Dodoma: Bunge lapitisha azimio la kuunga mkono mkataba wa Tanzania na DP World

Dodoma: Bunge lapitisha azimio la kuunga mkono mkataba wa Tanzania na DP World

Dhamira yake ilikuwa wazi toka siku ya kwanza,niliona wajomba zetu wakirudi bagamoyo na pwani nilimuona Sultan Jamshid Bin Abdullah akirudi tena kudai eneo lake lililopinduliwa na John Okello,nilijiuliza tunaelekea wapi kama nchi!?
 
Wadau Nawasalimu ktk Jina la TANGANYIKA.Inasemekana SAKATA la BANDARI yetu limekwisha naamini kwa Kupewa DP WORLD ili AIENDESHE.Mie nasema SAFI SANA.Ili tuendelee KUKUSANYA KODI basi Tunatakiwa KUUZA na BAHARI.
20230705_093155.jpg
 
Wadau Nawasalimu ktk Jina la TANGANYIKA.Inasemekana SAKATA la BANDARI yetu limekwisha naamini kwa Kupewa DP WORLD ili AIENDESHE.Mie nasema SAFI SANA.Ili tuendelee KUKUSANYA KODI basi Tunatakiwa KUUZA na BAHARI.View attachment 2678968
Mimi sielewi kitu

Tatizo la DP WORLD ni lipi ikiwa makusanyo ya mapato na ajira zinaongezeka? Nchi nyingine ambayo bandari yake imeuzwa kwa DP WORLD ni ipi? Je, alternative ya DP WORLD ni nani?
 
Kuna msemo wa kiingereza kwamba " the devil is in the details"!

Hii ndo sababu vi.laza wengi hawapendi details kwa sababu wanaogopa kukutana na shetani uso kwa uso!

Tumemsikiliza Profesa Shivji, Profesa Anne Tibaijuka, Dr.Rugemeleza Nshala, Tundu Lissu, Boniface Mwabukusu n.k .
At least naweza kusema hizo ni Big Brains tulizo nazo kama Taifa!

Sasa msitulazimishe sijui kuwasikiliza kina Zembwela, Maulidi Kitenge, Shehe 'Ubwabwa" Mwaipopo, Steve Nyerere , Majaliwa, Mbarawa na hata Sa100!

Hatutaki habari za kwamba wana nia njema na Taifa! Even the way to hell is paved by people with good intention!

Mkataba huo (Bogus Treaty) Rais kama ni msikivu na mwelewa asiusaini na aurejeshe Bungeni na wabunge waache ushabiki wa kiCCM kwani hata mimi ni mwana CCM lakini najua hii Nchi si mali ya CCM wautupilie mbali huo mkataba au kama Mbarawa na team yao wanaupenda watafute Bandari zao wawape hao Waarabu!

Tunachotaka Katiba yetu iheshimiwe, Uhuru wetu kama Taifa uheshimiwe ,sheria zetu zifuatwe na kama kuna haja ya uwekezaji katika Bandari zetu basi sheria za manunuzi zifuatwe na si kuletewa Bogus treaties!

Halafu wanaCCM tuache unafiki kwani ni jana tu hapa mwamba Hayati Rais Magufuli alikuwa akisema TUNAWEZA sote tulishangilia lakini ghafla chini ya Rais Samia HATUWEZI chochote!

Kama binadamu angekuwa anakufa halafu baada ya muda anarudi basi siku Hayati Magufuli anarudi tungeona wanafiki wanaomsifia Rais Samia sasa kuhusu Bandari zetu ambavyo wangemkimbia kwenda kumlaki Magufuli! Hili hata yeye Rais Samia anajua deeply kwamba hajatutendea haki kuwapa Waarabu Bandari zetu kienyeji hivi!

Chini ya CCM yetu, tumeuza madini, mbuga za wanyama, gesi n.k basi sasa tuone aibu kama tumeshindwa kununua tu cranes na systems za kuendesha Bandari tuziache wengine pia waje wakute cha kuuza!

Narudia kusema Mimi ni mwana CCM ila tujue hii Nchi si mali ya CCM!

Kwa hili la Bandari Serikali yetu ya CCM na Bunge la Tulia Ackson zimetutia aibu mbele ya Watanzania wenye maarifa!
 
I am so proud of my fellow Tanzania on this.
Tumeamka Kwa pamoja na asilimia kubwa tunaongea lugha Moja ya kutetea rasilimali zetu. Tusiwe selfish, tufikirie vizazi vijavyo siku tukiondoka hapa duniani
 
Bunge limeshakubaliana na mpango wa kuwaita wawekezaji kuja kuendesha bandari kwa ufanisi. Heshimuni katiba acheni kazi iendelee
 
Bunge limeshakubaliana na mpango wa kuwaita wawekezaji kuja kuendesha bandari kwa ufanisi. Heshimuni katiba acheni kazi iendelee
Hata ubakaji pia ni kazi! Sasa ni kutumia tu akili kujua ni kazi zipi ziendelee na zipi za kupingwa!
Hili la Bandari kupewa Waarabu kitapeli kupitia viongozi mbumbumbu au hata kwa rushwa hatutakubali.
Hao DP World (Waarabu) walipatikanaje?!
 
Itaingia kwenye rekodi ya kudumu. Bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania 2020-2025 limeridhia kuuzwa kwa bandari zetu bure kwa waarabu wa DP World!! Nasema ni bure maana hawajaainisha manufaa yoyote tutakayopata wala hawajaainisha huyo mwarabu atawekeza kiasi gani cha pesa!! Ukisimuliwa huwezi kuamini lakini ndio ukweli wenyewe!!

Wameenda mbali zaidi wanataka kufanya marekebisho ya sheria inayozuia mgeni kumiliki ardhi ili huyo mwarabu amiliki pia ardhi ambako kuna bandari zetu!! Inatia kisirani sana!! Sultan Mangungo tutasema hakuwa na elimu, je hili bunge lililojaa wasomi tutasemaje? Lazima kuna "kitu kikubwa" wamepewa hawa!! maana si kwa kujitoa ufahamu hivyo!! hawana aibu! Wabunge mtaficha wapi sura zenu!!
 
Back
Top Bottom