Dodoma: Mahakama Kuu yatupilia mbali shauri la mapitio kuhoji Uhalali wa Mawakili kuwatetea waliombaka Binti wa Yombo

Hapo ulipo jirekodi unaichana picha ya samia uone kitakachotokea.....hii ndio Tanzania ambayo mimi huwa naamini mahakama ipo kwa ajili ya wenye pesa na vyeo
 
Watz tuna mihemko mitandaoni tu, ila action ni 0.
Si ajabu hamna hata waliokua wanaenda mahakamani huko zaidi ya kusubiri taarifa mitandaoni tu.
 
Kuna watu humu unasikia wanasema imeisha hiyo. Kwamba kesi imeisha au...? Kesi ya msingi imetajwa hapo. Mnaijua?
 
Hoja yangu,mawakili walitafutwa na wabakaji kuiisimamia kesi au mawakili wamejitolea kufanya hivyo?

Lakini najiuliza hao mawakili wanataka kwenda mahakamani kutetea nini?
 
Mahakama kuu wako sahihi. Hawa ni watuhumiwa. Kuwahukumu bila kufuata sheria ni kuvunja sheria. Na wana haki ya kujitetea ili sheria iwe na mashiko mbele ya umma
 
Muogope Mungu ndugu yangu na weka akiba ya maneno lililotokea kwa mtoto wa mwenzio usishangae likatokea kwa mwanao au wewe ni mkristo?
Watu wanajisahau Sana, chizi huwa anachekesha akiwa hatoki kwenu.
 
Watz tuna mihemko mitandaoni tu, ila action ni 0.
Si ajabu hamna hata waliokua wanaenda mahakamani huko zaidi ya kusubiri taarifa mitandaoni tu.
Kesi ile inasikilizwa faragha (chamber Court) hata waandishi wa habari hawaruhusiwi kuingia.
Kama umeshafuatilia huwa wanasema tu shahidi namba fulani katoa ushahidi wake. Lakini hawaelezi kwa undani.
Kesi za namna ile huwa zinasikilizwa hivyo
 
Kesi ile inasikilizwa faragha (chamber Court) hata waandishi wa habari hawaruhusiwi kuingia.
Kama umeshafuatilia huwa wanasema tu shahidi namba fulani katoa ushahidi wake. Lakini hawaelezi kwa undani.
Kesi za namna ile huwa zinasikilizwa hivyo
Kwanini?
 

Hahahaha hapo vipi, hukumu imetoka rasmi leo. Bado unashikilia unachosema ama unakuja na remix?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…