Dodoma: Mahakama Kuu Yabaini Upendeleo Kamati ya Taifa ya Maadili ya Mawakili, Yamtaka AG Kuacha Matumizi Mabaya ya Mamlaka

Dodoma: Mahakama Kuu Yabaini Upendeleo Kamati ya Taifa ya Maadili ya Mawakili, Yamtaka AG Kuacha Matumizi Mabaya ya Mamlaka

Abdul Said Naumanga

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2024
Posts
673
Reaction score
1,318
Mahakama Kuu ya Tanzania masijala kuu ya Dodoma imebaini upendeleo katika muundo wa Kamati ya Taifa ya Maadili ya Mawakili (National Advocates Ethics Committee) baada ya Wakili Peter Madeleka kuwasilisha shauri la kikatiba akipinga wajumbe wa kamati hiyo, akidai wana mgongano wa kimaslahi.

Katika kesi hiyo, Madeleka alihoji uwezo wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) kuwa mlalamikaji dhidi yake huku akiwa mjumbe wa kamati hiyo. Mahakama, ikiongozwa na jopo la Majaji Mugeta, Magoiga, na Masabo, ilikubaliana na hoja hii, ikieleza kwamba muundo wa sasa wa kamati unaleta upendeleo ambao unaweza kuhatarisha haki ya kusikilizwa kwa haki.

Mahakama imeeleza kuwa AG hawezi kuwa mlalamikaji na wakati huo huo kuwa sehemu ya chombo kinachosikiliza malalamiko yake. Kwa msingi huo, Mahakama imemtaka AG apeleke malalamiko yake kwenye Kamati ya Maadili ya Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) badala ya Kamati ya Kitaifa ya Maadili ya Mawakili. Pia, AG ameshauriwa kufanya mabadiliko ya muundo wa Kamati hiyo ili kuondoa upendeleo.

Zaidi ya hayo, Mahakama imekemea vikali matumizi mabaya ya mamlaka ya AG katika kufanya marekebisho ya sheria bila kufuata taratibu za kisheria zinazotakiwa kufanywa na Bunge. Mahakama imeonya kuwa vitendo hivyo vinakiuka utawala bora wa sheria na vinapaswa kukoma mara moja.​
IMG_6863.jpeg

IMG_6864.jpeg

IMG_6865.jpeg

IMG_6866.jpeg

IMG_6867.jpeg


KESI KAMILI, soma hapa
 
Mahakama Kuu ya Tanzania masijala kuu ya Dodoma imebaini upendeleo katika muundo wa Kamati ya Taifa ya Maadili ya Mawakili (National Advocates Ethics Committee) baada ya Wakili Peter Madeleka kuwasilisha shauri la kikatiba akipinga wajumbe wa kamati hiyo, akidai wana mgongano wa kimaslahi.

Katika kesi hiyo, Madeleka alihoji uwezo wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) kuwa mlalamikaji dhidi yake huku akiwa mjumbe wa kamati hiyo. Mahakama, ikiongozwa na jopo la Majaji Mugeta, Magoiga, na Masabo, ilikubaliana na hoja hii, ikieleza kwamba muundo wa sasa wa kamati unaleta upendeleo ambao unaweza kuhatarisha haki ya kusikilizwa kwa haki.

Mahakama imeeleza kuwa AG hawezi kuwa mlalamikaji na wakati huo huo kuwa sehemu ya chombo kinachosikiliza malalamiko yake. Kwa msingi huo, Mahakama imemtaka AG apeleke malalamiko yake kwenye Kamati ya Maadili ya Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) badala ya Kamati ya Kitaifa ya Maadili ya Mawakili. Pia, AG ameshauriwa kufanya mabadiliko ya muundo wa Kamati hiyo ili kuondoa upendeleo.

Zaidi ya hayo, Mahakama imekemea vikali matumizi mabaya ya mamlaka ya AG katika kufanya marekebisho ya sheria bila kufuata taratibu za kisheria zinazotakiwa kufanywa na Bunge. Mahakama imeonya kuwa vitendo hivyo vinakiuka utawala bora wa sheria na vinapaswa kukoma mara moja.​
View attachment 3093580
View attachment 3093581
View attachment 3093582
View attachment 3093584
View attachment 3093585

KESI KAMILI, soma hapa
Mbona hii haina tofauti kabisa na Mwenyekiti wa CCM kumchagua Msajili wa vyama vya siasa Tanzania!? Mgongano wa kimaslahi upo mkubwa sana!!
 
Mbona hii haina tofauti kabisa na Mwenyekiti wa CCM kumchagua Msajili wa vyama vya siasa Tanzania!? Mgongano wa kimaslahi upo mkubwa sana!!
Yan hii ni kama jaji anakushtaki alafu kesi yako anaisikiliza na kuiamua mwenyewe.​
 
Back
Top Bottom