaja ukomo kuhusu Ushirikiano katika Uendeshaji, Uendelezaji na Uboreshaji wa Bandari zote za Baharini na Maziwa zilizopo Tanzania Bara

Mkataba umeibua maswali ambayo hayajapatiwa ufafanuzi wa kina ikiwemo thamani na muda wa uendeshaji pamoja na sababu za Tanzania kuingia mkataba na kampuni inayotajwa katika kesi za ukwepaji kodi na migogoro katika utekelezaji mikataba huku baadhi ya Nchi zikiikataa kampuni hiyo.

Je, unaufahamu kiasi gani Ushirikiano wa DP-World na Bandari?

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa anawasilisha Pendekezo la Kuridhiwa kwa Mkataba baina ya Serikali ya Jamhuri ya Mungano wa Tanzania na Serikali ya Dubai

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa anawasilisha Pendekezo la Kuridhiwa kwa Mkataba baina ya Serikali ya Jamhuri ya Mungano wa Tanzania na Serikali ya Dubai kwa lengo la kuanzisha Ushirikiano wa Kiuchumi na Kijamii katika Uendelezaji wa Maeneo ya Bandari Nchini, leo Juni 10, 2023

UTOAJI HUDUMA HAUJAFIKIA VIWANGO VINAVYOTAKIWA KIMATAIFA
Prof. Mbarawa amesema: "Pamoja na kuchukua hatua mbalimbali za maboresho ya Bandari ya Dar es Salaam, bado ufanisi katika utoaji Huduma za haujafikia viwango vinavyotakiwa kimataifa.”

“Hali ya sasa ya utendaji imeendelea kuwa ya kiwango cha chini ikilinganishwa na Bandari shindani kikanda. Kwa mfano, wastani wa meli kusubiri nangani kwa Bandari ya Dar es salaam ni Siku 5 ikilinganishwa na Siku 1.25 kwa Bandari ya Mombasa na siku 1.6 kwa Bandari ya Durban.”

"Ufanisi mdogo wa Bandari ya Dar umetokana na changamoto ikiwemo kukosekana kwa Mifumo ya kisasa ya TEHAMA, maeneo ya kutosha ndani na nje ya Bandari kwa ajili ya kuhifadhia shehena, Maegesho ya Meli, mitambo ya kutosha na ya kisasa ya kuhudumia shehena ambayo ina gharama kubwa ya Uwekezaji.”

“Meli kutumia muda mrefu kupakia na kupakua shehena gatini kwa wastani wa Siku 5 ikilinganishwa na Siku 1 inayokubalika Kimataifa, pamoja na Meli kubwa kutokuja katika Bandari ya Dar kutokana na kuchukua muda mrefu kuhudumiwa

MSINGI WA MKATABA HUU KUENDANA NA MIKATABA
Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa, amesema Mkataba wa DP World kuendesha Bandari utakuwa hai mpaka pale ambapo shughuli za Miradi zitasitishwa au kuisha kwa muda wa Mikataba ya Nchi mwenyeji na Mikataba ya miradi

Amesema "Msingi wa Mkataba huu kuendana na Mikataba ya miradi ni kutokana na kwamba unaweka msingi unaowezesha kuingia na kutekelezwa kwa Mikataba 10 Nchini."

KAMPUNI YA DP WORLD INA UZOEFU WA KUENDESHA BANDARI BARANI AFRIKA
Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi amesema Kampuni ya DP World ina uzoefu katika uendeshaji wa shughuli za Bandari Barani Afrika, Asia, Ulaya na Amerika ya Kaskazini na Kusini

Amesema "Baadhi ya Kampuni zilizowasilisha nia ya kuwekeza Bandarini hazina wakati Kampuni ya DP World inaendesha takriban Bandari 6 Afrika na Bandari zaidi ya 30 Duniani kote kwa ufanisi mkubwa.”

DP WORLD INATAKIWA KUENDELEZA AJIRA ZA WATUMISHI WALIOPO
Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa amesema “Uwepo wa ajira za Watanzania hususani Watumishi wa Bandari ya Dar es Salaam ni kipaumbele kikubwa cha Serikali sio tu katika Azimio hili bali katika kila aina ya uwekezaji ambao Nchi itaufanya.”

Amesema “Ibara ya 13 ya Mkataba huu inaitaka DP World kuendeleza ajira za Watumishi wote waliopo, kuwaajiri Watanzania pamoja kuwaendeleza kitaaluma.”

TAUHIDA: KIONGOZI ANAYETAMKA KAULI ZA UBAGUZI TUNAMSHANGAA SANA

Mbunge Tauhida Gallos Nyimbo amesema “Nikimuona kiongozi anayewaongoza watu anatamka kauli ya kibaguzi tunamshangaa sana, mimi natokea Songea, mama yangu ni Mzaramu lakini ni Mbunge wa #Zanzibar.”

Ameongeza “Serikali haikatai kukosolewa, ikikosolewa inafanya uboreshaji zaidi.”

MDEE: MKATABA WA DP WORLD UMETAJA VITU KIJUMLAJUMLA
Akizungumzia mkataba wa #Tanzania na Kampuni ya #DPWorld, Mbunge #HalimaMdee amesema “Tuna nafasi ya kubadilisha baadhi ya vitu katika Mkataba huu lakini najua hatutabadilisha

Ameongeza “Kama Mkataba huu unagusa Mtwara, Tanga, Mwanza, Dar es Salaam na Kigoma kwani usizungumzwe kwa mapana yake? Tukiupitisha unaenda kuwa mkataba wa Kimataifa, chochote ambacho kimetajwa kijumlajumla kuhusu Bandari kitahusika.”


BOFYA HAPA KUSOMA: Maoni ya Kamati ya Pamoja Kuhusu Azimio la Bunge Kuridhia Makubaliano Kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali Ya Dubai Kuhusu Ushirikiano wa Kiuchumi na Kijamii Kwa Ajili ya Uendelezaji na Uboreshaji Wa Utendaji Kazi wa Bandari Tanzania la Mwaka 2023

RASMI: BUNGE LAPITISHA AZIMIO LA KUUNGA MKONO MKATABA WA TANZANIA NA DP WORLD


Bunge limepitisha mkataba kuhusu Ushirikiano wa Tanzania na Kampuni ya Dubai ya DPWorld katika Uendeshaji, Uendelezaji na Uboreshaji wa Bandari zote za Baharini na Maziwa zilizopo Tanzania Bara, ikiwemo Bandari ya Dar es Salaam

Sehemu ya Azimio hilo imesomeka, "kwa kuzingatia manufaa ambayo Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itayapata kutokana na Mkataba huu, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Mkutano wake wa 11 na kwa mujibu wa Ibara ya 63(3)(e) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, linaazimia kuridhia Makubaliano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Dubai Kuhusu Ushirikiano wa Kiuchumi na Kijamii kwa ajili ya Uendelezaji na Uboreshaji wa Utendaji Kazi katika Bandari Tanzania"

Mkataba huo uliibua maswali kutoka kwa Wananchi ikiwemo thamani na muda wa utekelezaji

Bunge limepitisha kwa 100% azimio la "kubinafsisha" bandari zote nchini kwa kampuni ya DP World, milele. Hongereni sana.!.

Mchezo umeisha kazi imeisha ,bandari zote zimebinafsishwa huko kwenye mjadala wa mkataba kumzidi akili mzungu au mwarabu sahau,alifanya hayo hayo magufuli kwenye mambo ya makinikia akatuahidi Noah kila mwananchi tuliziona ? Na trion 300+ tuliziona? Baadae kabudi akaja kusema ule mkataba au mazungumzo ilikuwa uongo.
 
Hakuna cha bure kuna Quid Pro Quo; kama kuna uwezekano wa watu kuvuna shamba la bibi kwa bei chee watafanya hivyo ukizingatia walamba asali hio Quid Pro Quo sio kwa manufaa ya Taifa bali kwa manufaa yao...., yaani ni wale ambao tunaweza kusema wana - Cut Their Noses to Spite their Faces, Nadhani wakimaliza huku hata Serengeti itakwenda....
 
Haya maandamano yanayofanywa na mashabiki wa yanga, wangeelekeza kuiondoa CCM tungekuwa mbali sana. Tate Mkuu unasemaje maana pia ni yanga lia lia huku CCM wakitupiga
Dah! Yaani tupo kama misukule vile. Watu hawa hawa ukiwaambia kesho wajitokeze kuandamana kudai Katiba Mpya ya wananchi, au kuishinikiza serikali kuacha kusaini mikataba ya Kimangungo; kamwe huwezi kuona mtu akijitokeza.
 
Potential side effects of giving Tanzania ports to DP World:

Increased foreign control over Tanzania's economy: DP World is a foreign company, and the deal gives it control over a major strategic asset in Tanzania. This could lead to increased foreign control over Tanzania's economy, which could have negative consequences for Tanzania's sovereignty and development.

Job losses: The deal could lead to job losses at the Port of Dar es Salaam, as DP World is likely to replace some Tanzanian workers with its own employees. This could have a negative impact on the Tanzanian economy and society.

Increased prices: DP World may raise prices for port services, which could make it more expensive for Tanzanian businesses to import and export goods. This could make Tanzanian goods less competitive in the global market, and it could also lead to higher prices for consumers.

Environmental damage: DP World's operations could cause environmental damage, such as pollution and the destruction of marine life. This could have a negative impact on Tanzania's environment and tourism industry.
 
Naunga mkono mkataba huu, ni mkataba wa kimkakati, kuna vifungu viwili virekebishwe

1: Muda, labda uwe wa miaka 33, baada ya miaka 33 ikiwa mkataba utaenda vizuri tuongeze tena muda.
2: Kifungu cha kuvunja mkataba, kuwe na provision ikiwa kuna sbb kubwa na ya msingi mkataba tunaweza kuuvunja

Mengine yote ni mazuri, manufaa ni makubwa sana.

Hongera sana Mh. Rais wetu, Mama Samia
 
Kwahiyo nyie mlitegemea bunge litakataa huo mkataba😃😃 basi mi nilikuwa mbeke ya muda maana nilishajua kitakachotokea
 
Back
Top Bottom