Dodoma: Makarani wasusia sensa wakidai kutolipwa fedha zao

Dodoma: Makarani wasusia sensa wakidai kutolipwa fedha zao

Hivi kwa nini Rais hatoi matamko katika mambo muhimu yanayogusa wananchi moja kwa moja kama hili zoezi la sensa ambalo limekuwa na dosari na malalamiko mengi toka kuanza kwa mchakato ?

Au amewaachia wenyewe watatazame huku wananchi wakipata maumivu na kuridhia kulalamika?
Bora liende, Kenya waliona haya wakachagua Ruto
 
Waongozaji 90 wa Makarani wa Sensa ya Watu na Makazi 2022, Wilaya ya Chemba Mkoani Dodoma wamesusia zoezi la Sensa ya watu na makazi linaloendelea kote Nchini kwa madai ya kutolipwa fedha zao.

Waongozaji hao wa Makarani wamedai kuwa waliahidiwa kulipwa laki moja kwa awamu mbili lakini hadi kufikia Agosti 28, 2022 hawakuwa wamelipwa.

Mwenyekiti wa Kamati ya Sensa wa Chemba ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Chemba, Samson Chacha alikutana na waongozaji hao wa makarani hao na kuahidi kuwa watalipwa kama walivyokuwa wamepangiwa.

Source: Azam TV
mbaya zaidi nafasi yenyewe umeipata kwa rushwa harafu hata hela yako haijarudi.
 
Waongozaji 90 wa Makarani wa Sensa ya Watu na Makazi 2022, Wilaya ya Chemba Mkoani Dodoma wamesusia zoezi la Sensa ya watu na makazi linaloendelea kote Nchini kwa madai ya kutolipwa fedha zao.

Waongozaji hao wa Makarani wamedai kuwa waliahidiwa kulipwa laki moja kwa awamu mbili lakini hadi kufikia Agosti 28, 2022 hawakuwa wamelipwa.

Mwenyekiti wa Kamati ya Sensa wa Chemba ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Chemba, Samson Chacha alikutana na waongozaji hao wa makarani hao na kuahidi kuwa watalipwa kama walivyokuwa wamepangiwa.

Source: Azam TV
kwa hali hi kupata takwimu sahihi sijuwi.
 
Madelu amepiga dili la barabara ya Uvinza to Malagarasi @ kilometa 1 = Bil 11 na tenda haikutangazwa popote hili lipo wazi kabisa
 
Kuna wilaya pia huku morogoro paka sasa makarani hawajalamba pesa ya kazi wala ya kumaliziwa semina
 
Back
Top Bottom